MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI

Welcome, Guest
You have to register before you can post on our site.

Username
  

Password
  





Search Forums

(Advanced Search)

Forum Statistics
» Members: 5,481
» Latest member: Kundlimatching
» Forum threads: 2,178
» Forum posts: 2,256

Full Statistics

Online Users
There are currently 146 online users.
» 0 Member(s) | 144 Guest(s)
Bing, Google

Latest Threads
Buy Vilitra 60 Mg |【Get E...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-24-2023, 11:45 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce50?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-19-2023, 12:59 PM
» Replies: 0
» Views: 0
About the Vidalista 60 Mg...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-04-2023, 04:07 PM
» Replies: 0
» Views: 0
What Is Vidalista 60?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-03-2023, 10:49 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce 100 ...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
03-29-2023, 02:37 PM
» Replies: 0
» Views: 66
How is Vidalista 10 Mg us...
Forum: Watunzi wa Kiswahili
Last Post: Kieth_winsett
03-27-2023, 01:26 PM
» Replies: 0
» Views: 117
Obtain Thesis Paper Assis...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Minny02
03-24-2023, 03:01 PM
» Replies: 0
» Views: 200
SEO services for sports f...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Maria Poland
03-17-2023, 01:51 PM
» Replies: 1
» Views: 223
NUKUU ZA KISWAHILI DARASA...
Forum: Nukuu
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:31 PM
» Replies: 0
» Views: 788
NECTA K4 2022
Forum: Mitihani
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:25 PM
» Replies: 0
» Views: 403

 
  NECTA 2022 KISWAHILI 2
Posted by: MwlMaeda - 07-21-2022, 02:26 PM - Forum: Mitihani - No Replies


.pdf   NECTA 2022 KISW 2.pdf (Size: 722.15 KB / Downloads: 40)

Print this item

  NECTA 2022 KISWAHILI 1
Posted by: MwlMaeda - 07-21-2022, 02:22 PM - Forum: Mitihani - No Replies


.pdf   NECTA 2022 KISW 1.pdf (Size: 962.96 KB / Downloads: 39)

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO 'BASHASHA'
Posted by: MwlMaeda - 07-18-2022, 06:33 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BASHASHA'

Neno *bashasha* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:

1. Hali ya kuonesha furaha; ucheshi, uchangamfu.

2. Furaha na uchangamfu.

*Mfano:* Mgeni rasmi alipokelewa kwa bashasha kubwa.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *bashasha* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'bashaasha* *(soma: bashaashatun/bashaashatan/bashaashatin  بشاشة)**  lenye maana zifuatazo:

1. Tendo-jina *masdar  مصدر* la kitenzi cha Kiarabu *bash-sha  بش* chenye maana ya: *amekunjua uso wake, amemfurahikia aliyekutana naye, amempa faraja.*

2. Hali ya kumlaki mtu kwa furaha na kicheko.

3. Uso mkunjufu uliojaa furaha na tabasamu. 

Kinachodhihiri ni kuwa neno *'bashaashatun بشاشة* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *bashasha* halikubadili maana yake katika lugha asili- Kiarabu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  MAENDELEO YA KISWAHILI BAADA YA UHURU NA CHANGAMOTO ZAKE
Posted by: MwlMaeda - 07-15-2022, 11:35 AM - Forum: Maendeleo ya Kiswahili - No Replies


.pptx   ppt.pptx (Size: 958.52 KB / Downloads: 11)

Print this item

  Baba alivyookoa ndoa ya kijana wake
Posted by: MwlMaeda - 07-13-2022, 07:42 AM - Forum: Je, wajua ? - No Replies

