MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI

Welcome, Guest
You have to register before you can post on our site.

Username
  

Password
  





Search Forums

(Advanced Search)

Forum Statistics
» Members: 5,481
» Latest member: Kundlimatching
» Forum threads: 2,178
» Forum posts: 2,256

Full Statistics

Online Users
There are currently 129 online users.
» 0 Member(s) | 127 Guest(s)
Bing, Google

Latest Threads
Buy Vilitra 60 Mg |【Get E...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-24-2023, 11:45 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce50?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-19-2023, 12:59 PM
» Replies: 0
» Views: 0
About the Vidalista 60 Mg...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-04-2023, 04:07 PM
» Replies: 0
» Views: 0
What Is Vidalista 60?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-03-2023, 10:49 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce 100 ...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
03-29-2023, 02:37 PM
» Replies: 0
» Views: 66
How is Vidalista 10 Mg us...
Forum: Watunzi wa Kiswahili
Last Post: Kieth_winsett
03-27-2023, 01:26 PM
» Replies: 0
» Views: 117
Obtain Thesis Paper Assis...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Minny02
03-24-2023, 03:01 PM
» Replies: 0
» Views: 200
SEO services for sports f...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Maria Poland
03-17-2023, 01:51 PM
» Replies: 1
» Views: 223
NUKUU ZA KISWAHILI DARASA...
Forum: Nukuu
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:31 PM
» Replies: 0
» Views: 788
NECTA K4 2022
Forum: Mitihani
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:25 PM
» Replies: 0
» Views: 403

 
  ETIMOLOJIA YA NENO "BUGHUDHA''
Posted by: MwlMaeda - 08-23-2022, 09:59 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BUGHUDHA''

Neno bughudha katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: i-/zi-] yenye maana ya mambo yanayomkasirisha au kumuudhi mtu, maneno na vitendo vinavyomfanya mtu audhike.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili bughudha linatokana na tendo-jina la Karabu bugh-dhwun بغض lenye maana ya chuki linalotokana na kitenzi cha Kiarabu baghadhwa (soma: baghadhwa/yabghadhwu/bugh-dhwan بغض، يبغض، بغضا)  chenye maana zifuatazo:

1. Kuchukia.

2. Kuchukiza.

3. Kuchukiwa.

Kinachodhihiri ni kuwa neno bugh-dhwun  بغض lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno bughudha lilichukua maana mpya ya maneno na vitendo vinavyomfanya mtu audhike, mambo yanayomkasirisha au kumuudhi mtu.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.

Print this item

  SHAIRI: CHOZI
Posted by: MwlMaeda - 08-23-2022, 08:52 AM - Forum: Ushairi - No Replies

CHOZI
Alipokuwa kufani, pumzi ikimkwama,
Aliniita pembeni, maneno akiyasema,
Sijitie kilioni, machozi ukayafuma,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Hata ukilia sana, useme olele mama,
Bure wajitesa mwana, tatizole litakwama,
Kisha macho yatatuna, aibu kujitazama,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Useme uvue nguo, ukaanza kulalama,
Wala hupati funguo, tatizo kuliandama,
Hakina kitu kilio, wajongezea dhahama,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Kwa tatizo yake dawa, uanze kulisakama,
Mwishowe kulitatatua, kwa busara na hekima,
Wako moyo utapowa, furaha ukiifuma,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Wakati tukifiliwa, mfano baba na mama,
Moyo hutaki kutuwa, machozi hujaa pima,
Vipi wanafufuliwa? mwisho vichwa vyatuuma,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Tupatapo mitihani, ya mabonde na milima,
Mikono huwa kichwani, tulie olele mama,
Mwisho tunapata Soni, kulia mtu mzima,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Nilikuwa bado kinda, alipofariki mama,
Kilio sikukishinda, nililia Kama kinda,
Huku kule nilikwenda, yani aamke mama,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Chozi halikubadili, kwa punje au alama,
Sikuziona dalili, aamke wangu mama,
Ndipo likumbuka mbali, maneno aliyosema,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Siku niliyoamini, chozi halina salama,
Yangu hapo sithamini, kulivisha koja jema,
Machozi ni kitu duni, aminj ninayosema,.
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Kwa heri wanazuoni, ndugu zangu maulama,
Nimefika ukingoni, ndiyo yangu kaditama,
Kulialia ya nini, bure kujitia homa?
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO "BUDI''
Posted by: MwlMaeda - 08-21-2022, 02:38 PM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BUDI''

Neno budi katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: i-/zi-] yenye maana zifuatazo:

1. Jambo la lazima.
Msemo:
Sina budi kusafiri: lazima nisafiri. (Kamusi Kuu ya Kiswahili).

2. Suala linalomlazimu mtu kulitimiza.
Msemo:
Sina budi kuwasilisha mada yangu leo. (Kamusi ya Karne ya 21)

3. Nomino (Msemo) Sina budi kuja kesho: Lazima nitakuja kesho; Hapana budi : lazima. (Kamusi ya Kiswahili Sanifu-TUKI).

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili budi linatokana na neno la Kiarabu buddun (soma: buddun/buddan/buddin بد)  lenye maana zifuatazo:

1. Sehemu ya kitu, mbadala, kutengana.
Waarabu hulitumia neno hili pamoja na herufi laa (لا), yaani: Laa budda لا بد  kwa maana ya: hakuna mbadala, hakuna hiari, hakuna pa kukimbilia.

