MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI

Welcome, Guest
You have to register before you can post on our site.

Username
  

Password
  





Search Forums

(Advanced Search)

Forum Statistics
» Members: 5,481
» Latest member: Kundlimatching
» Forum threads: 2,178
» Forum posts: 2,256

Full Statistics

Online Users
There are currently 143 online users.
» 0 Member(s) | 140 Guest(s)
Bing, Facebook, Google

Latest Threads
Buy Vilitra 60 Mg |【Get E...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-24-2023, 11:45 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce50?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-19-2023, 12:59 PM
» Replies: 0
» Views: 0
About the Vidalista 60 Mg...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-04-2023, 04:07 PM
» Replies: 0
» Views: 0
What Is Vidalista 60?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-03-2023, 10:49 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce 100 ...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
03-29-2023, 02:37 PM
» Replies: 0
» Views: 66
How is Vidalista 10 Mg us...
Forum: Watunzi wa Kiswahili
Last Post: Kieth_winsett
03-27-2023, 01:26 PM
» Replies: 0
» Views: 117
Obtain Thesis Paper Assis...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Minny02
03-24-2023, 03:01 PM
» Replies: 0
» Views: 200
SEO services for sports f...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Maria Poland
03-17-2023, 01:51 PM
» Replies: 1
» Views: 223
NUKUU ZA KISWAHILI DARASA...
Forum: Nukuu
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:31 PM
» Replies: 0
» Views: 788
NECTA K4 2022
Forum: Mitihani
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:25 PM
» Replies: 0
» Views: 403

 
  SHAIRI: HANI NIPO KITANDANI
Posted by: MwlMaeda - 07-30-2022, 02:16 PM - Forum: Ushairi - No Replies

HANI NIPO KITANDANI
haloo!hanii halo, Rwaka hani wasikia?
Ndio hapo sawa halo, vipi unaendelea?
Tatizo nililonalo, lazizi ninaugua,
Hani nipo kitandani, taabani hali yangu.

Wala sijahama njia, nitafika huko Rwanda,
Ikinijia afia, na wangu mwili kuwanda,
Basi huko nitatua, unione mie kinda,
Sasa nipo kitandani, taabani hali yangu.

Ila ninayo pumzi, bado moyo unahema,
Bora nikweleze wazi, kinifanyacho kukwama,
Matatizo ya uzazi, ndiyo yaloniandama,
Jua nipo kitandani, taabani hali yangu.

Ina machungu dunia, na mie yamenikuta,
Nusu niage dunia, kwa tumbo kunikeketa,
Japo nimeamkia, bado najivutavuta,
Ila nipo kitandani, taabani hali yangu.

Maradhi yanaghasia, Karagama sikiliza,
Yakishakuangukia, dira unaipoteza,
Mwilini nimelegea, vile nimepata siza,
Love nipo kitandani, taabani hali yangu.

Nitahama nikipona, Tanzania sitarudi,
Na wewe tukionana, itatulia fuadi,
Ila sasa raha sina, Darling I feel bad,
Vile nipo kitandani, taabani hali yangu.

Namshukuru Karima, ningali hai mpenzi,
Ninaungoja uzima, japo kutwa nakuenzi,
Ningelikufa mapema, ungelipata simanzi,
Hapa nipo kitandani, taabani hali yangu.

Na mie napata ganzi, nikikukosa kijana,
Heri kunipiga konzi, utosini nitapona,
Sitahimili majonzi, na wewe tukikosana,
Japo nipo kitandani, taabani hali yangu.

Maumivu yamezidi, yanikataza kutunga,
Kuacha imenibidi, utungo huu kufunga,
Ila ninakuahidi, huko Rwanda nitatinga,
Nikitoka kitandani, iwe njema hali yangu.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO 'BALAGHAMU/BELGHAMU'
Posted by: MwlMaeda - 07-29-2022, 07:56 PM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BALAGHAMU/BELGHAMU'

Neno *balaghamu/belghamu* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: li-/ya-*] yenye maana ya kioevu kizito kilichochanganyika na utandoute kinachotolewa kwa wingi kwa njia ya kupumulia hususan mtu anapougua mafua au kikohozi, mate mazito yanayokuwa kooni ambayo hutoka mtu anapokohoa.