Baba alivyookoa ndoa ya kijana wake
Iko hivi, katika familia moja yenye mabinti watatu na kijana mmoja wa pekee wa kiume siku moja paliingia tafrani. Kijana wa familia alipofikia umri wa kuoa wazazi na dada zake walihakikisha kijana mpendwa wao anapata mke wa ndoto zake lakini jukumu la kumtafuta mke mwenyewe likawa la muoaji.
Kijana hatimaye aliamua kumtambulisha binti mmoja aliyekuwa naye katika mahusiano kwa muda uliotosha kuwashawishi wote kujiona kila mmoja ameumbwa kwa ajili ya mwenzake.
Baada ya kutambulishana hatua za kuhalalisha uhusiano wao zilianza na hatimaye wakafunga pingu za maisha wakawa mke na mume halali. Mungu akawajalia watoto wawili katika ndoa yao.
 Kadiri siku zilivyosonga wakazidi kuzoeana na mauzauza ya ndani ya ndoa yakaanza kujitokeza kama ilivyokawaida ya vijana wengi wakishazoeana katika ndoa. Makandokando huwa hayakoseni. Mume akaanza vituko mara kuchati kwingi, kuchelewa kurudi na mwisho hata mapenzi kwa mkewe yakawa haba tofauti na ilivyokuwa awali. Katika hali hiyo mke akagundua dhahiri kuna jambo zi bure.
Uvumilivu ulipomshinda mke naye akaona isiwe tabu bora ajiliwaze kwa namna inayomfaa. Hapo mke naye akajipatia kiben ten wake akawa wanapeana raha duniani. Mapenzi kama kikohozi huwezi kukificha. Wakanogewa mpaka mume akagundua na hapo mfumo dume ukajidhihirisha waziwazi kuwa kuchepuka achepuke mume si mke.
Mume alipojiridhisha kwa Ushahidi alionao, siku ya siku akaikusanya familia yake na kwenda kwa wzazi wake. Kufika huko tena akaitisha kikao, ndugu wote wakakusanyika kusikiliza neno la kijana wao wa pekee mpendwa.
Hatimaye kijana akatumbua jipu na kumwaga ushahidi alionao licha ya ushahidi kuwa wa maneno matupu. Mama wa kijana na dada wa kijana hawakutaka kusikiliza la mkwezi wala mfua madafu macho na vidole vyao vikawa juu ya mke wa kijana wao huku wakimtuhumu na kumshutumu kwa maneno makali. “Unataka kutuulia kaka yetu, malaya mkubwa wewe.” Binti wa watu hakutia neno akaamua machozi yamtetee tu.
Wakati hayo yote yakiendelea baba wa kijana alikuwa kimyaaaaaa akitafakari nini cha kufanya. Waswahili wanasema utu uzima dawa. Baada ya muda baba akasema, haya tumekusikia kijana wetu hebu na wewe bitni yangu tueleze una lipi la kusema juu ya tulichoelezwa? Binti yule kwa sauti ya chini sana akasema baba kama anayoyasema ni kweli basi Mungu atajua.
Baada ya kimya kirefu baba wa kijana akasema haya sasa naomba mnisikilize. Kwanza, wewe kijana wangu urudi kwako huyu mkeo na watoto wabaki hapa. Pili, leo hiihii nitasafiri kwenda kutafuta dawa ya kumaliza tatizo hili. Kisha kusema hayo baba akaondoka kwenda alikokuita safari. Huku nyuma binti yule aliishi pale kwa mateso makali na manyanyaso mengi lakini alivumilia akisubiri muujiza utakaoletwa na baba mkwe wake.
Baada ya siku mbili kupita baba yule alirejea nyumbani na kuita tena familia yake yote. Hapo akatoa rai kuwa huko alikokwenda amefanikiwa kupata dawa ya kumaliza tatizo la ndoa ya kijana wao lakini dawa yenyewe inatakiwa kuandaliwa na mtu “safi” na hasa ndugu wa damu. Hapo akamuomba mama mzazi atayarishe dawa hiyo. Mama mzazi wa kijana aliruka futi mia moja akikataa kutayarisha dawa hiyo kwa kuhofia masharti ya “usafi” uliosemwa na baba.
Mpira ukarushwa kwa dada mkubwa wa kijana, naye akaruka na kukataa kabisa kuandaa dawa hiyo kwa kuhofia madhara yanayoweza kumkuta kwani naye hakuwa “safi” kama sharti la dawa linavyotaka.
Baada ya ndugu wote wa kijana kukataa kuandaa dawa baba wa kijana akaamuru wote waondoke na wamuache yeye na kijana wake. Walipoondoka wote baba akamgeukia kijana wake na kumuuliza, “Vipi mwanangu umejifunza nini?” Kijana akajibu nimegundua kumbe hata wewe ni uvumilivu tu ndio unakuweka na mama bila, kumbe hata mama anachepuka!
Baba akamwambia kijana wake, “mchukue mkeo mkaendelee na maisha yenu”.
Je, na wewe umejifunza nini?
 