2. Sanamu, nyumba ya kuhifadhi sanamu.

Kinachodhihiri ni kuwa neno buddun  بد lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno budi lilichukua maana ya Laa budda inayoashiria  'ulazima'  katika Kiarabu lakini wakalipa neno lenyewe ' budi ' maana ya 'lazima' ambayo ikitanguliwa na neno ' hapana ' linaleta maana kinyume na kilichokusudiwa.
Neno ' budi ' lilipaswa kupewa maana ya hiari au kitu mbadala ili linapotanguliwa na neno ' hapana/sina' lilete maana ya ulazima. 

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.

Print this item

  VIJANA JENGENI KWENU
Posted by: MwlMaeda - 08-21-2022, 10:01 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

VIJANA JENGENI KWENU
Yananipata mashaka, kwa vijana wa mijini,
Kwenu mlikoondoka, hivi kuna hali gani?
Nadhani kuna vichaka,  nyoka yake masikani,
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.

Kuna vijana wajanja, ukiwakuta mjini,
Nyumbani hana kiwanja, japo hukesha baani,
Si nyumba hata kichanja, kijana unafanyani?
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.

Kiatu chake thamani, na mavazi ya fasheni,
Utadhani Sultani, kumbe kwao kichakani,
Kutazame kijijini, kijana aibu gani?
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.

Kijana acha aibu, rudi kwenu ukajenge,
Usitafute majibu, hoja yangu uichenge,
Ninaona maajabu, hizo akili za kenge,
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.

Nikitiwa hatiani, kudhani nimepotoka,
Mambo kuwa hadharani, mseme nimeropoka,
Mtunzi nishitakini, mahabusu kuniweka,
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.

Kiwa ni njema kauli, kazi kaifanyieni,
Mlao mbuzi kwa wali, hali kwenu taabani,
Fikirini mara mbili, jipimeni kwa mzani,
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.

Kama kwenu hukujenga, nawe raha unaponda,
Wala hujapata kinga, kupona hiki kidonda,
Shairi likupe mwanga, kwenu ukajenge nenda,
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.


Sasa shairi nafunga, haya shime kijijini,
Dhamira kwetu kujenga, initiayo huzuni,
Japo mkono napunga, hatua zikuchueni,
Kwenu jengeni jamani, nawausia vijana.

Mtunzi: Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO "BINAMU''
Posted by: MwlMaeda - 08-14-2022, 09:46 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BINAMU''

Neno *binamu* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: a-/wa-*] yenye maana ya mtoto wa kike au wa kiume wa shangazi au mjomba.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *binamu* limechukuliwa kutoka maneno mawili ya Kiarabu *bun (ibnu) بن/ابن na ammi (soma: ammun/amman/ammin عم).* 

Neno *ibnu/bnu بن/ابن* lina maana ya mtoto wa kiume. Unaposema: Khamis bun Said, maana yake ni: Khamis mtoto wa kiume wa Said.

Watu wa Mauritania badala ya neno *bun بن* wao hutumia neno *walad ولد* neno la Kiarabu lenye maana ya mtoto wa kiume. Yaani: *Khamis bun Said* Wa-Mauritania husema: *Khamis Walad Said.*

Na neno *ammun عم* lina maana ya ndugu wa kiume wa baba.

Neno hilo pia lina maana ya kundi la watu wengi, majani (nyasi) na mtende mrefu.

Kinachodhihiri ni kuwa maneno ya Kiarabu *'ibnu ammi  ابن عم* yenye maana ya mtoto wa kiume wa ndugu wa kiume wa baba yalipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *binamu* yalichukua maana mpya ya mtoto wa kike au wa kiume wa shangazi au mjomba.

*TANBIHI:*
Katika lugha ya Kiarabu neno *ibnu* hutumika katika lugha ya mafumbo kama vile:
1. *Ibnus Swulbi ابن الصلب* (mtoto wa uti wa mgongo) kwa maana ya mtoto halisi/mtoto halali kisheria.
2. *Ibnu Amsi/Albaariha ابن امس/البارحة* (mtoto wa jana) kwa maana ya mtu asiye na tajriba ya maisha.
3. *Ibnu Batwinihi ابن بطنه* (mtoto wa tumbo lake) kwa maana ya mchumia tumbo.
4. *Ibnu Jalaa ابن جلا* (mtoto wa wanja)  kwa maana ya mtu mashuhuri maarufu.
5. *Ibnul Balad ابن البلد* (mtoto wa mjini) kwa maana ya mtu anayeishi katika mji aliozaliwa na kukulia.
6. *Ibnul Halaali ابن الحلال* (mtoto wa halali) kwa maana ya mtoto aliyezaliwa ndani ya ndoa ya kisheria.