*Msemo:* *Toa balaghamu zako*: toa hasira zako.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *balaghamu/belghamu* limechukuliwa kutoka neno la  Kiarabu  *'balghamu* *(soma: balghamun/balghaman/balghamin  بلغم)**  lenye maana ya mate yaliyochanganyika na kamasi na hutoka kwa njia ya upumuaji, dutu laini ya mate iliyochanganyika na kamasi; *kohozi*.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *'balghamun بلغم* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *balaghamu/belghamu* halikubadili maana katika lugha asili- Kiarabu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  MAANA YA METHALI
Posted by: MwlMaeda - 07-29-2022, 08:04 AM - Forum: Semi - No Replies

MAANA YA METHALI
Wataalamu mbalimbali wamejaribu kutoa fasili ya maana ya methali. Mazrui na Syambo (1992), methali ni misemo mifupi yenye hekima fulani. Wamesisitiza kuwa methali hudhihirisha mkusanyiko wa mafunzo waliyopata watu wa vizazi vingi vya jumuiya wanayoishi katika maisha yao. Aidha, wameongeza kusem kuwa methali ni sehemu moja ya lugha inayoweza kubaini falsafa ya watu fulani kuhusu maisha kwa ujumla.
Ngole na Honero (1981), wamesema kuwa methali ni aina ya usemi mzito na ambao unakusudiwa kusema jambo maalumu kwa njia ya fumbo. Methali hukusudiwa kumuonya, kumuongoza na kumuadilisha mwanadamu katika maisha yake. Aidha, kwa umbile la nje methli huwa na muundo wa pande mbili. Upande mmoja wa methali hueleza mazoea au tabia ya watu au kitu katika utendaji wa jambo. Upande wa pili wa methali hueleza matokeo yaliyosababishw na mazowea au tabia iliyoelezwa katika upande wa kwanza.
Murega (2015), ameona kuwa methali ni semi fupi ya kimapokeo yenye muundo mahsusi na iliyo na fumbo amblo linapofasiliwa  hupata maana mbalimbali hutegemea muktadha na hali halisi ya maisha ya watumiaji.
Wamitila (2001), ameeleza kuwa methali ni msemo unaojitosheleza, wenye maana yenye nguvu au uzito, wenye muundo au sifa za kishairi, unaokusudiwa kuadibu au kuelekeza, kuelimisha, kushauri na kadhalika.
Kutokana na fasili za wataalamu hao, tunaweza kusema kuwa methali ni aina ya usemi mzito unaoelezea wazo pana kwa muhtasari ukiwa na umbo mahsusi na unaotumia uzowefu wa jamii kuonya, kuadilisha na kufunza kwa kuzingatia miktadha maalumu. Methali hutumia hekima, uficho wa kauli, usanii w kimsamiati, uzowefu wa matukio katika jamii na falsafa ya jamii katika mitazamo ya masuala mbalimbali ambayo huakisi maisha na utamaduni wa jamii husika.

Print this item

  SHAIRI: UCHAWI
Posted by: MwlMaeda - 07-27-2022, 10:17 PM - Forum: Ushairi - No Replies

UCHAWI
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi,
Huko awako gizani, mbona ya Mana hayawi,
Pasi na nguo mwilini, lake baridi mchawi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mchawi hupenda tabu, hapendi mambo rahisi,
Kona anaziharibu, apite kwa wasiwasi,
Mlangoni hajaribu, apite kwa urahisi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Yake kazi kuharibu, akageuza kizazi,
Ili unapojaribu, huoni chako kizazi,
Hapo hawana sababu, mambo yao ni ushenzi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Japo yu mtu mkubwa, chamani kuheshimika,
Tabiaye kama mbwa, anapotaka kuruka,
Na baridi atakumbwa, hana nguo kujivika,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Juzi nilipata kesi, mtu katiwa kifafa,
Matabibu na manesi, wakadhani amekufa,
Mwisho katoa kamasi, tukagundua hajafa,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mchawi akifahamu, una kitu kumzidi,
Jua umejipa sumu, kukuroga hana budi,
Utateswa kwa awamu, ukuishe ukaidi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Msiwaone vichaa, kidhani yote ya Mumba,
Wengine tukashangaa, ovyo waanza kuimba,
Wachawi walishakaa, kuchanganya mitishamba,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mtu umesoma sana, Mara vyeti huvioni,
Kumbe walishagawana, watandike kaburini,
Miaka kazi hauna, uchawi ni ushetani,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Machawi yake hasara, ulie yeye acheke,
Wala haimpi fora, hadharani asifike,
Kiumbe mwenye mikwara, japo asifaidike,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mchawi mtu wa ila, mambo yake ni kinyume,
Usiku sie twalala, yu uchi atutazame,
Na hawi tajiri wala, kiwa wongo na aseme,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Sasa ninafunga beti, utungo siendelezi,
Msijenishika shati, ati nimewapa kazi,
Naona bora niketi, kuandika nimesizi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO 'BEDUI/BEDAWI'
Posted by: MwlMaeda - 07-26-2022, 07:32 PM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BEDUI/BEDAWI'