Print this item

  MOKU DSM KIDATO CHA 4 JULAI 2022
Posted by: MwlMaeda - 07-11-2022, 10:05 AM - Forum: Mitihani - No Replies


.pdf   MOKU DSM KIDATO CHA 4 JULAI 2022.pdf (Size: 1.28 MB / Downloads: 46)

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO 'BAHASHISHI'
Posted by: MwlMaeda - 07-11-2022, 08:05 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BAHASHISHI'

Neno *bahashishi* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:

1. Kitu anachopewa mtu kama zawadi kwa kazi nzuri aliyoifanya.

2. Malipo ya ziada anayopewa mtu baada ya kupewa mshahara wake; nyongeza anayopewa mtu kama shukurani.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *bahashishi* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'bakhshiishi* *(soma: bakhshiishun/bakhshiishan/bakhshiishin  بخشيش)** yenye maana zifuatazo:

1. Malipo yatolewayo kwa mtu kama zawadi na Shukurani kwa kazi aliyoifanya. Kiarabu huitwa pia *ikraamiyyah إكرامية* pia *hadiyyah هدية.*

2. Malipo yatolewayo kwa mtu ili kumshawishi; rushwa.

3. Zawadi, hiba.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *'bakhshiishun بخشيش* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *bahashihi* halikubadili maana zake katika lugha asili- Kiarabu.

*TANBIHI:*
Neno *bakhshiishun* linachukuliwa kuwa lahaja ya Kiarabu ya Kimisri na kwa Kiarabu Fasaha na Sanifu neno hili hutamkwa *baqshiishun بقشيش* kwa herufi *q* badala ya *kh* .

Etimolojia ya neno hili ni lugha ya Kiajemi ambapo lilipohamia katika lugha ya *ki-Turky* lilitamkwa *bahsis* na ndipo walipolichukua Waarabu wakati wa Utawala wa Ottoman.

Kwa Waturuki bahsis (bahashishi)  ilikuwa ni ada anayotoa mteja anapoingia sokoni kama ishara ya kuwashukuru wanaolihudumia soko kwa kuliweka katika hali ya usafi, kuvutia na kulisimamia vizuri.

Kisha maana ya *bahashishi* ikageuka kuwa zawadi, hiba na sadaka inayokuza mtangamano wa kijamii na kuchukuliwa kama ukarimu unaowasaidia wale wenye kipato kidogo.

Kadiri neno *bahshishi* ilipotamalaki likafungamana na utoaji wa huduma nzuri na ikawa ni kitu cha lazima na kuchukuliwa kuwa aina mojawapo ya rushwa.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  Je wafahamu misingi iliyowezesha Kiswahili kuadhimishwa 7/7?
Posted by: MwlMaeda - 07-08-2022, 04:24 PM - Forum: Kiswahili Kimataifa - No Replies

Mkutano Mkuu wa 41 wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO tarehe 23 mwezi huu wa Novemba mwaka 2021 ulipitisha azimio namba 41C/61 la kutangaza tarehe 7 mwezi Julai kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

SOMA KWA KINA HAPA >>>>>>>>

Print this item

  ETIMOLOJIA YA NENO 'BAHARI'
Posted by: MwlMaeda - 07-08-2022, 06:11 AM - Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili - No Replies

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BAHARI'

Neno *bahari* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:

1. Sehemu ya maji chumvi yanayozunguka mabara na visiwa.

2. Kitu, eneo au jambo kubwa na lenye mawanda mapana.

*Msemo:* Elimu ni bahari: Elimu haina mwisho.

