MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI

Welcome, Guest
You have to register before you can post on our site.

Username
  

Password
  





Search Forums

(Advanced Search)

Forum Statistics
» Members: 5,481
» Latest member: Kundlimatching
» Forum threads: 2,178
» Forum posts: 2,256

Full Statistics

Online Users
There are currently 152 online users.
» 0 Member(s) | 150 Guest(s)
Bing, Facebook

Latest Threads
Buy Vilitra 60 Mg |【Get E...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-24-2023, 11:45 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce50?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-19-2023, 12:59 PM
» Replies: 0
» Views: 0
About the Vidalista 60 Mg...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-04-2023, 04:07 PM
» Replies: 0
» Views: 0
What Is Vidalista 60?
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
04-03-2023, 10:49 AM
» Replies: 0
» Views: 0
How to take Cenforce 100 ...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Kieth_winsett
03-29-2023, 02:37 PM
» Replies: 0
» Views: 66
How is Vidalista 10 Mg us...
Forum: Watunzi wa Kiswahili
Last Post: Kieth_winsett
03-27-2023, 01:26 PM
» Replies: 0
» Views: 117
Obtain Thesis Paper Assis...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Minny02
03-24-2023, 03:01 PM
» Replies: 0
» Views: 200
SEO services for sports f...
Forum: Historia ya makabila ya kibantu
Last Post: Maria Poland
03-17-2023, 01:51 PM
» Replies: 1
» Views: 223
NUKUU ZA KISWAHILI DARASA...
Forum: Nukuu
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:31 PM
» Replies: 0
» Views: 788
NECTA K4 2022
Forum: Mitihani
Last Post: MwlMaeda
01-15-2023, 05:25 PM
» Replies: 0
» Views: 403

 
  MAELEZO YA METHALI ZA KISWAHILI
Posted by: MwlMaeda - 06-15-2021, 08:24 AM - Forum: Semi - No Replies