Neno bedui/bedawi katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: a-/wa-, wingi: mabedui/mabedawi] yenye maana zifuatazo:

1. Mtu wa jamii ya Waarabu anayeishi jangwani au karibu na jangwa.

2. Mtu katili asiyemwonea mwenzie huruma.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili bedui/bedawi limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  'badawiyyun (soma: badawiyyun/badawiyyan/badawiyyin  بدوي)*  lenye maana zifuatazo:

1. Mkazi wa eneo la jangwani lililowekwa makazi, malisho na panapopatikana maji.

2. Mtu anayelinda na kuendelea na utamaduni wake wa asili.   

Kinachodhihiri ni kuwa neno 'badawiyyun بدوي lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno bedui/bedawi halikubadili maana yake ya mkazi wa jangwani katika lugha asili- Kiarabu, likaacha maana ya mtu anayehifadhi na kuendelea na utamaduni wake wa asili na likachukua maana mpya ya mtu katili asiyemwonea mwenzie huruma.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.

Print this item

  SHAIRI: NAINGOJA SIMU YAKO
Posted by: MwlMaeda - 07-25-2022, 08:26 PM - Forum: Ushairi - No Replies

NAINGOJA SIMU YAKO
Nimeamka mapema, nimekaa kitandani,
Mawazoni nimezama, ninakuwaza mwandani,
Fikira zimenihama, nipo kwako ewe hani,
Naingoja simu yako!

Mara nasimama wima, ghafla nakaa chini,
Mpenzi nashika tama, bila wewe mimi nyani,
Wewe wangu maulama, wanitia tulizoni,
Naingoja simu yako!

Usidhani nalalama, nijinadani mnadani,
Moyo wangu unauma, Mimi nicheze na nani?
Au simu ulizima, upo kwea kitandani?
Naingoja simu yako!

Sio mwingi wa lawama, nakuomba samahani,
Kwakowe nimetuama, kama somba mtungoni,
Haki kwako nimekwama, mithili mwiba kooni,
Naingoja simu yako!

Basi uamke vema, pasi mavune mwilini,
Nakungoja mtu mwema, unijuze hali gani,
Hamu bado hijakoma, kukusubiri mwendani,
Naingoja simu yako!

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704

Print this item

  MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA 50
Posted by: MwlMaeda - 07-25-2022, 09:12 AM - Forum: Riwaya - No Replies


.pdf   Maisha Yangu na Baada ya Miaka Hamsini (Shaaban Robert) (z-lib.org).pdf (Size: 16.8 MB / Downloads: 18)

Print this item

  NYERERE NA SAFARI YA KANAANI
Posted by: MwlMaeda - 07-24-2022, 09:04 AM - Forum: Tamthiliya - No Replies

Oktoba, 1966 kulizuka mgogoro mkubwa wa kihistoria kati ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Muhimbili. Wanafunzi hawa walifanya maandamano makubwa hadi Ikulu wakipinga vikali sera ya kuwataka wajiunge na Jeshi la kujenga Taifa (JKT). Wasomi hawa walilalama kwa hasira wakisema, "afadhali wakati wa mkoloni kuliko serekali ya Nyerere. Mkitulazimisha basi tutaenda KIMWILI, lakini MIOYO yetu, asilani, haitaenda JKT..." Katika kuukabili upinzani huu, Mwalimu, katika ile hotuba maarufu: "Tanzania itajengwa na wenye moyo" aliwacharaza viboko baadhi ya wasomi hao kadamnasi na kuwafukuza takribani wanafunzi 400 warudi kwao, wakalime! Mwandishi anatudokeza, miongoni mwa masuala mengine kuwa: Mgogoro huu wa 1966, ulichangia katika kukuza mimba ya safari ya Kanaani nchi ya asali na maziwa.Hapana shaka kuwa tamthiliya hii, iliyoandikwa kwa ustadi kabisa, ni kitabu muhimu kwa wanasiasa, wasomi na wapenzi wote wa fasihi ya Kiswahili.

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO 'BAYANI'
Posted by: MwlMaeda - 07-24-2022, 08:52 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BAYANI'

Neno *bayani* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/i-*] yenye maana ya *stadi mojawapo katika mafunzo ya lugha ya Kiarabu  inayohusu ujuzi wa kuzungumza.*

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *bayani* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'bayaan* *(soma: bayaanun/bayaanan/bayaanin  بيان/البيان)**  lenye maana zifuatazo:

1. Maelezo kuhusu bidhaa anayoyatoa mzalishaji wa bidhaa au wakala/muuzaji wake yanayoweka wazi aina ya bidhaa, kiwango chake, uzito wake na hata utumiaji wake.

2. Ubini wa mtu asiyejulikana asili na nasaba yake; *bin bayyaan بن بيان.* 

3. Ufasaha wa kulieleza jambo fulani.

4.  Taarifa itolewayo baada ya kikao cha pande mbili, *bayaanum mushtarikun بيان مشترك.*

5. Taaluma ya lugha ya Kiarabu ya kuelezea maana moja kwa njia tofauti kama vile *tashbihiتشبيه , majazi مجاز  na kinaya كناية.*

Kinachodhihiri ni kuwa neno *'bayaanun بيان* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *bayani* halikubadili maana yake katika lugha asili- Kiarabu.

*TANBIHI:*
Bayani, Kiarabu *Bayaan/Al-Bayaan البيان* ni moja ya fani za *Balaagha ya Kiarabu*, taaluma ya ufasaha wa kusema na kutia madoido. 

Fani nyingine mbali ya *ALBAYAAN  البيان (Rhetoric)* , ni *ALMAAN المعاني (Semantic)* na *ALBADII'I البديع (The Art of Figures of Speech/The Art of Metaphors and Stylistics/Good Style).*

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  SHAIRI: NIMPENDE NANI ?
Posted by: MwlMaeda - 07-22-2022, 06:23 AM - Forum: Ushairi - No Replies

NIMPENDE NANI ?

Mwenzenu nipeni rai kwa haya yalonifika
Moyo wangu haukai, kwa hapa nilipofika
Japo naona nishai,  moyoni nimewatika
Kati ya hawa wawili, Nipende nani zaidi?

Huyu  wa kwanza mpole ,  tena si muongeaji
Kama simba mwenda pole, kwenye ufatiliaji 
Hutembea polepole ,amdake mwiwindwaji
Kati ya huyu nayule jama  nimpende nani?

Huyu wa pili  mweusi , kapanda juu kidogo
Mwenye pua ya kitusi,  mwili mwembamba kidogo
Mtalamu wa kukisi,utadhania mgogo
Kati ya huyu na yule ,jama  nimpende nani?

Akili inanituma , wa pili awe mwandani
Ninategemea mema ,sitotoka asilani
Kama ikiwa salama ,nitasota uvunguni
Kati ya hawa wawili Nimpende nani?

Nilikuwa na furaha,nimefika maskani
Nikayaanza madaha, nikavipata vya ndani
Nilishazika karaha,ninapokuwa chumbani
Alivyokuja wa pili , Moyo wangu umeshindwa

Wa pili yeye mcheshi , muda wote tabasamu
Ni kweli kuwa achoshi ,twacheka kama binamu
Kwangu hamu haiishi, jama mpeni salamu
Kati ya Hawa wawili nimpende nani?

Wa kwanza ananijali, kwa pesa nayo mahaba
Nikimuuzi hajali,  hunilea kama baba
Na hunijulia hali,  upendowe sio haba
Wanagenzi mnijuze nimpende yupi?

Rama  karibu javini ,  unipe  jibu murua
Na wengine karibuni, jibu nataka kujua
Nitomuweka moyoni,  kofuli kumfungia
Kitendawili tegua  Yupi kwangu anafaa?

DINNA ( MOM J )
21/7/22
KUWA TAYARI KUHESABIWA
MPE USHIRIKIANO KARANI WA SENSA??

Print this item