3. Mojawapo ya tungo za ushairi.

4. Mshororo wa mwisho wa ubeti usiobadilika katika kila ubeti wa shairi au utenzi.

5. Kitu kikubwa na kipana.
Msemo: Ana bahari ya shamba.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *bahari* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'bahru* *(soma: bahrun/bahran/bahrin  بحر)** yenye maana zifuatazo:

1. Maji mengi yanayochukuliwa na mawimbi hadi nchi kavu, mfano Bahari Hindi.

2. Aina za tungo za mashairi au tenzi zipatazo 16 katika Arudhi ya Kiarabu.

3. Sehemu ya wiki, mwezi au mwaka.

4. Mawingu meupe mepesi ambayo hutanda kabla ya majira ya kiangazi.

5. Ugonjwa wa Kifua Kikuu unaosababisha kiu kikali na kuhitaji sana kunywa maji.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *'bahrun بحر* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *bahari* halikubadili maana yake inayohusu maji na aina ya tungo za ushairi katika lugha  asili ya Kiarabu bali liliongeza maana mpya ya ushairi ya mshororo wa mwisho wa ubeti usiobadilika katika kila ubeti wa shairi au utenzi.

*TANBIHI:*
Katika Arudhi ya Kiarabu neno *bahru (wingi: buhuurun)* lina maana ya aina za tungo za ushairi 16 nazo ni: AT-TWAWILU, AL-MADIIDU,AL-BASIITWU, AL-WAAFIRU, AL-KAAMILU, AL-HAZAJU, AR-RAJAZU, AR-RAMALU, AS-SARII-U, AL-MUNSARIHU, AL-KHAFIIFU, AL-MUDHWAARI-U, AL-MUQTADHWABU, AL-MUJTATHU, AL-MUTAQAARIBU NA ALMUHDATHU.
Mgunduzi wa bahari 15 ni AL-KHALILU BIN AHMAD AL-FARAAHIIDY na bahari ya 16 ambayo imeitwa AL-MUHDATH imeongezwa na mwanafunzi wake AL-AKHFASHU AL-AWSATWU.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*

Print this item

  Kwa nini 7/7 na si tarehe nyingine?
Posted by: MwlMaeda - 07-07-2022, 09:00 PM - Forum: Kiswahili Kimataifa - No Replies

Kwa nini 7/7 na si tarehe nyingine?

Tarehe iliyopendekezwa ya siku ya Kiswahili duniani ni tarehe 7 mwezi Julai kwa kuwa katika tarehe hiyo mwaka 1954 ni siku ambayo chama cha Tanganyika African National Union, TANU chini ya hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kilipitisha Kiswahili kama lugha ya kuunganisha harakati za ukombozi. Bila shaka, Rais wa zamani na pia Baba wa Taifa la Kenya, Hayati Mzee Jomo Kenyatta, pia alitumia lugha ya Kiswahili kupitia kauli yake maarufu, “Harambee” ya kuhamisha watu wakati wa harakati dhidi ya ukoloni. Zaid iya hapo tarehe 7 mwezi Julai mwaka 2000, jumuiya ya Afrika Mashariki, EAC, ilianzishwa tena kurejesha ushirikiano na utangamano baina ya wananchi wa Kenya, Tanzania na Uganda ambako Kiswahili kinazungumzwa zaidi. Rwanda, Burundi na Sudan Kusini zimejiunga baadaye na ni wanachama wa EAC.

Print this item