Katika lugha ya Kiarabu, shangazi huitwa *ammat عمة* na mtoto wa shangazi huitwa *ibnu ammat ابن عمة* na mjomba huitwa *khaalun خال* na mtoto wa mjomba huitwa *ibnu Khaalin ابن خال.*

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  MASUALA YA KISARUFI KATIKA MAGAZETI YA MITAANI YA KISWAHILI - TANZANIA
Posted by: MwlMaeda - 08-09-2022, 07:48 AM - Forum: Sarufi na Utumizi wa lugha - No Replies


.pdf   MASUALA YA KISARUFI KATIKA MAGAZETI YA MITAANI YA KISWAHILI - TANZANIA.pdf (Size: 153.26 KB / Downloads: 0)

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO "BILADI ''
Posted by: MwlMaeda - 08-08-2022, 08:08 PM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - Replies (1)

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BILADI ''

Neno *biladi* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya *mji* .

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *biladi* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'bilaad* *(soma: bilaadun/bilaadan/bilaadin  بلاد)** likiwa ni wingi wa neno la Kiarabu *baldah (soma: baldatun/baldatan/baldatin بلدة)* lenye maana zifuatazo: 

1. Eneo kubwa la ardhi.

2. Eneo maalumu la ardhi wanalokaa watu fulani lenye miji, vijiji na mipaka inayotambulika; *nchi*.
*Yaa baladii, yaa bilaadii يا بلادي، يا بلدي* Ee nchi yangu!

3. Sehemu ya nchi au mji.

4. Mji mdogo.

5. Chanzo.

Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *'bilaadun  بلاد*  lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *biladi* lilichukua kutoka lugha ya Kiarabu maana ya *mji* na kuziacha maana nyingine.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO SHUKURANI ''
Posted by: MwlMaeda - 08-06-2022, 08:54 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO SHUKURANI ''

Neno *shukurani* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya maneno yanayotolewa kuonesha kuupokea kwa mikono miwili wema uliotendewa; *ahsante/asante.*

*Nahau* : *Toa shukurani:* sema ahsante.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *shukurani* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'shukraan* *(soma: shukraanun/shukraanan/shukraanin  شكران)**  tendo-jina  *Masdar مصدر* la *kitenzi* cha Kiarabu *shakara شكر* chenye maana zifuatazo:

1. Amemsifu na kumtaja mtu mwengine kwa wema kutokana na hisani aliyomfanyia.

2. Amemlipa mtu mwengine malipo fulani kwa kuifanya vizuri kazi aliyomtuma.

Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *'shukraanun  شكران*  lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *shukurani* halikubadili maana katika lugha ya Kiarabu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO 'BIASHARA'
Posted by: MwlMaeda - 08-05-2022, 11:27 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BIASHARA'

Neno *biashara* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya mchakato wa kununua na kuuza mali au vitu.
*Biashara sukutu*: aina ya uuzaji na ununuaji wa bidhaa bila maongezi.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *biashara* limechukuliwa kutoka maneno mawili ya  Kiarabu  *'bay-un* *(soma: bay-un/bay-an/bay-in  بيع)**  na *'shiraau* *(soma: shiraaun/shiraa-an/shiraain    شراء)**  yenye maana zifuatazo:
*Bay-un* ni:
1. Tendo-jina *Masdar مصدر* ya kitenzi cha Kiarabu *baa-a  باع* chenye maana ya *ameuza* .

2. Kitendo cha kuchukua kitu na kulipa thamani yake.

3. Kitendo cha kutoa kitu na kuchukua thamani yake.

4. Bidhaa za kuuzwa. 

Na *shiraau  شراء* ni:

1. Kitendo cha kutaka kununua kitu na kulipa thamani yake.

2. Mahali pa kuuza na kununua; *suuq سوق*, *soko* .

Kinachodhihiri ni kuwa maneno mawili ya Kiarabu *'bay-un wa shiraa بيع و شراء* yalipoingia katika Kiswahili na yalitoholewa kuwa neno *biashara* na neno hili la Kiswahili halikubadili maana ya msingi ya maneno hayo ya Kiarabu, kuuza na kununua.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  JANGA SUGU LA WAZAWA
Posted by: MwlMaeda - 07-30-2022, 08:41 PM - Forum: Riwaya - No Replies


.docx   JANGA SUGU LA WAZAWA.docx (Size: 29.96 KB / Downloads: 6)

Print this item