1. Mwenye pupa hadiriki kula tamu

Mtu mwenye haraka asiye na uvumilivu huwa hafanikiwi
2. Mwenye tumbo ni tumbole, angafunga mkaja
Mkaja ni aina ya mkanda aghalabu hufungwa tumboni na mwanamke hasa baada ya kujifungua. Methali hii inatumiwa kuasa kuwa mwenye kupata tumbo kalipata tu asijisumbue kufunga mkaja atajiumiza bure. Wanawake wengi hupenda kufunga mkaja baada ya kujifungua ili kuzuia tumbo lisiwe kubwa na kuharibu muonekano.
3. Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana
Mwenye kuiba ni mwizi tu japo Mlifi (mlipaji), huuwa ni muungwana. Ukiiba unapoteza sifa ya uaminifu uliyokuwa nayo hata kama utalipa ulichoiba bado utabaki na sifa ya wizi.
4. Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.
Ujanja ukizidi mwisho huondoa maarifa na hatimaye mtu huweza kuangukia asipotegemea kama inavyokuwa kwa ndege mjanja
5. Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana chukua kikapu ukavune
Ndugu huwa hawagombani na hata ikitokea wakagombana ujue ugomvi wao hauvunji undugu wao hivyo usiingilie maana utapoteza muda wako bure ni bora ukalime ili siku wakipatana uwe na ulichovuna.
6. Nifae na mvua nikufae na jua
Methali hii inasisitiza umuhimu wa kusaidiana kwa kujua kuwa kila mmoja ana umuhimu wake kwa wakati fulani, mtu asipokufaa kwa jambo hili ipo siku atakufaa kwa jambo lingine
7. Lila na fila hazitangamani.
Lila ni wema au uzuri na fila ni ubaya/uovu,kutangamana ni kukaa pamoja/kuchangamana. Mambo mema hayakai pamoja na mambo maovu hivyo hata watu wema hawakai pamoja wala kufungamana na watu wabaya/waovu.
8. Kuzima koleo si mwisho wa uhunzi
Koleoni zana ya ufundi na uhunzi ni ufuaji vyuma. Kuvunjika kwa koleo sio sababu ya kuacha kazi ya uhunzi, methali hii inahimiza kutoacha kufanya mambo kwa visingizio
9. Jambo usilolijua, usiku wa giza
Kutolijua jambo humnyima mtu maarifa juu ya jambo hilo sawa na jinsi ambavyo mtu hushindwa kuona iwapo kuna giza. Mtu asiyefahamu jambo kwa kina hawezi kuwa na maarifa ya kutosha kwa jambo hilo
10. Jino la pembe si dawa ya pengo.
Jino la pembe ni jino la bandia ambalo mtu huweka kuziba sehemu iliyotoka jino. Jino hili huwa haliwezi kushika kama ilivyo kwa jino halisi la kuzaliwa nalo. Methali hii huasa kutotegemea vitu vya muda kwani huwa havidumu.
11. Jitihadi haiondoi kuduru
Jitihada ni bidii na kudura ni nguvu au uwezo wa Mungu. Hivyo bidii haiondoi uwezo wa Mungu, methali hii hutumiwa kuwatahadharisha watu wasiopenda mafanikio ya wengine hasa inapotokea aliyefanikiwa ni kwa uwezo wa Mungu tu.
12. Jungu kuu, halikosi ukoko.
Jungu kuu ni chungu kikubwa, chungu kikubwa kikipikiwa hakikosi ukoko hata kama chakula kitakuwa kimekwisha. Methali hii inatujulisha kwamba mtu aliyekuwa tajiri hata akiharibikiwa na kufilisika, hakosi akiba yoyote japo ndogo.
13. Jununu fununu.
Fununu ni habari za mnong’ono; habari zisizo na hakika. Jununu ni sawa na jambo. Mambo mengi huanza kufahamika kwa fununu kabla ya kusikika kwa ukweli wake, methali hii inahusiana kabisa na ile isemayo lisemwalo lipo kama halipo laja.
14. Kafiri akufaaye, si muislamu asiye kufaa
Kafiri huhesabiwa kuwa ni mtu asiye na dini, asiyeamini Mungu. Methali hii inatumika kuonesha umuhimu wa kutenda mema bila kujali unaimani au la kwa sababu matendo mema humpa mtu thawabu, lakini usialmu usioambatana na wema hauna tofauti na ukafiri.
15. Kafiri akufaye si Isilamu asiyekufaa.
Kafiri huhesabiwa kuwa ni mtu asiye na dini, asiyeamini Mungu. Methali hii inatumika kuonesha umuhimu wa kutenda mema bila kujali unaimani au la kwa sababu matendo mema humpa mtu thawabu, lakini usialmu usioambatana na wema hauna tofauti na ukafiri.
16. Kanga hazai ugenini.
Kanga ni ndege jamii ya kuku, kwa desturi kanga huishi porini ingawa hutokea akafugwa majumbani mwa watu. Kanga awapo ugenini nje ya mazingira yake huwa vigumu sana kutaga kwa sababu hukosa mazingira aliyoyazoea huko porini. Methali hii hutumiwa kuonesha ugumu wanaoupata watu wawapo katika mazingira mapya.
17. Kibuzi na kibuzi hununua jahazi.
Methali hii inaonesha umuhimu wa kuweka akiba kidogokidogo, watu hudharau vitu vidogo bila kujali kuwa vinaweza kuwa vingi na kuleta faida kubwa.
18. Kichango kuchangizana.
Methali inahimiza ushirikiano katika masuala mbalimbali hasa yanayohusu kuchangiana, baadhi ya jamii huwa na utaratibu wa kupitisha harambee ili kufanikisha jambo la mtu mmoja na utaratibu huo huendelea kwa kila atakayepatwa na haja kama hiyo.
19. Kikulacho ki nguoni mwako.
Kikulacho ni aina fulani ya mdudu anayeuma na mwenye maumivu makali sana huwa anapenda kujificha kwenye nguo. Aghalabu mtu mbaya kwako huwa hatoki mbali na wewe ni mtu anayekufahamu vizuri.
20. Kikushindacho kukila usikitie ila.
Kutia ila ni kutoa sifa mbaya juu ya kitu, methali hii inaitaka jamii kutosema vibaya kuchafua sifa ya kitu ambacho unahisi hakikufai au kukunufaisha huku ukitambua kuwa huwezi kukitumia.
21. Kila chombo kwa wimblile.
Wimbi ni mvumo mkali wamaji unaosababishwa na upepo hasa baharini, kila chombo cha kwenye maji hudhuriwa na wimbi kutegemea na uwezo wa chombo chenyewe, methali hii inataka watu wasifanye mambo kwa kuiga bali kupima uwezo kwanza juu ya jambo lenyewe ili kujiridhisha kama litawezekana ama la.
22. Kila mwamba ngoma ,ngozi huivuta kwake.
Kuwamba ngoma ni kule kuivuta ngozi ili ienee kwenye kibao cha kutengenezea ngoma na huwezi kuwamba ngoma bila kuivuta ngozi kuja kwako. Methali hii hutumiwa kwa watu ambao huonekana kujipendelea wao zaidi ya wengine na kutaka vitu vizuri viwe kwao tu mf. mafisadi hujilimbikizia mali bila kujali watu wengine huwa sawa na wawamba ngoma.
22. Kila shetani na mbuyu wake.
Shetani ni kiumbe kisichoonekana na huogopwa sana, shetani huaminika kuwa anapenda sana kuishi kwenye mibuyu na huwa akichagua mbuyu mmoja ndiyo huo huo. Methali hii hutumiwa kwa watu wanaoonekana kupenda sana vitu fulani au mtu fulani kiasi cha kuwa tayari kufanya lolote kwa ajili ya mtu huyo, yani huwa kama shetani ashikiliavyo mbuyu na asitake kuuachia kwa namna yoyote.
23. Kilimia kikizama kwa jua, huzuka kwa mvua, na kikizama kwa mvua, huzuka kwa jua
Kilimia ni kikundi cha nyota zinazoambatana na majira ya mvua. Kuibuka na kuzama kwa nyota hizi huendana na majira. Methali hii inatufundisha kuwa kila jambo huwa na wakati wake hivyo tusilazimishe mambo kabla ya wakati wake kwani huweza kutokea yakaharika kabisa.
24. Kipofu hasahau mkongojo wake.
Kipofu ni mtu asiyeona ambaye hutegemea mkongojo (aina fulani ya fimbo inayomuongoza) kutambua njia. Methali hii hutumiwa kuonesha jinsi watu wanavyokuwa makini na kukumbuka vitu wanavyovithamini kutokana na umuhimu wa vitu hivyo kwao sawa kabisa na mkongojo kwa kipofu.
25. Kipya kinyemi ingawa kidonda.
Kinyemi ni kitu cha kupendeza, chenye kufurahisha. Methali hii hutumiwa kwa mtu aliyepata kitu kipya ambacho si kizuri hivyo, lakini akakienzi zaidi kuliko kizuri alichokuwa nacho tangu zamani. Pia, watu hutumia methali hii wanapomwona mtu anapenda kuvaa nguo hiyo hiyo mara nyingi kwa sababu ni mpya.
26. Kisebusebu na kiroho papo.
Kisebusebu ni mtu mwenye tabia ya kuonyesha watu kwamba jambo fulani hana haja nalo na kumbe analitaka. Methali hii hutumiwa kuwasema watu wenye tabia ya kujifanya hawataki vitu fulani na kumbe wanavitamani.
27. Kisokula mlimwengu,sera nale.
Kisichofaa kwa mwanadamu hufaa kwa shetani na hicho hakifai kutumiwa. Methali hii huasa watu kutofanya mambo ambayo hayana utu kwa walimwengu kwani hayo huwa ni ya kishetani.
28. Kitumbua kimeingia mchanga.
Kitumbua ni aina ya kitafunwa kiachotokana na unga wa mchele, kitumbua kikiingia mchanga huwa hakiliki. Methali hii hutumiwa kuashiria jambo kuharibika mathalan mtu anapofukuzwa au kuachishwa kazi, husemwa kitumbua chake kimeingia mchanga.
29. Kiwi cha yule ni chema cha; hata ulimwengu uwishe.
Kiwi hapa inamaanisha giza la machoni linalofanywa na kitu kinachong’aa sana. Methali hii hutumiwa kuwatambulisha watu ambao hawazingatii sana mvuto wa vitu kwa nje bali thamani ya kitu husika, huwa ni kama hawaoni vyenye mvuto wa nje wanapopata chenye thamani
30. Konzi ya maji, haifumbatiki.
Konzi ni kiasi au kadiri inayoweza kushikwa kwa kufumbata vidole. Methali hii inaasa kuwa sio kila kitu kinafaa kushikiliwa katika maisha kwani vingine havishikiki.
31. Kozi mwandada, kulala na njaa kupenda
Kozi ni ndege mkubwa kama mwewe anayekamata wanyama wadogowadogo. Ulaji wa ndege huyu hutegemea juhudi zake, akilala tu kwa uvivu wake atalala njaa. Methali hii huhimiza watu waache uvivu wajishughulishe na kuacha kukaa tu.
32. Bwawa limeingia ruba.
Ruba ni mdudu anayefanana na nyungunyungu afyonzaye damu na huishi kwenye sehemu za majimaji na bwawa ni mkusanyiko mkubwa wa maji mengi ambao ni mdogo kuliko ziwa. Methali hii hutumiwa kuashiria kuwa uhuru uliozoeleka mahali sasa haupo tena kutokana na kuingia kwa mtu/kiongozi mwenye msimamo na kufuata taratibu na sheria.
33. Chaka la samba, halilali nguruwe.
Chaka ni mwitu mkubwa. Sehemu ya mwitu anamokaa samba, nguruwe halali, au hakai kwa kituo, mahali hapo. Methali hii inatumiwa na mtu kwa maana ya kuwa hawezi kukaa mahali fulani kwa sababu ya maonevu ya aliyemzidi nguvu.
34. Choko mchokoe pweza, binaadamu hutomuweza.
Pweza ni jamii ya samaki anayejificha mwambani ili kumpata lazima kumchokoa (kumchokoza) ilia toke alikojificha. Methali hii hutambiwa watu wanaopenda ugomvi ambao huchokoza wengine ili sababu ya kugombana ipatikane.
35. Chombo cha kuzama hakina usukani.
Chombo kama jahazi au meli kikishajaaliwa kuzama kitazama tu, hakina nahodha wala baharia. Methali hii hutumiwa kuonesha kwamba jambo likipangwa kuharibika basi hakuna cha kuzuia
36. Chovya – chovya yamaliza buyu la asali
Buyu la asali ni chombo cha asili kinachohifadhia asali, chovyachovya ni kule kulamba asali kwa kutumia kidole, kwa kufanya hivyo mtu hujikuta amemaliza buyu zima la asali bila kutarajia. Methali hii hutumika kuasa watu wasio na utaratibu mzuri katika matumizi hujikuta mtu amechukua pesa kidogo kidogo hata mwisho imekwisha na alichokifanya hakionekani.
37. Chururu si ndo ndo ndo.
Chururu ni mlio wamaji yanapomiminika kwa wingi na ndo ndo ndo ni mlio wa matone ya maji yanapodondoka, hasa kwenye ndoo au debe, tone baada ya tone. Methali hii hutumika kwa maana ya kuwa bora mtu kupata kidogo kidogo kila siku kuliko wingi wa mara moja na kukosa. Kwa mfano afadhali mtu apate kitu cha matumizi japo ni kidogo cha kila siku kuliko kupata kingi cha mara moja kikiisha iwe basi
38. Dalili ya mvua mawingu.
Dalili, yaani alama ya kuonesha kuwa itanyesha mvua ni kuyaona mawingu ya mvua angani. Dalili ya kupata ulilokusudia, kwanza ni kuiona ishara ya kukuonesha kuwa hicho kitu kipo tayari kukufika. Methali hii hutumiwa kwa maana ya kuwa jambo likitaka kuwa, huwepo ishara (dalili) kwanza inayoonesha kuwa jambo hilo litatokea. Watu husema methali hii wanapoiona dalili kama hiyo.
39. Dau la mnyonge haliendi joshi, likienda joshi ni matakwa ya Mungu.
Dau ni Aina ya chombo cha majini. Joshi ni Chombo cha baharini kwenda kwa kasi/kina kirefu. Methali hii hutumika mtu anapoona jambo lake halinyooki au haliendi ipasavyo kwa sababu ya kukosa pesa au kwa kuwa hali yake ni duni.
40. Donda ndugu halina dawa.
Donda ndugu ni donda la siku nyingi, lisilopona. Donda la siku nyingi hata ukilifanyia dawa namna gani huwa halisikii dawa, na kupoa huwa ni kwa bahati sana. Methali hii hutumiwa kwa mtu aliye na tabia mbaya na amezama kabisa katika tabia yake hiyo. Mtu huyo huwa ametolewa tamaa tena kuwa kuna dawa ya kumwachisha tabia yake mbovu.
41. Fahari ya macho haifilisi duka.
Katika biashara wateja hurusiwa kutazama bidhaa ili kuona kama watavutiwa. Ili kuwahamasisha hasa iwapo wanaonekana kuogopa bei kutokana na uzuri wa bidhaa husika basi muuzaji huwatoa woga kwa kuwaambia fahari ya macho haifilisi duka. Yani hata kama hawakununua kutazama tu hakuwezi kumfilisi muuzaji.
42. Farasi hamuwawezi, tembo mtawalishani?
Farasi ni mnyama anayekula kidogo kuliko tembo, methali hii huambiwa watu wanaotaka mambo makubwa hali madogo yenyewe hawayamudu.
43. Funika kombe mwanakharamu apite.
Kufunika kombe ni kauli inayotumiwa kumwashiria mtu akubaliane tu ili yaishe yasifike kwa wakubwa na kuleta balaa zaidi, mwanaharamu ni mtu asistahili katikajambo au mazingira fulani. Iwapo tunakuwa na mambo yetu ya kuzungumza na ikatokea kubishana hata kutaka kuwanufaisha wasiohusika, methali hii ndipo hutumika kama namna ya kuwaasa wahusika kumaliza tofauti zao hata kama hawakuridhika.
44. Ganda la mua la jana, chungu kaona kivuno.
Chungu ni aina ya wadudu wadogo wanaopenda sukari na aghalabu huwakuta wamejazana kwenye maganda ya muwa. Mtu anapofikia kutema ganda la muwa ni ishara kwamba hakuna kitu cha thamani amemaliza sukari yote hivyo halimfai, lakini pindi anapolitema tu hukuta chungu (wadudu) wamejaa tele wanafanya karamu. Hii ni kusema tusidharau visivyotufaa na kuvitupa kuna wanaovihitaji na kuvithamini. Mathalan mavazi yaliyochujuka kwako au kuwa madogo kuna watu wakiyapata hayo huwa ya kuzaa siku ya sikukuu.
45. Gome la udi, si la mnuka uvundo.
Udi ni magome ya mti fulani yanayotoa harufu nzuri yanapoungua, agh. hutumika kufukizia. Uvundo ni harufu mbaya. Methali hii hutumiwa kuonesha kuwa kisicho chako hakiwezi kukusiri hivyo ni bora kukubaliana na hali yako kama ilivyo. Iwapo unanuka uvundo hata ukitumia udi kufukiza harufu ya uvundo itapotea tu kwa muda na harufu ya udi ukiisha unabaki na harufu yako ya asili, vivyo hivyo katika hali zetu tusiwe watu wa kuishi maisha ya kuigiza kwa vitu vya kuazima.
46. Haba na haba, hujaza kibaba.
Haba katika methali hii inaukilia punje ya nafaka, kidogo na kibaba ni kipimo cha ujazo wa takriban gramu 700. Punje moja moja ukizikusanya mwishowe huwa nyingi za kuweza kujaza kibaba kizima. Methali hii inatufunza tusidharau kitu kidogo. Kwa mfano, pesa kidogo kidogo tukizikusanya mwishowe pesa hizo huwa nyingi.
47. Hakuna masika yaso mbu
Masika ni Majira ya mvua nyingi. Masika kabisa hayakosi mbu (kwa sababu ya mvua na tope nyingi zinazokuwepo). Methali hii inatufahamisha kuwa kila wakati huja na taabu na shida zake, kama vile wakati wa masika unavyokuja na mbu.
48. Hala hala mti na macho.
Methali hii hutahadharisha watu juu ya matendo yao kuwa huweza kuumiza wengine pasipo wao kujua au kukusudia. Ni sawa na mtu awapo na mti mkononi na akawa anaugeuzageuza bila kujali waliko pembeni mwake huweza kuwachoma machoni na ikaishia pole tu.
49. Hamadi ni ilio kibindoni, na silaha ni iliyo mkononi. na mwisho.
Hamadi ni tamko la mtu anaposhtuka na kibindo ni mkunjo wa nguo unaofungwa kiunoni k.v. kwenye shuka au kikoi, unaotumiwa kama mfuko kuhifadhia pesa za mtu. Ukishtuliwa (na adui au mnyama mbaya) na kushituka, yataka silaha iweko kibindoni, haiko mbali. Methali nii inamfahamisha mtu kuwa wakati wa haja au dhiki kinachomfaa ni kile alichonacho mkononi, yaani karibu naye. Pia methali hii inamhimiza mtu aweke akiba, kwani ndiyo itakayomfaa akitokewa na haja ya ghafla.
50. Akili ni nywele kila mtu ana zake.
Akili huchukuliwa sawa na nywele ambazo huwa kila mtu anazo na aghalabu hazifanani. Methali hii hutumiwa kuonesha tofauti baina ya watu katika kufanya maamuzi, jambo moja lile lile mmoja anaweza kuliamulia hivi na mwingine tofauti.
51. Akili nyingi huondowa maarifa.
Kujitia akili nyingi au uwerevu mwingi wakati mwingine huondoa busara na hekima ya mtu, na baada ya mtu kufanya jambo likatengenea, huliharibu. Hutumiwa methali hii kwa mtu asiyesikia nasaha na mashauri ya wenziwe katika kufanya jambo; anahisi fikra zake tu ndizo sawa. Mwishowe mtu huyo anashtukia jambo lake limemharibikia.
52. Moyo ukipenda chongo huita kengeza
Methali hii hutumiwa kuonesha nguvu ya mapenzi miongoni mwa wanadamu, kwamba mtu akipenda haoni dosari zilizopo na hata akiziona basi hutafuta namna ya kuzifanya zisionekane kubwa sana.
53. Akupaye kisogo si mwenzio.
Kisogo ni sehemu ya nyuma ya kichwa. Anayekupa kisogo maana yake hataki mtazamane wala mfahamiane na hivyo hataki ukaribu na wewe. Methali hii huambiwa watu wasiopenda ushirikiano na wenzao.
54. Aliye kupa wewe kiti (kibao) ndiye aliyenipa mimi kumbi.
Kumbi ni gamba la nje la nazi. Hutumiwa methali hii kumwambia mtu mwenye kujivuna na kumkandamiza mwenziwe aliyekuwa chini ambaye hana uwezo au madaraka kama yeye.
55. Aliye kutwika, ndiye atakaye kutua.
Kutwika ni kubebesha hasa mzigo kichwani. Aliyekutweka mzigo huyo huyo ndiye atakayekutua mzigo wako. Methali hii hutumika kuambiwa mtu aliyejitakia taabu mfano binti kupata ujauzito.
56. Aliyekupa mkeka ndiye aliyenipa kumbesa.
Mkeka ni zulia la ukili hutumiwa kukalia na kumbesa ni kumbi la nazi aghalabu mnapofika mahali ugenini mwenyeji wenu ndiye huwapa vya kukalia na hapana anayeamua akae wapi kati yenu zaidi ya mwenye wenu. Katika maisha inaaminika kila mmoja anapewa fungu lake na mtoaji ni mmoja tu Mungu. Hivyo hutumiwa methali hii kuwatia watu moyo wasijiumize kwa mafanikio ya wengine kwani kila mtu hupewa alichobarikiwa nacho.
57. Amani haipatikani mpaka kwa ncha ya upanga.
Amani wakati mwingine haiji ila kwa kutumia nguvu. Methali hii inamnasihi mtu ambaye anaonewa na mwenziwe au wenziwe, kuwa apinge maonevu hayo – hapo ndio atapata suluhu na salama.
58. Ana hasira za mkizi.
Mkizi ni samaki ambaye aghalabu huwa na tabia ya kujirusha juu na wakati mwingine huweza kujirusha na kuingia mwenyewe katika mtumbwi wa mvuvi akafurahia. Methali hii hutumiwa kwa watu ambao wakikasirika hufanya mambo yenye kuwanufaisha wengine.
59. Anayekuja pasi na hodi, huondoka bila ya kuaga.
Kuja pasi na hodi ni kutokea bila taarifa na kuondoka bila ya kuaga ni kutoweka kimyakimya. Methali hii hutumiwa kuonesha hali ya kutokea kwa jambo lisilotarajiwa na kutoweka kwake, mathalan huweza kuzuka ugonjwa ukasumbua sana na kisha kutoweka bila ya watu kutegemea.
60. Angurumapo simba, mcheza ni nani?
Simba ni mnyama mbabe na mkali ambaye akiunguruma sauti yake hutisha sana wanyama wengine. Methali hii hutumika kuonesha jinsi mtu fulani alivyombabe hasa katika mazingira ya ushindani kama mpira wa miguu timu moja inaposhinda huweza kuitambia timu pinzani kwa methali hiyo.
61. Aninyimaye mbaazi kanipunguzia mashuzi
Mbaazi/kunde ni mazao jamii ya kunde yenye kusababisha matumbo kujaa gesi na kutoa harufu mbaya.Katika maisha hutokea mtu akakunyima baadhi ya vitu akidhani anakukomoa lakini kumbe amekuepusha na madhara mengine. Hutumiwa methali hii kwa watu wanaowanyima wengine mambo ambayo kimsingi hata wakiyakosa hawapati hasara.
62. Atangaye na jua hujuwa.
Kutanga na jua ni kuhangaika katika kutafuta na kila anayejishughulisha huwa hakosi kupata japo taarifa itakayomwezesha kufahamu mafanikio yalipo. Kwa ujumla methali hii inahimiza watu kujituma na kujishughulisha.
63. Atangazaye mirimo, si mwana wa ruwari (Liwali)
Mirimo ni siri, atoae habari za siri huwa si mhusika wa jambo lenyewe. Mara nyingi watu wasiohusika na jambo ndio hupenda kusema mambo yasiyowahusu.
64. Avumaye baharini papa kumbe wengi wapo.
Katika mazingira ya bahari mnyama anayesifika sana ni papa licha ya kuwa hafui dafu kwa baadhi ya wanyama wakubwa kumzidi kama nyangumi. Methali hii inatoa hadhari juu ya kutolewa sifa na kujisahau hata ukajikuta unapata upinzani mkali kwa kutotambua kwamba kuna wenye uwezo kukuzidi.
65. Bamba na waume ni bamba, hakuna bamba la mume.
Mume hakamiliki bila mke wala mke hakamiliki bila mume. Methali hii hutumika kuonesha hali ya kuhitajiana baina ya wake na waume.
66. Bandu bandu huisha gogo.
Bandu bandu ni ile hali ya kuchonga sehemu ya gogo ili kupata vipande vya kuwashia moto, halii hii hufanywa taratibu na kwa muda mrefu na hatimaye hujikuta gogo limekwisha hata kama lilikuwa kubwa sana. Methali hii inataka watu kutoogopa mambo kwa kuyaona mazito bali kuyaingilia kidogokidogo na mwisho yatakamilika.

Print this item

  Aina za Vitendawili
Posted by: MwlMaeda - 06-15-2021, 08:10 AM - Forum: Semi - No Replies

a) Vitendawili sahili ni vifupi na huwa na na muundo mwepesi kueleweka. K.v.
b) Vitendawili mkufu huwa na vipande vinavyofuatana na kila kipande huwa na uhusiano na kipande kilichotangulia. Mfano “ nikisimama anasimama, nikiketi anaketi, nikiondoka huondoka pia”
c) Vitendawili vya tanakali hutumia tanakali za sauti Mfano: Drrrrrrh mpaka ng’ambo “buibui”; huku ng’o na kule ng’o.
d) Vitendawili sambamba huwa na maelezo marefu (kama hadithi fupi) halafu jibu lake huwa ni refu pia (kama mafumbo)

Print this item

  Sifa za Vitendawili
Posted by: MwlMaeda - 06-15-2021, 07:59 AM - Forum: Semi - No Replies


  1. Vitendawili huwa na mwanzo maalum : Kitendawili  tega

  2. Hupitishwa baina ya watu wawili anayetega na anayetegua

  3. Vitendawili huwa na muundo maalum wa kuendelezwa (utangulizi, swali, (majaribio ya) jibu; wanaotegua wakishindwa anayetega huwa ameshinda, huitisha apewe mji/zawadi na kisha kutoa jibu)

  4. Huwa na vipande viwili swali na jibu. Mfano: Kila niendapo ananifuata  kivuli.

  5. Hutumia mbinu ya jazanda, kufananisha vitu viwili moja kwa moja. K.v. Nyumba yangu haina mlango  yai (yai limelinganishwa moja kwa moja na nyumba isiyo mlango)

  6. Hurejelea vitu vinavyopatikana katika mazingira na vinavyojulikana sana

  7. Vitendawili vilitegwa wakati maalum, hasa wa jioni

  8. Vitendawili hutumia tamathali za usemi (mbinu za lugha) kama istiara, tashihisi, tashbihi, jazanda, chuku, tanakali za sauti, n.k

  9. Vitendawili huwa na jibu maalum.

Print this item

  HISTORIA YA WACHAGA
Posted by: MwlMaeda - 06-15-2021, 07:45 AM - Forum: Historia ya makabila ya kibantu - No Replies

WACHAGA
Usuli
Wachaga ni kabila la watu wenye asili ya Kibantu lakini pia mchanganyiko wa damu, hasa ya Kikushi wanaoishi kaskazini mwa Tanzania chini ya mlima Kilimanjaro, mkoani Kilimanjaro.Shughuli kubwa ya Wachaga ni biashara, kilimo na kazi za ofisini.Wachaga ni kabila la tatu kwa ukubwa nchini Tanzania. Takwimu za mwaka 2003 zinaonyesha kuwa idadi ya Wachaga ni watu 2,000,000.
Vikundi vya Wachaga
Wachaga wana historia ndefu ya asili yao na ya maingiliano yao na makabila mengine. Kabila la Kichaga ni mkusanyiko wa makabila madogomadogo (ya Kichaga) yaliyosambaa kijiografia kuzunguka mlima Kilimanjaro kuanzia mashariki (Tarakea, Rombo) hadi magharibi kwa Kilimanjaro (Siha, Machame).
Makabila ya Kichaga ni Wa-Rombo, Wa-Vunjo ambao wanajumuisha watu wa Mwika, Mamba, Marangu, Kilema na Kirua ambayo ndio inajulikana na wengi kama Kirua Vunjo. Ukipenda unaweza kuwagawa watu hawa wa Vunjo kama Wa-Mwika, Wa-Mamba ,Wa-Marangu,Wa-Kilema,na Wakirua.Makabila mengine ni Wa-Old Moshi, Wa-Kibosho, na Wa-Machame, Wa-Uru, na Wa-Siha.
Lugha ya Kichaga
Lugha ya Kichaga inabadilika kuanzia unapotoka Tarakea mpaka unapofika Siha magharibi mlima Kilimanjaro.
Kutokana na tofauti hizo Kichaga kimegawanyika katika Kirombo (ambacho nacho kinatofautiana kadiri unavyotoka eneo moja hadi jingine; mfano Kisseri, Kimashati, Kimkuu, Kimengwe, Kimahida), Kivunjo, Kimarangu, Kirombo, Kioldimoshi, Kingassa, Kiuru, Kikibosho, Kimachame na Kisiha.
Lugha hizo zinakaribia kufanana kadiri makabila hayo yalivyopakana. Kwa mfano, Kivunjo kinafanana na Kioldimoshi. Vile vile Kisiha kinafanana sana na Kimachame ambacho pia kinafanana kidogo na Kikibosho.
Baadhi ya Wamachame walihamia sehemu za Meru, Arusha, na kuchanganyikana na Waarusha, hivyo lugha yao ikabadilika kidogo na kuwa Kimeru. Kwa sababu hiyo Wameru wanasikilizana sana na Wamachame ingawa lafudhi zao zinatofautiana kidogo.
Koo za Kichaga
Majina ya kiukoo ya Kichaga pia huashiria wanatoka sehemu gani ya Uchaga, japo si lazima kuwa hivyo: kwa mfano, familia maarufu za Kichaga nchini Tanzania ni kama ukoo wa akina Mushi, Mmasy Kimaro, Swai, Massawe, Lema, Urassa, Nkya, Ndosi, Meena hutoka Machame.
Akina Temu, Mlaki, Mlay, Lyimo, Moshiro, Mselle, Kamnde, Kileo, Kimambo, Tesha, Msaki, Assey, Kyara, Kessy, Ndanu, Macha, Mbishi, Kombe, Njau wanatoka Old Moshi na Vunjo.
Majina mengine ya Old Moshi ni kama yafuatayo: Mmari, Macha, Mshiu, Kyara, Moshi, Massamu, Kimambo, Mboro, Mlngu, Saule,Tenga, Njau, Malisa, Maro, Maeda, Ringo,Olomi, Ngowi, Lyatuu na mengine mengi.
Kavishe, Mariki, Tarimo, Laswai, Mallya, Mrema, Mkenda, Massawe, Silayo, Lyaruu, Makyao, Mowo, Lamtey, Tairo, Masue, Maleto, Mramba, Kauki wanatoka Rombo.
Sawe, Usiri, Shayo, Kiwelu, Makundi, Urasa, Mtui, Moshi, Meela, Minja, Njau,Mtei wanatoka Marangu na Kilema.
Rite, Makule, Minja, Mashayo, Chao, Shao, Makawia, Ndesano, Kimario, Tilla, Mariale, Tarimo, Mafole, Kituo, Mrosso, Lyakundia, Kessy, Mmbando, Matemba, Ndenshau, Morio, Akaro, Matowo, Towo, Mkony, Temba, Foya, Munishi, Kilawe, na kadhalika hutoka Kibosho.
Ukoo wa akina Teri wako Mamba, Chami, Chuwa, Kiria Owoya na wachache Sango, Old Moshi na wengine walihamia Maji ya Chai, Mkoa wa Arusha.
Utawala wa jadi wa Wachaga
Watawala wa Kichaga waliitwa “Mangi”. Hawa walihodhi mashamba, ng’ombe na waliheshimiwa kama viongozi wa kikabila. Walikuwa na nguvu za kisiasa na utajiri. Baadhi ya Ma-mangi mashuhuri katika historia ni kama Mangi Rindi aliyeingia mikataba na wakoloni (Wajerumani), Mangi Sina wa Kibosho na Mangi Horombo wa Keni – waliojulikana kwa uhodari wao wa vita katika kupigana na Wamachame na kupora ng’ombe na mazao yao, hata mpaka leo makabila ya Kimachame na Kikibosho hayaoani kwa urahisi, na Mangi Marealle wa Marangu na Vunjo. Mangi Meli huyu alikuwa mangi wa waoldmoshi ambaye alipigana na wajerumani na aliishia kukatwa kichwa na mpaka sasa kichwa chake kipo ujerumani alizikwa kiwiliwili tuu baada ya kumnyoga na mti aliyonyongewa upo mpaka sasa sehemu ya oldmoshi bomani karibu na kolila sekondari .
Wakoloni walipokuja Kilimanjaro waliingia mikataba na viongozi hawa wa kikabila ili kuweza kuweka misingi yao ya kikoloni. Pia ndugu na watoto wa Ma-mangi walikuwa wa kwanza kupata elimu ya kikoloni, kwa hiyo waliweza kushirikishwa katika serikali za kwanza. Hawa pia wanaaminika walikuwa kama mabepari wa kwanza wa kijadi, maana walifanyiwa kazi na watu wengine wakati wao Ma-mangi wamekaa kuhesabu mali zao.
Usemi maarufu wa “u-Mangi-meza” nadharia inawezekana kuwa umetokana na watawala hawa wa Kichaga.
Elimu kati ya Wachaga
Wachaga wanajulikana kwa uwezo wao mkubwa katika uwanja wa elimu, hususani katika masomo ya sayansi na hisabati. Moshi ni maeneo ya mwanzo ambayo wamisionari wa Ukristo walijenga makanisa na shule.
Sababu hii imefanya Wachaga kuwa kabila namba moja lenye watu wengi zaidi walio na elimu ya kisasa (elimu ya juu) na mkoa wa Kilimanjaro unaongoza kwa idadi ya shule za sekondari nchini Tanzania. Kulingana na takwimu za elimu mkoa huo una shule za sekondari zaidi ya 320. Pia mkoa una shule za msingi zipatazo 950. Idadi hii ya shule ni kubwa zaidi ya idadi ya shule katika mikoa mingine Tanzania.
Shule nyingi za sekondari ziko katika mkoa huu kwa sababu zifuatazo: 1) Hali ya hewa na vivutio vya kitalii katika mkoa huu viliwavutia zaidi walowezi na wakoloni na kuweka makazi yao hapo. Hivyo wamisionari walijenga shule za kwanza wakifuatiliwa na serikali za wakoloni 2) Serikali ya Tanzania ilirithi shule zilizojengwa na wakoloni 3) Wachaga waliobahatika kupata fedha binafsi baadaye waliwekeza kwenye ujenzi wa shule binafsi kama kitega-uchumi, wakati wakazi wa mikoa mingine kadhaa walisubiri serikali iwajengee shule. 4) Ukichanganya sababu 1, 2 & 3 utagundua shule katika mkoa wa Kilimanjaro zimezidi sana idadi ya shule katika mikoa mingine yote.
Ni vema pia kusema kuwa shule hizo huvutia wanafunzi kutoka Tanzania nzima, haziwasomeshi Wachaga tu.
Ardhi
Ingawa ardhi ni msingi wa maendeleo kwa watu wote, kwa Wachaga, ardhi ni mali sana kwa sababu kilimo chao ni cha mazao ya kudumu kama kahawa na ndizi hukaa shambani kwa muda wa miaka mingi.
Mojawapo ya urithi wapewayo watoto ni “kihamba”. Hii ni sehemu ya ardhi ambayo mtoto anategemewa atajenga na kuanzisha familia yake. Bahati mbaya watoto wa kike walikuwa hawapewi kipaumbele katika ugawanaji wa vihamba. Uhabawa ardhi huko Uchaga ulipelekea Wachaga wengi kuhamia mikoa mingine. Hivi leo utakuta Wachaga wakiishi Dodoma, Morogoro, Iringa, Mbeya n.k. wakiwa wamepanda migomba yao na kuendesha biashara za maduka ya vyakula.
Ukienda kwenye mikoa hiyo utakuta wamejenga jamii zao na vyama vyao vya kusaidiana wakati wa sherehe au matatizo. Aidha hata pombe ya mbege utaweza kuikuta kwenye makusanyiko ya Wachaga katika mikoa mbalimbali.
Kilimo na chakula
Wachaga hulima mazao ya chakula kama vile mahindi, maharagwe, viazi, ndizi, ulezi na mboga mbalimbali. Pia mazao ya biashara kama vile kahawa, nyanya na vitunguu.
Ndizi za Wachaga
Ingawa Wachaga wa leo wanakula vyakula mbalimbali kama vile ugali, wali na viazi, chakula kikuu cha Wachaga ni ndizi.
Kuna ndizi za aina mbalimbali na kwa matumizi tofauti. Mfano ndizi sukari ni fupi na huachwa hadi ziive na huliwa mbivu kama tunda.
Ndizi mshale hukatwa zikiwa mbichi na kupikiwa vyakula mbalimbali pamoja na nyama ya ng’ombe, kondoo au mbuzi. Mara nyingine hupikwa na maharage, choroko, kunde au hata maziwa ya mtindi. Vyakula vya ndizi huja kwa ladha tofauti kama vile ndizi nyama, mtori, machalari, kiburu na kadhalika.
Aina nyingine ni ndizi ng’ombe ambazo huachwa ziive halafu humenywa na kutumiwa kutengenezea pombe maarufu iitwayo mbege. Mbege hutengenezwa kwa kutumia ndizi mbivu, maji, na ulezi.
Aina nyingine ni ndizi mzuzu. Hizi zikikomaa huachwa zianze kuiva kidogo halafu huchomwa na kuliwa kama kitafunwapamoja na chai au pombe. Ukipita mitaa ya Dar es Salaam utaona ndizi mzuzu zikichomwa sambamba na muhogo au kuku vumbi au kiti moto.
Wachaga na muhogo
Inasemekana kuwa “Mchagga halisi hali muhogo – akila muhogo atakufa”. Usemi huu umetokana na historia ya mababu kuwa Wachaga waliopanda mihogo Kilimanjaro enzi za kale walikufa baada ya kuila. Historia hiyo yaweza kuwa ya ukweli kwa sababu aina nyingi za mihogo zinajenga sumu ya sianidi ndani yake; watu waliozoea kutumia mihogo huwa na njia za kuondoa sumu kwa kuiloweka mihogo katika maji kwa muda. Lakini kama Wachaga wale wa zamani, hasa wa Machame, walifanya jaribio bila kujua mbinu ya kuondoa sumu, ajali iliweza kutokea. Cha kushangaza ni kwamba hukohuko Kilimanjaro, majirani na watani wa Wachaga, yaani Wapare, walikuwa wameshazoea mihogo na ilikuja kuwa moja ya chakula chao kikuu.
Ulaji kiti-moto
Pamoja na kilimo cha mazao, Wachaga hupendelea sana kufuga nguruwe. Tabia ya kula nyama ya nguruwe ijulikanayo leo kwa jina la “kiti moto” ni moja ya mambo yaliyoenezwa na Wachaga. Ulaji wa “kiti moto” haukuwa pendeza baadhi ya wenyeji wa Pwani kama Dar es Salaam ambapo Wachaga walihamia, kwani wakaaji wengi wa Pwani ni Waislamu kwa hiyo nguruwe kwao ni haramu. Wakazi wa Dar es Salaam watokao makabila mengine na wasiyo Waislamu kwao kula nguruwe ilikuwa “ruksa”.
Maoni juu ya Wachaga
Ingawa wanaume wa Kichaga hupendelea kufanya kazi mbali na kwao, wake zao hukaa nyumbani (Moshi) na hufuga ng’ombe na kazi za shambani. ila kwa sasa kutokana na ugonjwa wa ukimwi tabia hii imepungua miongoni mwao.
Wanawake wa Kichaga (hasa kutoka Machame) hujulikana kama wafanyakazi hodari. Huchangia sana katika mapato ya nyumbani na chakula.
Ingawa kipato cha Wachaga ni kikubwa kulingana na cha makabila mengine, takwimu zinaonyesha watoto wa mkoa wa Kilimanjaro kuongoza kwa utapiamlo. Sababu kubwa ya watoto kuwa na utapiamlo ni wazazi kujali zaidi kazi kuliko muda wa kuwahudumia watoto.
Wengi wa watoto hao ni wale ambao wazazi wao ni watu wa pombe na kipato chao kinaishia kilabuni. Utaona kwamba Uchagga una vilabu vingi vya pombe na vinaongezeka kwa sababu imekuwa biashara kubwa. Karibu kila kaya kumi na tano kuna kilabu cha pombe na kiwango cha chini kabisa cha pombe inayouzwa kwa siku katika vilabu hivyo si chini ya madebesita au lita mia moja. Pombe ni sababu moja ya watoto kuwa na utapiamlo.
Hii inawezekana kuwa matunda ya wazazi kutowalisha watoto wao chakula cha kutosha au chakula bora. Kuna sehemu nyingine za Uchagga kama Old Moshi na Kibosho ambapo watoto wadogo hupewa pombe ya mbege asubuhi, mchana na jioni.
Sababu nyingine ni kazi; mama wa Kichaga anaweza kushinda shambani kutwa na hana desturi ya kubeba watoto mgongoni kwenda nao shambani, hivyo wanakuwa nyumbani ama wenyewe au na mayaya. Mfano ulio dhahiri ni nyakati za asubuhi na mapema kwenye vyombo vya usafiri karibu robo tatu ya abiria ni wanawake wakienda katika shuguli za biashara na kilimo na vivyo hivyo nyakati za jioni wakirudi majumbani. Hao ni nje ya wale wanaotumia usafiri wa miguu ambao ni wengi zaidi.
Pia baadhi ya kina mama wa Kichaga wanawajali waume zao zaidi kwani nyama nzuri ni ya baba. Kuepuka gharama baba ataandaliwa chakula kizuri, tofauti na chakula walichoandaliwa watoto, japo ni chakula kilekile.
Pia Wachaga wamekuwa na desturi ya kuwaenzi wazee wao waliotangulia mbele za haki kwa kuwatambikia kwa pombe na nyama za mbuzi pale tu wanaporudi nyumbani ifikapo mwezi Desemba. Hili limekuwa suala la kawaida sana na halipingiki. Wengi wao huwa wanarudi na magari, ndiyo sababu utaona ya kwambwa kila ifikapo mwezi Desemba kila mwaka foleni za magari zimekuwa zikiongezeka kutokana na Wachaga kurudi nyumbani msimu wa sikukuu. Wengi wao wamekuwa wakitoka sehemu mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi.
Wachaga wengi hupenda kurudi nyumbani kipindi cha Krismasi, ikiwa ni kuwatembelea wazazi wao, rafiki, au ndugu.
Ingawa wengi hudhani kwamba Wachaga wamepokea sana dini [imani] ya Ukristo kwa kuwa wengi wao ni Wakristo na hiki huwa ni kipindi cha likizo kwao, inaaminika pia kuwa kurudi kwao Uchagani wakati wa Krismasi ni pamoja na kutembelea ndugu zao na kujumuika pamoja katika kuumaliza mwaka baada ya kazi nyingi za kutafuta pesa mwaka mzima.
Pia imekuwa kama desturi wanaukoo kukaa pamoja na kujadiliana mambo jinsi yalivyokwenda katika kipindi kizima cha mwaka na wakati mwingine inakuwa sehemu ya kwenda kuwatambulisha watoto kwa bibi na babu zao, hasa wale waliozaliwa mijini.
Dola Ya Wachaga
Wakati wazungu wanagawana bara la Afrika, walipokuja walikuta baadhi ya maeneo kuna tawala zenye nguvu, zilizokua na mfumo rasmi wa uongozi. Wao waliziita tawala za jadi (Chiefdoms).
Moja ya tawala iliyokua na nguvu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki ni dola ya Wachaga (Chagga state). Zilikuwepo nyingine zenye nguvu kama Himaya ya Sultani wa Zanzibar, Dola ya Buganda, Nyamwezi, Ngoni, Haya, Hutu, Tutsi na Hehe,
Dola ya Wachaga imetamalaki eneo la pembezoni mwa mlima Kilimanjaro kuanzia maeneo ya Rongai hadi Siha.
Eneo hili lilikua na mtawala mkuu mmoja (aliyeitwa Mangi Mkuu). Huyu alikua kama Rais ama Mfalme wa jamii hiyo. Chini yake walikuwepo watawala wakuu wawakilishi wa majimbo. Hawa waliitwa ‘Mangi Waitori’. Chini yao walikuwepo watawala wa wa maeneo madogo, hawa waliitwa Mangi kama vile Mangi Meli wa Old Moshi, Mangi Sina wa Kibosho, Mangi Salakana wa Useri.
Kwa mfano eneo kama Rombo lilikuwa na Mangi wengi. Alikuwepo Mangi wa Keni, Mangi wa Mashati, Mangi wa Mengwe nk. Lakini wote waliunganishwa na Mangi Mwitori wa Rombo.
 Vivyo hivyo katika maeneo ya Kibosho, Machame, Siha, Old Moshi, Marangu nk.
Mangi mdogo aliripoti kwa Mangi Mwitori. Mangi Mwitori naye aliripoti kwa Mangi Mkuu aliyeunganisha Wachaga wote.
Kwa mfano kufikia mwaka 1953 Mangi Mwitori wa Vunjo alikua Petro Itosi Marealle, Mangi Mwitori wa Hai alikua Abdiel Shangali, Mangi Mwitori wa Rombo alikua James Selengia Kinabo kabla ya kustaafu mwaka 1952 na John Maruma kuchukua nafasi yake.
Mangi Mwitori alichaguliwa na wamangi wadogo. Kisha wamangi wadogo na wamangi waitori waliunda baraza kuu la uongozi (Supreme council) ambalo lilimchagua Mangi Mkuu.
January 1952 kulifanyika uchaguzi wa kumchagua Mangi Mkuu wa Wachaga. Wagombea walikua watano. Abdieli Shangali wa Machame, Jackson Kitali wa Mbokomu (Old Moshi), Petro Marealle wa Vunjo, John Maruma wa Rombo, na Thomas Marealle wa Marangu.
Baada ya kila mgombea kunadi sera zake, hatimaye kura zilipigwa na Mangi Thomas Marealle kutangazwa mshindi, akifuatiwa kwa mbali na ndugu yake Mangi Petro Itosi Marealle, aliyekuwa Mangi Mwitori wa Vunjo.
Mangi Mkuu ndiye aliyekuwa Kiongozi mkuu wa dola ya Wachaga. Baraza la uongozi (Supreme council) ndicho kilikua chombo cha juu kinachosimamia utendaji wa serikali.
Kwahiyo Mangi mkuu alijitahidi sana kushirikiana mangi waitori na mangi wadogo kuhakikisha jamii nzima ya Wachaga inajiletea maendeleo.
Kila Mangi alikua na baraza lake la ushauri lililojulikana kama ‘baraza la wachili’, ambalo lilifanya kazi kama baraza la mawaziri kwa sasa.
Ushirikiano huu ulifanya dola ya Wachaga kupiga hatua kubwa kimaendeleo kuliko jamii nyingi za wakati huo.
Kwa mfano kufikia mwaka 1920 dola ya Wachaga ilikua ya kwanza kwenye ukanda wa Afrika Mashariki kuanzisha na kumiliki gazeti lake (Komkya). Miaka 10 baadae dola ya Buganda (Buganda Kingdom) nayo ilianzisha gazeti lake (Buruuli) na mwaka 1940 Himaya ya Sultani wa Zanzibar (Zanzibar Sultanate) nayo ikaanzisha jarida lake (Imperial).
Si hivyo tu, huduma za maji, umeme, miundombinu ya barabara, hospitali na shule vilifika mapema kulinganisha na maeneo mengine ya nchi. Ikulu ya kisasa ya Mangi Mkuu wa Wachaga, iliyojengwa karibu miaka 100 iliyopita ndiyo inayotumika hadi sasa kama Ikulu ndogo ya Rais kwa mkoa wa Kilimanjaro.
Zilizokuwa ofisi za watendaji wa serikali ya Mangi mkuu (eneo la KDC Moshi) ndio ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Moshi kwa sasa.
Maendeleo haya na mengine mengi, Wachaga waliamini yalitokana na elimu. Kwahiyo mwamko wa elimu ulikua mkubwa hasa baada ya wamisionari kujenga shule na huduma za afya kila walipojenga kanisa. Vitu hivi vitatu viliambatana. Kanisa, Shule, na Kituo cha afya.
Kwahiyo hata kwenye kuchagua viongozi, yule aliyekuwa na elimu nzuri ndiye aliyepewa nafasi kubwa ya kushinda ikiaminika kwamba elimu yake itachochea kasi ya maendeleo. Na hii ni moja ya sababu iliyomfanya Thomas Marealle kushinda kiti cha umangi mkuu mwaka 1952, kwani kati ya wagombea wote yeye ndiye aliyekua na shahada ya uzamili (masters degree) kwa wakati huo.
Kabla ya uhuru kulikua wachumi wawili tu wazawa ambao ni Thomas Marealle na mzee Fredrick Mchauru ambaye walisoma pamoja London School of Economics, kabla ya Marealle kupata ufadhili Cambridge University (Trinity College).
Iliaminika pia kwamba Uingereza ilitaka dola ya Wachaga ijitenge kutoka Tanganyika na itafute uhuru wake yenyewe, kama Rwanda na Burundi zilivyojitenga kutoka Tanganyika baada ya vita vya kwanza vya dunia, wakati huo zikiitwa Ruanda-Urundi.
Hata hivyo mpango huo ulishindikana kwa kuwa Tanganyika ilikua ‘Trusteeship colony’ ya Umoja wa mataifa, na Uingereza alikabidhiwa tu aisimamie hadi iweze kujitawala. Kwahiyo hoja ya Muingereza ilitupwa kwa maelezo kwamba wakati wa kugawanya bara la Afrika pale Berlin mwaka 1984/85 hakuna nchi inayoitwa ‘Chagga state’ iliyogawanywa. Hivyo uhuru unaopaswa kuwa wa Tanganyika kwa ujumla na sio wa jamii moja moja.
Baada ya jaribio hilo kushindwa, inadaiwa shirika la ujasusi la Uingereza (M16) lilimpendekeza Mangi Thomas Mareale kuwa Rais wa kwanza wa Tanganyika baada ya uhuru.
Katika moja ya barua za Richard Turnbull (Gavana wa mwisho wa Uingereza) kwenda kwa shirika la ujasusi la nchi hiyo (M16) ilieleza mapendekezo hayo kwa Thomas Mareale.
Sehemu ya nyaraka hiyo iliyoandikwa mwaka 1958 ilisema ‘I consider Thomas Marreale an outstanding Chagga leader. I dont know him personally but he would be the leader of Tanganyika if British had to leave. However he lack support from other tribes’.
Turnbull alikua akiwaelezea M16 kuhusu Mangi Thomas Marealle na umahiri wake katika uongozi. Hata hivyo alionesha hofu kuwa Marealle hakuwa na ushawishi mkubwa kwa makabila mengine nje ya Wachaga.
Na hii ni moja ya hofu kubwa aliyokua nayo Mwalimu Nyerere wakati wa kudai uhuru. Alipofika uchaggani alikuta dola ya Wachaga ina mamlaka kamili. Ilikua na ‘well defined leadership structure’, bendera yake, wimbo wake, na askari wake.
Nyerere alisema ili Tanganyika iwe uhuru lazima dola ya Wachaga ife kwanza, kwa sababu hatuwezi kuwa na taifa moja ndani ya taifa jingine. Mwaka 1961 Nyerere aliagiza bendera ya Tanganyika isipandishwe kabla bendera ya Wachaga haijashushwa kwanza. Tarehe 8 December 1961 saa 5 usiku bendera ya Wachaga ilishushwa katika Ikulu ndogo ya Moshi, na muda mfupi baadae (saa 6 usiku, December 9) bendera ya Tanganyika ikapandishwa.
Hata hivyo hofu ya Nyerere haikua na mashiko kwa sababu Mareale mwenyewe alimpa ushirikiano mkubwa wakati wa kudai Uhuru. Na ili kuonesha kwamba hakuwa na mpango wowote wa kumhujumu, aliamua kujiuzulu nafasi yake ya umangi mkuu mwaka 1960, na kuruhusu askari wake kujiunga na jeshi la Tanganyika.
Pichani ni wagombea watatu kati ya watano walioshiriki uchaguzi wa Mangi Mkuu mwaka 1952. Kutoka kushoto ni Mangi Thomas Mareale aliyeshinda uchaguzi huo), Mangi John Maruma (Mangi Mwitori wa Rombo), na Abdieli Shangali (Mangi Mwitori wa Machame).
Kwanini Wachaga hupenda kwenda kwao mwishoni mwa mwaka?
Kumekuwa na dhana nyingi potofu juu ya Wachaga kwenda kwao kipindi cha mwisho wa mwaka, maarufu kama “kwenda kuhesabiwa”.
Je ni kweli Wachaga huenda kuhesabiwa? Jibu ni Hapana.. si kweli. Wachaga hawaendi kuhesabiwa.
SWALI; Sasa kama hawaendi kuhesabiwa neno “kuhesabiwa” limetoka wapi na kwanini litumike kwao tu sio kwa Wasukuma, Wamasai, Wayao au Wamakonde?
JIBU; Neno “kuhesabiwa” limetoholewa kutoka neno la Kiebrania “מִפקָד אוֹכלוּסִין” linalomaanisha Wana wa Israel kurudi kwao kwa ajili ya kuhesabiwa.
Mara nyingi Waisrael walikua wanarudi kipindi cha mwisho wa mwaka wa Kiyahudi katika mwezi uitwao “Adar Beit” ambao kwa mujibu wa Kalenda ya Kiyahudi huo ndio mwezi wa mwisho wa mwaka. Na hukaa huko hadi mwezi wa kwanza wa mwaka ambao kwa kiyahudi huitwa “Nissan”.
Utamaduni huu ulitumika katika Israel ya zamani (Ancient Jews) japo kwa sasa haupo tena. Katika kipindi hiki Waisrael walikua wakikutana nyumbani na kupanga mipango ya maendeleo pamoja na kuhesabiwa ili kujua idadi yao kutokana na kutawanyika katika mataifa mengi duniani.
Tangu enzi za Musa miaka zaidi ya 4,000 kabla ya Kristo; Waisrael walikua na utamaduni wa kurudi kwao kuhesabiwa.
Katika kitabu cha 1Nyakati 23:2-3 Biblia inasema “Akawakusanya wakuu wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi. Nao wakahesabiwa Walawi wenye miaka thelathini na zaidi; na jumla yao kwa vichwa, mtu kwa mtu, ikapata thelathini na nane elfu.”
Huu ni udhibitisho wa kuhesabiwa kwa Wana wa Israel zamani hizo. Lakini pia kitabu cha Hesabu 3:14-15 kinasema “Kisha Bwana akanena na Musa huko katika bara ya Sinai, na kumwambia, Uwahesabu wana wa Lawi kwa kuandama nyumba za baba zao na jamaa zao; kila mtu mume tangu umri wa mwezi mmoja na zaidi utawahesabu.”
Maandiko yanayoeleza juu ya kuhesabiwa kwa wana wa Israel ni mengi na unaweza kuyasoma baadae katika (Kutoka 12:37, Waamuzi 20:14, 1 Samweli 11:8, Ezra 2:64).
Kwa hiyo kuhesabiwa ni agizo la Mungu na utamaduni huu wa wana wa Israel kurudi kwao kwenda kuhesabiwa ni utamaduni uliokua maagizo ya Mungu mwenyewe (Jehovah).
Sasa je ikiwa Wachaga hawaendi kuhesabiwa iweje wafananishwe na WaIsrael?
Sababu mbili hufanya Wachaga kufananishwa na utamaduni huu wa Israel wa kuhesabiwa.
SABABU YA KWANZA ni kitendo cha Wachaga kurudi kwao mwishoni mwa mwaka (December) na kukaa huko hadi mwanzoni mwa mwaka mpya (January). Ikumbukwe wana wa Israel nao huenda kwao mwishoni mwa mwaka wa Kiyahudi (Adar Beit) na kurejea mwanzoni mwa mwaka mpya (Nissan). Ufanano huu wa majira hufanya Wachaga nao waonekane kuwa wanaenda “kuhesabiwa” kama waIsrael.
SABABU YA PILI ni mtawanyiko wa jamii hizi mbili. Wana wa Israel wametawanyika katika mataifa mbalimbali duniani. Kutokana na ufinyu wa nchi yao wamejikuta wakisambaa nchi mbalimbali ambapo wanaishi na kufanya kazi huko. Wengine ni wahandisi, madaktari, majemadari wa vita etc. Wana wa Israel wametawanyika mataifa yote ya Ulaya, America na baadhi ya nchi za Asia na Afrika. Pamoja na kutawanyika huku lakini mwisho wa mwaka hukumbuka kurudi kwao.
Kwa upande wa Wachaga nao wametawanyika sana katika mikoa mbalimbali nchini. Mtawanyiko wao unafananishwa na ule wa wana wa Israel kwa sababu mbili. Kwanza eneo lao la makazi (Kilimanjaro) ni dogo na haliwatoshi, sawa na Israel ilivyo ndogo na isivyotosha watu wake. Pili ni “nature” ya mtawanyiko wao. Wachaga kama Waisrael wametawanyika sehemu mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi.
Hakuna mkoa au Wilaya yeyote unaweza kwenda nchini ukamkosa Mchagga. Wametapakaa kila kona ya nchi wakifanya shughuli mbalimbali hususani biashara. Mtu mmoja aliwahi kutania kuwa “ukienda eneo la nchi hii ukakosa Mchagga ondoka haraka maana hapafai kuishi”.. Hii ina maanisha Wachaga wanaweza kuishi katika mazingira yoyote na hali yoyote.
Mtawanyiko wa Wachaga katika maeneo mbalimbali ya nchi hufananishwa na mtawanyiko wa Waisrael katika maeneo mbalimbali ya dunia, na hivyo basi kitendo cha Wachaga kurudi kwao mwishoni mwa mwaka hufananishwa na kitendo cha Waisrael kurudi kwao mwishoni mwa mwaka wa kalenda ya kiyahudi. Tofauti ni kuwa Waisrael huenda kuhesabiwa lakini Wachaga hawaendi kuhesabiwa.
Kama Wachaga hawahesabiwi, wanaenda kufanya nini?
Pengine hili ndio swali la msingi ambalo wengi wanajiuliza. Ikiwa Wachaga hawaendi kuhesabiwa kama ilivyo kwa waisrael, Je wanaenda kufanya nini?
Ukweli ni kwamba Wachaga wanakwenda kwao kwa sababu mbalimbali. Leo nitaainisha kwa uchache sababu 10 zinazorudisha Wachaga kwao kila mwisho wa mwaka. Zipo nyingi zaidi ila kwa kifupi ni kama ifuatavyo;
  1. 1. Kuna wanaokwenda kwao kwa ajili ya kuonana na familia zao na kuwaona wapendwa wao na kujumuika nao kwa ajili ya kufurahia sikukuu za mwisho wa Mwaka huhusani “Krismasi” na “Mwaka mpya”.
Kwa mfano wazazi wako (baba na mama) au ndugu zako wengine (babu, bibi, kaka, dada, shangazi, wajomba etc) hujawaona kwa kipindi cha mwaka mzima. Mmekuwa mkiwasiliana tu kwa simu. Hivyo basi December huwa ni kipindi kizuri cha kurudi nyumbani na kuwaona na kuwajulia hali.
  1. 2. Pia kipindi hiki hutumika kupanga mipango ya maendeleo ya familia kama vile kujenga. Kwa kuwa watoto wote wa familia hukutana kipindi hiki basi huweka mipango ya maendeleo kwa familia yao. Wanaweza kupanga kujenga nyumba kwa ajili ya wazazi wao ambao ni wazee, kuweka umeme, maji etc.
Uchaggani ni mojawapo ya maeneo nchini ambako kuna nyumba nyingi za kisasa vijijini na ni mkoa uliofanikiwa kupiga vita nyumba ya Nyasi tangu mwaka 1996.
Ni jambo la Kawaida kukutana na maghorofa ya kisasa kule “Machame Uswaa, Kibosho Kirima, au Mamba Komakundi”.. au ukipita “Uru Mawela, Rombo Mamsera au Kilema Poffo” nyumba zote unazokutana nazo ni self-contzined za kisasa, lakini wanaishi wazee. Watoto wao wapo Shinyanga, Dar, Kigoma, Mwanza etc wanatafuta maisha. Mipango hiyo ya kujenga na kuhudumia wazazi hupangwa msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.
  1. 3. Msimu huu wa sikukuu hutumika kupatanisha ndugu, jamaa au marafiki waliokosana. Wazee huitwa na kuzungumza na pande zote mbili kisha kuwapatanisha. Mkikubali kuelewana basi huchinjwa mbuzi kama ishara ya furaha ambapo jamii yote hujumuika kwa kula na kunywa.4. Kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ndio kipindi kizuri ambacho vijana hukitumia kutambulisha wachumba zao nyumbani. Unaweza kuwa unaishi Dar na umepata mchumba wa Morogoro. Lakini ndugu zako wametawanyika. Wengine wapo Tabora, wengine Mwanza, wengine Mbeya. Huwezi kupita na mchumba wako kote huko kumtambulisha. Kwahiyo “option” nzuri ni kusubiri msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka ambapo ndugu zako wote watakuwepo nyumbani ndipo umpeleke mchumba wako kumtambulisha, na kupanga mipango ya ndoa.5. Kuwaleta watoto wafahamu ndugu zao na wafahamike nyumbani. Unaweza kuwa unaishi Dar na familia lakini ndugu zako wanaishi na familia zao maeneo mengine ya nchi, watoto wenu hawafahamiani maana hawajawahi kuonana. Hivyo mkikutana nyumbani msimu wa sikukuu ni kipindi kizuri cha watoto wenu kufahamiana na kufahamu asili yao.
Pia ikiwa umejaliwa mtoto ukiwa huko unakofanyia shughuli zako lakini wazazi wako hawajamuona mjukuu wao, hiki ni kipindi kizuri cha kuwapelekea wazazi wako mjukuu wao wamuone na kumpa baraka.
  1. 4. Kushiriki shughuli za kijamii (charity work). Wachaga wengi ni waumini wazuri sana wa dini iwe ukristo au uislamu. Hivyo kipindi cha msimu wa sikukuu hutenga muda wa kutembelea wagonjwa, Yatima na Wasiojiweza na kuwapa misaada mbalimbali. Kwa wale Wakristo huita “sadaka ya Epifania”.7. Kipindi hiki hutumika pia kufanya usafi na kurekebisha maeneo waliyopumzika wapendwa wetu (makaburi). Wachaga kama ilivyo binadamu wengine hutenga maeneo maalumu ya kuzikia ndugu zao; na mara nyingi kila familia ina eneo lake.
Kwa hiyo ikiwa kuna ndugu amefariki na akazikwa basi msimu huu huwa ni kipindi kizuri cha kujengea makaburi kama kumbukumbu ya sehemu walipopumzika wenzetu.
Bahati mbaya wapo watu wanaohusisha utamaduni huu na matambiko. Kwanza ieleweke kujengea makaburi si dhambi na si matambiko. Hata Yakobo alipofia kule Misri alipoenda kwa mwanae Yusufu alizikwa kwenye Kaburi lililojengewa (Matendo 7:15-16). Hivyo basi ni vizuri ikaeleweka kuwa kujengea makaburi si dhambi.
Na mara nyingi uchaggani kabla ya kujengea Kaburi kiongozi wa dini huitwa na kufanya sala, kabla ya shughuli ya ujenzi haijaanza. Kwahiyo hakuna nafasi ya matambiko.
Ikiwa kuna mchagga anafanya matambiko wakati wa kujengea makaburi ichukuliwe kuwa ni tabia ya mtu binafsi na isihuhishwe Wachaga wote. Kwani wapo watu wa makabila mengine hufanya matambiko pia lakini huwezi kusema jamii yote hutambika.
  1. 5. Msimu huu wa sikukuu ni kipindi kizuri ambacho Wachaga hukitumia kupanga na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ya jamii yao kama vile mashule, hospitali, Maji, barabara n.k
Kwa mfano zipo barabara nyingi ambazo zimejengwa kwa nguvu ya wananchi wenyewe kwa kuamua kujichangisha bila kusubiri serikali ifanye. Barabara ya Uru Kusini ni mojawapo. Mipango hii hupangwa msimu huu wa sikukuu.
  1. 6. Msimu huu hutumika kwa ajili ya mapumziko ya familia baada ya mahangaiko ya mwaka mzima. Ni wakati wa familia kutulia pamoja kutafakari mipango ya mwaka uliopita na kuweka mipango mipya ya mwaka unaofuata.
Ndugu na jamaa hukutana pamoja na kufurahia sikukuu za “Krismasi” na “mwaka mpya” kwa kula na kunywa hasa vyakula vya asili kama “kisusio, faya, supu ya mbuzi iliyopikwa kiasili kwa kuchanganywa na majani aina ya “mahombo” na vyakula vingine bila kusahau kinywaji aina ya mbege.
  1. 7. Kipindi hiki hutumiwa kujenga na kukarabati nyumba za ibada. Ni wazi kuwa Kilimanjaro ni miongoni mwa maeneo ambayo kuna nyumba nzuri na za kisasa za Ibada.
Kanisa kubwa na la kisasa kama la KKKT Old-Moshi Rau, au La RC Kristu Mfalme, Au TAG Kilimanjaro Revival, au Msikiti wa kisasa kama wa Riadha, ni nadra kuvipata mahali pengine. Au Kanisa la kale kama la KKKT Old-Moshi Kidia lililojengwa mwaka 1843 utalipata wapi kwingine?
Mipango ya ujenzi wa nyumba hizi za ibada za kisasa na kukarabati zile za zamani hufanywa msimu huu wa sikukuu.
Pia Wachaga wengi hupenda kwenda kwao kwa kuwa ibada zote katika msimu huu huongozwa kwa kichagga. Yani kuanzia usomaji wa misa, mahubiri hadi nyimbo huimbwa kwa kichagga, wakati huo nyumba za ibada zimepambwa kwa mapambo ya asili kama “Makurera, makangachi, migomba imechimbiwa vichumini (njia za kwenda nyumbani)” etc.
Hii huongeza nakshi na kufanya mtu ajisikie kupungukiwa kitu ikiwa hatakuwepo Nyumbani msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.
Utamaduni huu wa Wachaga ni mzuri sana, na kuna mengi jamii nyingine zinaweza kujifunza kupitia Wachaga kama ambavyo Wachaga wanaweza kujifunza kupitia jamii nyingine.
Bendera Ya Wachaga
Halmashauri ya Uchaga ilikuwa na bendera yake ambayo ipo hadi leo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, yenye nembo tano kuu:
1. Mlima Kilimanjaro uliochorwa katikati ya bendera ukionyesha mandhari nzuri ya kilele cha Kibo. Kilele cha Kibo kinatoa maji safi na ni kielelezo cha umoja wao.
2. Chini ya kilele cha Kibo, upande wa kushoto wa bendera kuna mgomba wenye ndizi. Hiki ni chakula kikuu cha Wachaga.
3. Upande wa kulia wa bendera ni tawi la mbuni ukiwa na matunda yake. Kahawa ni zao lililowaletea maendeleo.
4. Bendera imezungukwa na matawi ya ‘sale’ lenye matawi mawili (draceana plant). Matawi haya yamefanya mduara kuzunguka kilele cha Kibo, mgomba wa ndizi na tawi la zao la kahawa. Masale ni mmea unaoheshimiwa sana na Wachaga wote.
Ni alama ya amani. Masale hutumika katika sherehe na shughuli zote za kimila zinazofanywa na Wachaga. Majani yake ni kijani kibichi yanayoonyesha jinsi Kilimanjaro ilivyo na rutuba nzuri inayostawisha mazao ya kila aina.
5. Juu kidogo ya kilele cha Kibo yupo chui ambaye amejipumzisha. Chui ni alama kuu ya mamlaka ya Wachaga.
Hapo awali kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro walikuwepo chui wengi wa rangi nyeusi lakini kutokana na ongezeko la watu pamoja na uharibifu wa mazingira chui hawa wametoweka.

Print this item

  Lugha za Kibantu
Posted by: MwlMaeda - 06-15-2021, 07:24 AM - Forum: Historia ya makabila ya kibantu - No Replies

   
Lugha za Kibantu ni kundi la lugha ambalo ni tawi la lugha za Niger-Kongo.
Lugha za Kibantu huzungumzwa hasa katika nchi za Nigeria, Kamerun, Guinea ya Ikweta, Gabon, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya, Tanzania, Komori, Msumbiji, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Angola, Namibia, Botswana, Lesotho, Swaziland na Afrika ya Kusini.
Uenezi huo unaonyesha kwamba kundi la lugha za Kibantu ni kubwa kabisa barani Afrika, na idadi ya wanaozitumia ni takriban watu milioni 310.
Neno Bantu, maana yake ni watu katika lugha nyingi za kundi hilo. Shina lake ni -ntu, na kiambishi awali cha ba- kinaonyesha uwingi wa viumbehai. Kwa sababu hiyo, mtaalamu Wilhelm Heinrich Immanuel Bleek (aliyeishi tangu mwaka 1827 hadi 1875) alitumia neno hilo kwa kurejea kundi la lugha hizo. Bleek alilinganisha sarufi za lugha mbalimbali za Kibantu, na baadaye Carl Meinhof alimfuata katika utafiti huo.
Kuna mamia ya lugha za Kibantu; wataalamu wengine wanahesabu 300, wengine wanahesabu 600. Mtaalamu Malcolm Guthrie aliziainisha kulingana na maeneo ya kijiografia. Kila eneo limepata herufi yake — A, B, C, D, E, F, G, H, K, L, M, N, P, R na S — na ndani ya kila eneo kuna tarakimu tena. Pia, Guthrie alichunguza lugha ya nasaba ambayo ni chanzo cha lugha zote za Kibantu.
Tabia za Kibantu na historia ya lugha
Lugha za Kibantu zina tabia mbalimbali za pamoja. Kati ya tabia hizo kuna viambishi awali na ngeli za nomino.
Kutokana na sifa hizo wataalamu wamekadiria kwamba asili ya lugha za Kibantu ilikuwa katika maeneo ya Kamerun ya Kusini; kutoka huko wasemaji asilia wa Kibantu katika milenia ya pili KK walihamia Kongo hadi Zambia. Waliendelea kuhamahama na kupanuka hadi kufika maeneo yote walipo sasa.
Sehemu kubwa ya maeneo ya wasemaji wa lugha za Kibantu zilikaliwa awali na wasemaji wa lugha za Khoisan. Wataalamu wamekisia kwamba Wabantu walifaulu kuenea kutokana na maarifa yao ya kilimo na hasa matumizi ya chuma katika zana za kilimo na pia silaha.
Lugha za Kibantu zenye wasemaji wengi
Kati ya lugha za Kibantu zinazotumika zaidi kuna Kiswahili na Kilingala. Lugha zenye wasemaji wengi kama lugha ya kwanza ni Kizulu na Kishona.
(Idadi ya wasemaji ni makadirio tu; bado ina tofauti kati ya makala na makala)
  • Kiswahili na lahaja zake (wasemaji milioni 75) : Tanzania, Kenya, Uganda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda, Burundi, Komori, Mayotte, Msumbiji, Somalia.
  • Kinyarwanda-Kirundi : (wasemaji milioni 15): Rwanda, Burundi
  • Lingala (wasemaji milioni 10): Angola, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Gabon
  • Chichewa (wasemaji milioni 9) : Malawi
  • Kizulu (wasemaji milioni 9) : Afrika Kusini
  • Kisukuma (wasemaji milioni 9) : Tanzania.
  • Kishona (wasemaji milioni 7) : Msumbiji, Zambia, Zimbabwe
  • Gikuyu (wasemaji milioni 7) : Kenya
  • Kikongo (wasemaji milioni 6) : Angola, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
  • Chiluba (wasemaji milioni 6) : Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Angola

Print this item

  UFAHAMU NA UFUPISHO (ZOEZI)
Posted by: MwlMaeda - 06-15-2021, 07:14 AM - Forum: Mitihani - No Replies

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata

 
 Niliendelea mbele kidogo, nikasema, nikatazama kulia, kushoto, mbele nyuma halafu kushoto tena, huku nikiwa makini zaidi. Moyo wangu uliniambia kwa huruma “cherwa, kamwe usipige hatua yoyote toka hapo ulipo na sasa tazama chini karibu na miguu yako.” Kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firaubi, niliona Joka kubwa ambalo lilikuwa limepanua mdomo wake mithili ya  pango. Niligutuka ghafla na kuhamaki, nilijupa moyo nikaruka kuelekea nyuma, mara joka lile likageuka binti mzuri mwenye umri wa kuolewa, binti yule alinisogelea ppale nilipokuwa nisijue la kufanya. “nataka kuongea na wewe, nimetoka mbali kwa ajili yako, leo matatizo yako yataisha” alisema binti yule aliyeonekana mwenye furaha na huruma kuu pale nilipokuwa nimesimama sikujua kuwa ninabubujikwa na machozi. “nasema tulia, usilie uwe na matumaini sauti ya msichana iliingia masikioni mwangu kama vile radi au upepo uvumao kwa nguvu.
Palepale nilianguka, giza likaniteka na nikapoteza fahamu palepale mtoni, nilizinduka na kugundua kuwa nilikuwa mikononi mwa watu nisiowafahamu nikiwa nimevalishwa kanzu nyeupe, niliangalia saa katika simu yangu ilikuwa ni saa tisa na nusu usiku. Sikutambua nilipokuwa lakini niligundua kuwa pale ni msituni, mara ikasikika sauti ya upole, “upo katika mikono salama, usiogope.”
 
Maswali
(i) Eleza maana ya maneno/tungo zilizopigiwa mstari
(ii) Kwa nini muhusika anasema alijipa moyo?
(iii) Msichana aliyemtokea muhusika alikuwa ametoka wapi?
(iv) Muhusika alipopoteza fahamu alikuwa katika mazingira gani?
(v) Andika kichwa cha habari hii kwa maneno yasiyozidi matano.2. Fupisha habari hiyo kwa (1/3)

Print this item

  WASIFU WA SITI BINTI SAAD
Posted by: MwlMaeda - 06-14-2021, 07:42 PM - Forum: Wasifu/Tawasifu - No Replies

Siti binti Saad alizaliwa katika kijiji cha Fumba, Zanzibari mwaka 1880. Alipozaliwa alipewa jina la ‘Mtumwa’ hii ni kwa vile alizaliwa katika kipindi cha utumwa wa Kiarabu. Jina la Siti alipewa na mkabaila mmoja wa kiarabu.Baba yake bwana Saadi alikuwa ni Mnyamwezi kutoka Tabora na mama yake alikuwa ni Mzigua toka Tanga, lakini wote wawili walizaliwa Zanzibari. Hali ya maisha ya familia yao ilikuwa ni duni sana na walijishughulisha zaidi katika shughuli za kilimo na ufinyanzi kazi ambazo Siti alijifunza na kuzimudu vizuri pia.Kama waswahili wasemavyo ‘kuzaliwa masikini si kufa masikini’ Siti alibarikiwa kuwa na kipaji cha pekee cha uimbaji. Kipaji hiki kilimsaidia sana tangu siku za awali za maisha yake kwani alitumia uimbaji wake kuuza vyungu vya mama yake alivyokuwa akimsaidia kuvitembeza. Siti alipoimba sauti yake iliweza kupaa na kusafiri kwa umbali wa maili nyingi na hii ndio ilikuwa ishara ya watu kujua kwamba vyungu vya kina Mtumwa vinapita leo. Alifananishwa kuwa na mapafu yenye nguvu kama ya simba kutokana na alivyoweza kupaza sauti yake mbali na bila kuachia pumzi.Kutokana na wakati huo elimu kwa watoto wa kike kutotiliwa mkazo, Siti hakuwahi kwenda shule wala kuhudhuria mafunzo ya Kurani. Hivyo mnamo mwaka 1911 aliona ni bora ahamie mjini ili kubooresha maisha yake zaidi. Ujio wake wa mjini ulikuwa wa neema kwani alikutana na bwana mmoja wa kundi la muziki wa Taarabu la “Nadi Ikhwani Safaa” aliyeitwa Muhsin Ali. Katika kipindi hicho hilo ndilo lilikuwa kundi pekee la muziki wa taarabu lililoanzishwa na Sultani mpenda starehe na anasa bwana Seyyid Barghash Said. Kundi hili lilikuwa ni la wanaume peke yake , wanawake hawakuruhusiwa kujiunga na vikundi vya muziki kwa vile ilikuwa ikichukuliwa kama ni uhuni. Bwana Muhsin alikiona kipaji cha pekee cha Siti na hivyo akajitolea kumfundisha kuimba kwa kufuata vyombo vya muziki na lugha ya kiarabu. Baada ya hapo alikwenda kumtambulisha kwa wanamuziki wenzie wa “Nadi Ikhwani Safaa” ambao bila kusita wakaanza kufanya naye maonyesho mbalimbali katika jamii. Walipata mialiko mingi hasa kutoka kwa Sultani na matajiri wengine wa Kiarabu, pia katika maharusi na sherehe zingine mbalimbali, inasemekana ulifika wakati ambapo sherehe ilishindwa kufana kama Siti binti Saadi hakuwepo kutumbuiza. Siti alikuwa ni moto wa kuotea mbali na jina lake lilivuma kwa haraka sana hadi nje ya mipaka ya nchi na bara la Afrika. Na punde Siti alianza kufananishwa na ‘Umm Kulthum’, mwimbaji mahiri wa kike aliyetamba wakati huo kutoka Misri.Kama nilivyosema moto wa Siti ulikuwa si wa kuusogelea karibu, mwaka 1928 kampuni ya kurekodi muziki ya Columbia and His Master’s voice yenye makazi yake Mumbai Indiailisikia umaarufu wa Siti binti Saadi na hivyo ikamwalika yeye pamoja na kundi lake kwenda kurekodi kwa lugha ya Kiswahili ili kujaribu kama muziki wake utauzika. Kampuni ile haikuweza kuamini jinsi muziki ule ulivyouzika kwa kasi kubwa kwani wastani wa santuri 900 ziliweza kuuzika katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo, na hadi kufikia 1931 santuri 72,000 zilikuwa zimeuzwa. Kutokana na kusambaa kwa santuri hizi, umaarufu wa Siti ulizidi mara dufu watu kutoka sehemu mbalimbali za dunia walikuwa wakija Zanzibari kuja kumwona. Mambo yalizidi kuwa mazuri kwa Siti hadi ikafikia hatua kampuni ya kurekodi ya Columbia kuamua kujenga studio ya kurekodi muziki palepale Zanzibar maalumu kwa ajili ya Siti binti Saadi.Hatua hiyo ya hadi kujengewa studio iliwaumiza wengi wenye wivu, hivyo wakaanza kumtungia nyimbo za kumkejeli ili kumshusha na hasa walitumia kigezo kwamba hana uzuri wa sura, nyimbo nyingi ziliimbwa lakini huu ndio uliovuma sana:-
    Siti binti Saad kawa mtu lini,
    Kaja mjini na kaniki chini,
    Kama si sauti angekula nini?
Na yeye kwa kujua hila za wabaya wake, akaona isiwe taabu akajibu shambulio namna hii:-
   Si hoja uzuri,
   Na sura jamali,
   Kuwa mtukufu,
   Na jadi kebeli,
   Hasara ya mtu,
   Kukosa akili.
Kwa kujibu shambulio hilo kwa namna yake aliwafunga midomo wale wote waliokuwa wakifumatafuata. Siti pia alikuwa ni mwanamke wa kwanza mwanaharakati katika kipindi chake, alitetea wanawake na wanyonge kwa ujumla, kwani katika kipindi chake watu matajiri walikuwa wakiwaonea masikini na walipofikishwa mbele ya haki waliweza kutoa hongo na kuachiwa huru halafu wewe uliyeshitaki ndiye unayefungwa.Utunzi wake wa wimbo wa Kijiti ulimpatia sifa kubwa kwani ulikuwa ukielezea kisa cha kweli kilichomkuta mwanamke mmoja mgeni kutoka bara, mwanamke huyu alipofika alikutana na Tajiri mmoja ambaye alijifanya amempenda, hivyo akamchukua na kulala naye halafu baadaye akamuua. Tajiri yule alishitakiwa na bahati nzuri walikuwepo mashahidi wawili walioshuhudia tukio lile, lakini kwa vile ni Tajiri alitoa pesa na kesi ikawageukia wale mashahidi na kufungwa.Siti akatoa wimbo huu :-
    Tazameni tazameni,
    Eti alofanya Kijiti,
    Kumchukua mgeni,
    Kumcheza foliti,
    Kenda naye maguguni,
    Kamrejesha maiti.
Siti aliendelea kumwambia katika nyimbo zake kwamba asijethubutu kwenda Dar er Salaam kwa maana watu wenye hasira wanamsubiri na wameapa kwa ajili yake.Siti aliendelea na shughuli yake ya muziki hadi uzeeni, muda mfupi kabla ya kifo chake alikutana na mwandishi maarufu na mwanamashairi Shaaban Robert ambaye alimhoji na kuweza kuandika wasifu wake katika kitabu alichokiita ” Wasifu wa Siti binti Saadi.” Wasifu huu unaonekana kuwa ndio bora zaidi uliowahi kuandikwa katika fasihi ya Tanzania. Kitabu hiki kinatumika kufundishia shule za sekondari za Tanzania.Tarehe 8 Julai 1950 Siti binti Saadi alifariki dunia na kuacha pengo kubwa katika fani ya Taarabu. Ingawa pengo hilo haliwezi kuzibika lakini kuna watu wengi walioweza kuibuka na umaarufu wa kuimba taarabu kupitia kwake, mfano hai ni Bi Kidude.Hata baada ya kifo chake jina lake bado linatumika sana kama kielelezo cha ushujaa wake, Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania (TAMWA), kimetumia jina lake kulipa jina gazeti la chama chao “Sauti ya Siti”. Hadi leo hii Siti hutumika kama kipimo cha kufundishia uimbaji wa Taarabu. Na anakumbukwa katika historia yake ya kuwa mwanamke wa kwanza Afrika mashariki kurekodi muziki katika santuri.

Print this item

  TAWASIFU YA SHAABAN ROBERT
Posted by: MwlMaeda - 06-14-2021, 07:25 PM - Forum: Wasifu/Tawasifu - No Replies

KATIKA kitabu chake cha tawasifu “MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI” Shaaban Robert anasimulia dhiki, adha na udhalili alioupitia, pengine kwa sababu ya Uafrika wake, kipindi cha ukoloni akiwa katika safari ya kikazi kama mtumishi wa serikali;
ABIRIA CHEO CHA PILI
DARAJA yangu katika kazi sasa ilikuwa imeniwezesha kusafiri kama abiria wa cheo cha pili katika gari moshi. Mapendelea haya yanayotamaniwa yalinijia baada ya miaka kumi na nne ya kazi serikalini. Julai 13, 1944, nilichukua tikiti, na baada ya kuagana na marafiki, nikasafiri kwenda Mpwapwa. Nilishuka Korogwe kungoja safari ya lori. Karibu ningalilala nje Korogwe kwa ukosefu wa malazi kwa abiria Waafrika., lakini mtu mmoja aliyenijua zamani alinichukua kwake akanipa malazi mema. Asubuhi nilionyesha tikiti zangu za safari kwa msimamizi wa safari. Mtu huyu alinitupia jicho kwa haraka kisha akaamuru nijipakie katika lori.
Palikuwa na malori manne tayari kwa safari siku ile. Nilikwenda nikajipakia katika lori la abiria cheo cha pili. Mimi nilikuwa msafiri wa kwanza kujipakia. Dakika chache baadaye loro letu lilijaa abiria. Abiria Waafrika tulikuwa mimi na watoto wangu tu. Wengine wote walikuwa ni Wahindi. Karibu na dakika ya mwisho kusafari pakaja Wahindi wanne wengine. Kuwapa watu hawa wanne nafasi katika lori nililojipakia mimi ilipasa watu wanne waliokuwa wamekwisha kuingia washuke. Msimamizi wa safari, Mhindi vilevile, hakuona mtu mwingine wa kushuka ila mimi. Baridi ina mzizimo siku zote kwa kondoo mwenye manyoya haba. Kwa maneno ya karaha alinilazimisha kushuka chini nikajipakie katika lori la abiria wa cheo cha tatu au la mizigo. Nilimkumbusha msimamizi wa safari kuwa mimi ni abiria wa cheo cha pili ambaye nilikuwa nikisafiri kwa kazi ya serikali; nilitangulia kujipakia mahali nilipostahili kukaa; alikuwa hana haki ya kuniteremsha; iwapo ililazimu kutenda atakavyo ililazimu vilevile yeye kunipa stashahada ya kuonyesha namna ilivyosafiri kutoka Korogwe. Kwa maneno hayo ulimi wa msimamizi wa safari ulianza kupotoka akadai kuwa aliweza kuzuia kusafiri lori nililoingia.
Kundi kubwa la watazamaji lilikuwepo. Karibu watu wengi katika kundi lile walicheka kwa maneno ya msimamizi wa safari. Kivumo cha kicheko kilichemsha hasira yake akaamuru niteremshwe chini kwa nguvu. Matarishi waliokuwa chini ya amri yake walitii wakawa tayari kunijia wanikamate na kunitupa chini kama mtumba, lakini kitu gani sijui kiliwafanya kusita kutimiza amri ya bwana wao. Halafu nilisikia kuwa desturi ya matarishi wale ilikuwa kutii na kutimiza kila amri njema waliyopewa, na kuacha mbali kila amri mbaya hata katika hatari ya kutolewa kazini mwao. Nilifurahi sana kusikia habari hii. Idadi ya watu wema ni kubwa siku zote kuliko jumla ya watu wabaya.
Siku zangu zilikuwa zikihesabiwa. Sikutaka kuchelewa bure pale Korogwe. Niliita watu kuja kushuhudia mwamale niliotendewa na tabia ya msimamizi wa safari. Watu wengi walikuwa tayari kunipa sahihi za mikono yao kuwa walishuhudia yote yaliyotokea. Kisha mimi na watoto wangu tulishuka na kujipakia katika gari jingine. Nafasi iliyokuwa imebaki mle garini ilikuwa si kubwa. Basi tulikaa juu ya mizigo yetu. Kutoka Korogwe tulikwenda Morogoro. Mchana wote ulituishia njiani. Hii ilikuwa siku ya pili ya safari yangu, nikafurahi kushuka katika gari.
Saa mbili na nusu usiku nilijipakia katika gari moshi lililotoka Dar es Salaam hata saa tisa usiku nikashuka Gulwe. Kutoka Gulwe nilichukuliwa na lori la Idara ya Utunzaji wa Wanyama kwenda Mpwapwa. Saa kumi alfajiri nikawa Mpwapwa. Mwisho wa safari yangu ilikuwa ni Kikombo, lakini niliambiwa nikae juu ya gari hata saa moja asubuhi wakati mwendeshaji wetu alipoingia nyumbani kwake kulala. Nje kulikuwa kukizizima sana kwa baridi na umande na lori letu lilikuwa wazi. Taya za watoto wangu zilitingishika na meno yakagongana kwa kipupwe. Julai ni mwezi wa kipupwe kikali pande zile za dunia. Mbwa hafi maji akiona ufuko, na sisi kwa kuwa sasa tulikuwa karibu kufika mwisho wa safari yetu jaribu la baridi halikutufadhaisha sana. Tulikuwa na mablanketi yaliyoweza kuzuia mzizimo wake kutudhuru. Tulijifunika mablanketi yetu tukasaburi kuche polepole.
Saa moja na nusu asubuhi nilikuwa mbele ya msimamizi wa Afisi ya Idara ya Utunzaji wa Wanyama. Huyu alikuwa ni Mzungu. Hakuwa tayari kushikana mikono na mimi kama nilivyozoea kuona Wazungu wengine. Labda mimi nilikuwa si kitu mbele yake lakini tuliongea vema. Alisema kuwa nitapata nyumba lakini kwa namna maneno yalivyotamkwa niliweza kufahamu kuwa idara ilikuwa na dhiki ya makao mema. Dhiki hii ilikuwa imeenea duniani wakati ule. Bati na simenti vilikuwa adimu kupatikana kwa sababu ya Vita Kuu Na. 2. Hii ilikuwa ni Jumapili, siku ya tatu ya safari yangu. Nilipewa ruhusa nikapumzike nihudhurie kazini Jumatatu asubuhi.
*** Vitabu vya sheikh Shaaban Robert vimerejewa kuchapwa upya, na sasa vinapatikana kwa wingi madukani, hususani jijini Dar es Salaam. Ni uzalendo wa kujivunia kwa kila Mswahili kumiliki na kuzisoma nakala za vitabu vya gwiji huyu na “baba wa Kiswahili”.
ORODHA YA KAZI ZA FASIHI ALIZOANDIKA SHAABAN ROBERT

1. MWAFRIKA AIMBA (1969), Nelson. Nairobi

2. ALMASI ZA AFRIKA (1971), Nelson, Nairobi

3. KOJA LA LUGHA (1969), Oxford, Nairobi

4. INSHA NA MASHAIRI (1967), Nelson, Nairobi

5. ASHIKI KITABU HIKI (1968), Nelson, Nairobi

6. PAMBO LA LUGHA (1968), Oxford, Nairobi

7. KIELEZO CHA FASILI (1962), Nelson, Nairobi

8. MASOMO YENYE ADILI (1959), Art&Literature, Nairobi

9. MAPENZI BORA (1969), Nelson, Nairobi

10. TENZI ZA MARUDI MEMA NA OMAR KHAYYAM (1973), TPH, Dar-es- salaam

11. UTENZI WA VITA VYA UHURU (1961), Oxford, Nairobi

12. ALMASI ZA AFRIKA NA TAFSIRI YA KIINGEREZA (1960), Art&Literature, Nairobi

13. MASHAIRI YA SHAABAN ROBERT (1971), Nelson, Nairobi 14. SANAA YA USHAIRI (1972), Nelson, Nairobi. Na vitabu vya nathari vya Sheikh Shaaban Robert ni:

15. KUFIKIRIKA (1968),Oxford, Nairobi

16. WASIFU WA SITI BINTI SAAD (1967), Art&Literature, Nairobi 17. MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI (1949), Nelson, Nairobi

18. KUSADIKIKA (1951), Nelson, Nairobi

19. ADILI NA NDUGUZE (1977), TPH, Dar-es- salaam

20. UTU BORA MKULIMA (1968), Nelson, Nairobi

21. SIKU YA WATENZI WOTE (1968), Nelson, Nairobi

22. KIELELEZO CHA INSHA (1954), Witwatersand, Nairobi

23. BARUA ZA SHAABAN ROBERT 1931- 1958, (2002), TUKI, Dar- es- salaam

24. MITHALI NA MIFANO YA KISWAHILI (2007), TUKI, Dar-es- salaam

Print this item

  WASIFU WA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
Posted by: MwlMaeda - 06-14-2021, 07:20 PM - Forum: Wasifu/Tawasifu - No Replies

Aprili 13, mwaka 1922, safari ndefu ya maisha ya Mwalimu Kambarage Nyerere iliyochukua miaka 77 na miezi 6 ilianza Mwitongo kijijini Butiama, kilomita takribani 30 kutoka mji wa Musoma, mashariki mwa Ziwa Victoria lililoko kaskazini mwa Tanzania. Siku hiyo mvua kubwa ilionesha. Mama Mgaya Nyang’ombe, aliyekuwa mke wa tano kati ya 23 wa Chifu Nyerere Burito wa Zanaki, alijifungua mwanae wa pili. Kwa desturi za kabila la Wazanaki, mtoto wa kike ama wa kiume aliyezaliwa siku ya mvua alipewa jina la KAMBARAGE (mzimu wa mvua).
Kambarage alikuwa mtoto wa maskini kama walivyokuwa watoto wengine kijijini. Ingawa baba yake alikuwa Chifu (Mtemi), cheo hicho alichopewa wakati wa utawala wa Kijerumani hakikuwa na maslahi yoyote ya maana. Kwa desturi za makabila mengi, watoto walilelewa na kutunzwa na mama zao.  Kwa hiyo, Mama Mgaya alijitegemea mwenyewe katika kuwalea wanawe 6 alioishi nao kwenye kibanda cha udongo, na paa la nyasi. Kambarage alipofikia umri wa kuelewa mambo, alimuhurumia sana mama yake na kumsaidia kazi kwa kadri alivyoweza.
Eneo la Mwitongo lilikuwa na mandhari ya kupendeza ya kilima kidogo kilichozungukwa na vichaka na mawe. Mtoto Kambarage alicheza michezo ya kujificha kwenye vichaka na kukimbiza pimbi na tumbili kwenye mawe.  Alichunga mbuzi za mamaye na alipofikia umri wa kutosha, alienda na vijana wenziwe kuwinda porini. Pamoja kumsaidia mamaye alipata muda wa kuwa karibu na babaye na kujifunza utamaduni wa kizanaki.
Siku moja, akiwa na miaka 10 baba yake alimtuma afuatane na mama yake wa kambo kwenda kwenye kijiji kingine kuhudhuria msiba wa jamaa wa mama huyo. Wakati wa kurudi walipewa mbuzi. Kambarage alimfunga kamba mbuzi na kumwelekeza njia. Mbuzi akagoma. Wakati wanakukurushana naye mzee mmoja akamwambia atamrahisishia kazi. Mzee yule akang’oa nywele kidogo kutoka kichwa cha Kambarage na manyoya kidogo toka kichwa cha mbuzi akachanganya na mizizi fulani, akatafuna na kumpa mbuzi akala. Yule mbuzi akamfuata Kambarage mpaka wakafika nyumbani Mwitongo bila kumsumbua!
Akiwa na umri wa miaka 11 baba yake akamtolea Kambarage mahari kwa binti mmoja kijijini. Kwa desturi za Kizanaki mzazi alikuwa na uwezo wa kufanya hivyo ili kuwa na uhakika kwamba hata akifa wanawe wa kiume watakuwa na uwezo wa kuoa.
Kambarage hakutegemea kwamba angeliweza kupata nafasi ya kwenda shule kwa sababu baba yake alikuwa hana uwezo wa kuwasomesha wanawe wote.  Hata hivyo, alidhihirisha kuwa na akili nyingi zilizo muwezesha kujifunza mambo haraka. Alijifunza kucheza bao kutoka kwa baba aliyependa kucheza bao na mama yake aliyekuwa hodari wa mchezo huo. Kila alipopewa nafasi ya kucheza bao na marafiki wa baba yake Kambarage aliweza kuwafunga!  Akili alizozidhihirisha katika mchezo huo ndizo zilizomuwezesha kupata bahati ya kwenda shule. Mmoja wa wazee hao alimshauri Chifu Nyerere amuingize mwanawe shule kwa kuwa alionekana kuwa na akili sana. Ilimuwia vigumu Chifu kuamua lakini mwanawe mkubwa Edward Wanzagi alimshawishi akakubali.
Hatimaye, siku moja ya mwezi Aprili mwaka 1934, Kambarage akiwa na umri wa miaka 12 aliamka mapema kwa furaha kwenda kuanza darasa la kwanza katika shule ya Mwisenge, Musoma mjini. Kambarage aliingia shule akiwa hajui Kiswahili sawasawa. Hata hivyo, haikupita muda akajua Kiswahili, akili alizooonesha kwenye bao zilidhihirika darasani pia.  Ingawa wakati alipoanza shule alikuwa amechelewa kwa miezi mitatu, aliweza kuelewa mambo kwa kasi kuwashinda wengine walioanza mapema. Alipoingia darasa la tatu walimu waliamua kumrusha hadi la nne, akasoma masomo ya miaka minne kwa miaka mitatu tu. Mwaka 1936 alifanya mtihani wa nchi nzima wa kuingia darasa la tano, akawa mtu wa kwanza Tanganyika nzima.  Alichaguliwa kuingia shule ya bweni Tabora ambayo ilikuwa na darasa la tano hadi la kumi.
KIJANA KAMBARAGE
Mwaka 1937 Kambarage akiwa kijana wa miaka 15 alianza masomo ya darasa la tano akiwa na ari ya kusoma kwa bidii.  Waalimu wake Tabora walimpenda kwa akili zake. Wanafunzi wenziwe nao walimpenda sana kwa sababu alikuwa mcheshi na mwema sana.  Waliosoma naye waliwahi kueleza kwamba ingawa alikuwa akienda shule na fedha kidogo sana za matumizi, alikuwa radhi kutoa fedha zote alizokuwanazo kuwasaidia wanafunzi waliokuwa na shida.  Pamoja na wema, alioonesha tabia ya kupenda kutetea HAKI. Hakukubali kuona uonevu uliokuwa ukifanywa na ma-kaka dhidi ya wanafunzi. Aliwahi kwenda kwa Mwalimu Mkuu kulalamika kuhusu adhabu ya kufungwa miguu na mikono aliyopewa mwanafunzi mmoja na kaka wa bweni.
Kwenye kuamua shauri hilo Mwalimu Mkuu alimpendelea kaka na alimpa mwanafunzi huyo adhabu nyingine ya viboko. Kambarage aliamuriwa kumchapa, ilibidi amchape ingawa hakupenda kabisa kufanya hivyo! Hata hivyo, Kambarage hakuuacha msimamo wake wa kuwatetea waliokuwa wakionewa.  Hatimaye, Waalimu waliamua kumpa naye cheo cha ‘Kaka’ lakini hiyo haikuwa dawa. Haikupita muda, alianzisha mgomo wa kupinga mtindo wa ma-kaka kupata upendeleo wa kujigawia chakula kingi kuliko wanafunzi wengine ingawa naye alikuwa kaka!
Pamoja na kutetea haki za wanafunzi wenziwe, alidhihirisha uhodari wa kutetea kile alichoamini. Siku moja wakati wa kipindi cha majadiliano, mada ya “Tanganyika iendelee kuwa chini ya utawala wa Waingereza” ilikuwa ikijadiliwa.  Katika kuchangia, bila woga wowote mbele ya Mwalimu Mkuu (Mwingereza) Kambarage alipinga kwa nguvu hoja ile na kuelezea waziwazi uovu mwingi uliokuwa ukifanywa na Serikali ya Uingereza katika kuitawala nchi kwa mabavu na kwa misingi ya ubaguzi wa rangi.  Mwalimu Mkuu alimkatisha na kumwamuru akae chini asiendelee kuzungumza.  Kambarage alihamaki na kuamua kutoka kwenda bwenini kubeba sanduku lake ili akapande gari moshi (treni) kurudi kwao Butiama!  Ilibidi Mwalimu Mkuu atume watu kumshawishi arudi shuleni.
JULIUS KAMBARAGE
Akiwa shuleni Tabora Kambarage aliweza kubatizwa na kuwa Mkatoliki akajipa jina la ‘JULIUS’. Mwalimu aliwahi kusimulia kwamba ingawa alianza kuingia kwenye mafundisho ya dini akiwa shuleni Mwisenge, hakuweza kubatizwa kwa sababu mapadri walidhani kwamba angeweza kumrithi baba yake uchifu na hatimaye kuwa na wake wengi! Wamisionari walijaribu sana kumhubiria Chifu Nyerere Burito ajiunge na ukristo bila mafanikio. Mara nyingi mapadri walipomfuata kumhubiria aliishia yeye kuwahubiria wao! Kambarage aliweza kubatizwa baada ya baba yake kufariki mwaka 1942. Wasiwasi wa mapadri ulikuwa umeisha kwa sababu aliyerithi u-chifu alikuwa Edward Wanzagi.
Baada ya masomo shuleni Tabora, Julius Kambarage alifanikiwa kwenda Chuo Kikuu cha Makerere. Akiwa  huko kidogo kidogo alianza kujihusisha na mambo ya kisiasa. Alianzisha tawi la chama cha TAA kilichokuwa kimeanzishwa Dar es Salaam kama chama cha kutetea maslahi ya Watumishi wa Serikali waliokuwa wakinyanyaswa na kudhulumiwa na Wakoloni.
MWALIMU JULIUS KAMBARAGE
Mwaka 1945 Julius Kambarage Nyerere alifaulu masomo yake na kupata Diploma ya ualimu.  Akarudi kijijini Butiama na kumjengea mama yake nyumba kabla ya kwenda kuanza kazi Tabora. Uamuzi wake wa kutaka kuajiriwa kwenye shule ya misheni ya Mtakatifu Maria Tabora ni kielelezo kimoja cha msimamo wake kuhusu HAKI. Alikuwa amepokea barua mbili za ajira – moja kutoka Serikalini ikimpa nafasi ya kufundisha kwenye shule ya Sekondari ya Tabora na nyingine kutoka kwenye shule ya misheni ya Mtakatifu Maria (St. Marys).  Barua kutoka Serikalini ilimweleza juu ya mshahara atakaopata na marupurupu ya malipo ya pensheni na kwamba shule za misheni hazikuwa na marupurupu yoyote. Julius hakupendezwa na utaratibu wa marupurupu ya walimu wa serikali na misheni kutofautiana. Akaamua kwenda kufundisha shule ya Sekondari ya misheni isiyo na marupurupu yoyote.
Tabia yake ya kupenda haki iliendelea kujidihirisha katika shughuli mbalimbali alizofanya akiwa Tabora. Aliendelea kujihusisha na chama cha TAA akawa katibu wa tawi la chama hicho mjini Tabora. Alishiriki kwenye midahalo ya shule za Sekondari na hoja alizotoa zilivutia sana. Katika mdahalo mmoja uliokuwa na mada “Mali ni bora kuliko Elimu” Julius alipinga vikali hoja. Akasema kwamba alichagua kazi ya ualimu ili iwawezeshe watu kuelewa mambo na kwamba wakielewa wanakuwa na furaha, si kwa sababu wana mali. Unaweza kuwa mtu mwenye mali lakini huna furaha!
Mwalimu Julius alikuwa na hamu sana ya kwenda ng’ambo kwa masomo ya juu lakini kutokana na msimamo aliokuwanao dhidi ya Serikali, wakoloni hawakutaka kumpa nafasi hiyo. Hatimaye kwa kutetewa na rafiki yake aliyekuwa padri wa kizungu (Father Walsh) aliweza kupewa scholarship na Serikali kwenda Chuo Kikuu cha Edinburgh kuchukua masomo ya historia na uchumi. Akalipenda sana somo la filosofia. Mawazo ya kuingia kwenye siasa yalianza kujengeka wakati huo.
Akiendelea na msimamo wake wa utetezi wa haki aliweza kuandika makala mbali mbali. Mbili alizopeleka kwenye mashindano alipata zawadi ya kwanza. Makala moja ilihusu ‘kuonewa wanawake’ akielezea kuhusu unyonge wa wanawake katika maisha ya makabila nchini. Ya pili ilikuwa na kichwa cha habari “Matatizo ya Ubaguzi wa Rangi katika Afrika Mashariki”. Katika makala hiyo alisema Wazungu alikuwa anatawala kudumisha umaarufu wao kwa njia ya unafiki…. Bepari Mhindi alikuwa anapata chakula chake kwa wizi mtupu au ujanja-ujanja na unafiki… Mwafrika naye alikuwa mnafiki alijipendekeza kwa Mzungu wakati moyoni anapasuka kwa wivu na chuki!
Alimaliza vema masomo yake huko Edinburgh na kuwa Mwafrika wa kwanza nchini Tanzania kupata Stashahada ya Juu. Aliporudi nyumbani alipokelewa na mchumba wake Maria Magige aliyemchagua mwenyewe si yule aliyetolewa mahari na baba yake. Ikambidi afanye tena zoezi la kujenga nyumba kwa ajili yake na Maria watakapofunga ndoa. Wanakijiji walimshangaa walipomuona msomi kama yeye akichanganya simenti na mchanga kufyatua matofali kwa ajili ya kujengea. Wasomi hawakupaswa kufanya kazi kama hizo! Julius na Maria walifunga ndoa tarehe 24 Januari 1953 kwenye kanisa Katoliki Musoma. Katika maisha yao ya ndoa waliweza kuwapatia watoto 7, watatu wa kike na wanne wa kiume.
AWA KIONGOZI
Baada ya mapumziko yake Butiama Mwalimu Nyerere alienda kuanza kazi ya kufundisha katika shule aliyopangiwa ya Pugu Sekondari, Dar es Salaam. Mwaka huo wa 1953 akiwa Pugu alianza kujihusisha kikamilifu na shughuli za chama cha TAA. Aliitembea kwa miguu na wakati mwingine kwa baiskeli ya kua zima umbali wa maili 12 kwenda mjini Dar es Salaam kuhudhuria mikutano na shughuli za chama hicho. Haikupita muda akili na uwezo mkubwa aliokuwanao ulidhihirika akachaguliwa kukiongoza. Kutokana na uongozi wake mahiri chama cha TAA kikabadilishwa kuwa chama kamili cha siasa tarehe 7 Julai 1954, kikaitwa TANU.
Chini ya uongozi wake baada ya kuanzishwa kwa chama cha TANU zilianza rasmi harakati za kupigania Uhuru. Pamoja na juhudi zote za Wakoloni kuchelewesha kupatikana kwa Uhuru hatimaye mwaka 1960 nchi ya Tanganyika ilifanikiwa kupata Serikali ya Madaraka. Desemba 9 1961 ikapata Uhuru kamili ,Mwalimu akawa Waziri Mkuu. 1962 nchi ya Tanganyika ikawa Jamhuri akawa Rais wa Kwanza wa Tanganyika Huru.
Simulizi kuhusu uongozi uliotukuka miaka 24 wa Mwalimu Nyerere akiwa Rais wa Tanzania unahitaji makala nyingine nyingi. Hakuna maelezo mafupi yanayoweza kutosheleza historia ya uongozi wake. Itoshe kusema alikuwa kiongozi shupavu sana aliyepigania uhuru wa nchi yake na wa nchi zingine za Afrika. Alijishusha na kuwa pamoja na wananchi aliowaongoza – shida zao aliziona ni zake, zilimgusa na kumnyima usingizi!  Akaondoa ubaguzi na kufuta matabaka ya walionacho na wasionacho. Akafuta ukabila na udini nchini. Watanzania wakaishi kidugu. Akafanikiwa kujenga AMANI, UMOJA NA MSHIKAMANO akiongozwa na dira ya MAENDELEO  YANAYOLENGA WATU WOTE. Akafanya Tanzania ijulikane kuwa kisiwa cha AMANI duniani.
HITIMISHO
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipendwa na kuheshimika sana ndani na nje ya nchi. Mwaka 1985 aliamua kwa hiari yake mwenyewe kuacha uongozi wa Taifa ili apumzike.  Alizunguka nchi nzima kuwaaga Watanzania. Kwa mapenzi makubwa wakampa zawadi za kila aina. Wananchi walioonesha wazi huzuni waliyokuwanayo kwa uamuzi aliouchukua. Walimuaga wakilia machozi!
Yote aliyoyaanza tangu utoto wake yalifikia kikomo tarehe 14 Oktoba 1999 alipoaga dunia kwenye kitanda cha hospitali ya Mtakatifu Thomas mjini London alikokwenda kwa matibabu. Kabla hajafariki dunia aliwakumbuka Watanzania wake akasema: “Najua nitakufa sitapona ugonjwa huu. Ninasikitika kuwaacha Watanzania wangu, najua watalia sana. Lakini nami nitawaombea kwa Mungu.”  Naam, Watanzania wake walilia sana walipopata taarifa za kifo chake. Mwili wake ulipoletwa nchini waliomboleza kwa uchungu mno. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alizikwa kijijini kwake Mwitongo Butiama kwa heshima zote na wananchi wa Tanzania, na wa mataifa mbalimbali wakiwemo viongozi mashuhuri waliokuja kwa ajili hiyo.
Ni dhahiri msingi wa yale yote aliyoyaamini na kuyasimamia utaendelea kudumu ndani ya mioyo ya kizazi chake, kizazi hiki na vizazi vijavyo kutokana na mchango mkubwa alioutoa akiwa Muasisi na Baba wa Taifa katika kujenga taifa la Tanzania. Huyo ndiye mtoto aliyezaliwa siku ya mvua na kupewa jina la mzimu wa mvua KAMBARAGE; mwana wa Chifu Nyerere Burito na Mgaya wa Nyang’ombe.  Ni dhahiri, tarehe  aliyozaliwa – 13 Aprili mwaka 1922, Mgaya hakujua kwamba alikuwa amejifungua mtoto ambaye angekuja kuwa kiongozi maarufu sana nchini na duniani, aliyewapenda binadamu wote na kuwatumikia Watanzania kwa moyo wake wote, akili na nguvu zake zote! MUNGU Ailaze Roho yake Mahali Pema Peponi. Amin.

Print this item

  MIIKO YA WASWAHILI/WAAFRIKA NA TAMADUNI ZA ULIMWENGU
Posted by: MwlMaeda - 06-14-2021, 07:11 PM - Forum: Historia ya makabila ya kibantu - No Replies

MIIKO  YA WASWAHILI/WAAFRIKA NA TAMADUNI ZA ULIMWENGU
Pamoja na mambo mengine mengi, mgeni au wageni hupenda kujifunza tamaduni za wenyeji. Hata kama watazidharau lakini lazima kwanza wazijue. Mimi na wewe tunaweza kuwa wageni ndani au nje ya nchi. Moja ya mambo ambayo tungejifunza ugenini ni utamaduni wa wenyeji wetu.
Au mimi na wewe tunaweza kuwa wenyeji, moja ya mambo ambayo wageni wetu wangependa kujifunza kwetu ni utamaduni wetu. Kwa ainisho la ujumla, utamaduni ni dhana inayokusanya mila, miiko, adabu, desturi, lugha, vyakula na kadhalika.
Kila jamii ina utamaduni wake. Waafrika na hasa Watanzania tuna miiko yetu ya kiutamaduni ambayo tungependa wageni waiheshimu. Baada ya kipindi cha kutawaliwa kikoloni, sasa tuna uhuru wa kulinda utamaduni wetu.
Yawezekana, kwa kiasi fulani, uhuru huu wa kulinda utamaduni wetu unatatizwa na umasikini wetu unaotulazimu kuomba misaada kwa wahisani lakini bado uungwana wetu hauuawi na umasikini.
Yawezekana Mtumwa akakosa hiyari kwa sababu ya maisha ya utumwani. Lakini masikini ana nafasi ya hiyari licha ya umasikini wake. Jamii yetu ina mila zake, na Taifa letu ni masikini, bado mila zetu haziwezi kuuawa kwa sababu ya umasikini wetu.
Tena eneo la utamaduni nalo pia sasa linaweza kuwa moja ya vivutio vya utalii. Watalii wanataka kuja kuona na kujifunza utamaduni wetu halisi. Wanawapenda Wamasai kwa sababu ya kubaki katika utamaduni wao halisi. Hatusemi kuwa kila cha utamaduni wetu kifuatwe au kisiachwe hata kama ni kibaya.
La hasha! Kile ambacho hakifai lazima kiachwe. Kama utamaduni unazuia watoto kusoma na wabaki kuchunga ng’ombe, hiyo hapana! Utamaduni huo uachwe mara moja. Si utamaduni bali ni ujinga huo.
Kama utamaduni unakeketa viungo vya uzazi, haufai kabisa! Uachwe mara moja au utungiwe sheria ya kuukomesha! Tungependa wageni wetu wajifunze mazuri ya utamaduni wetu, na tusingependa wajifunze mabaya ya utamaduni wetu.
Mazuri yako mengi mno, kuanzia Lugha yetu ya Kiswahili, mavazi yetu, vyakula vyetu, ushujaa wetu, maungwana yetu, ukarimu wetu, heshima yetu kwa wazazi, heshima yetu kwa wakwe zetu, adabu za mke kwa mume, na mume kwa mke na kadhalika.
Haya ni mambo mazuri kabisa. Tusijidharau katika haya hata kidogo, na tuwe ngangari katika kuyaenzi yote hayo. Lugha yetu ya Kiswahili ina nafasi kubwa katika utamaduni wa Lugha ulimwenguni.
Utamaduni wetu wa lugha una nafasi ya kupata heshima kubwa na kututambulisha popote pale. Kuitwa Mswahili kwaweza kuwa fahari ya kilimwengu. Lakini hii itategemea msimamo wetu katika kuuenzi utamaduni huu.
Nitaje maeneo kadhaa ambayo labda bado yanaonesha udhaifu wetu wa kutojiamini pale linapokuja suala la lugha yetu. