ETIMOLOJIA YA NENO 'BIASHARA' - Printable Version +- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz) +-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1) +--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16) +--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO 'BIASHARA' (/showthread.php?tid=2799) |
ETIMOLOJIA YA NENO 'BIASHARA' - MwlMaeda - 08-05-2022 HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BIASHARA' Neno *biashara* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya mchakato wa kununua na kuuza mali au vitu. *Biashara sukutu*: aina ya uuzaji na ununuaji wa bidhaa bila maongezi. Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *biashara* limechukuliwa kutoka maneno mawili ya Kiarabu *'bay-un* *(soma: bay-un/bay-an/bay-in بيع)** na *'shiraau* *(soma: shiraaun/shiraa-an/shiraain شراء)** yenye maana zifuatazo: *Bay-un* ni: 1. Tendo-jina *Masdar مصدر* ya kitenzi cha Kiarabu *baa-a باع* chenye maana ya *ameuza* . 2. Kitendo cha kuchukua kitu na kulipa thamani yake. 3. Kitendo cha kutoa kitu na kuchukua thamani yake. 4. Bidhaa za kuuzwa. Na *shiraau شراء* ni: 1. Kitendo cha kutaka kununua kitu na kulipa thamani yake. 2. Mahali pa kuuza na kununua; *suuq سوق*, *soko* . Kinachodhihiri ni kuwa maneno mawili ya Kiarabu *'bay-un wa shiraa بيع و شراء* yalipoingia katika Kiswahili na yalitoholewa kuwa neno *biashara* na neno hili la Kiswahili halikubadili maana ya msingi ya maneno hayo ya Kiarabu, kuuza na kununua. *Shukran sana.* *Khamis S.M. Mataka.* |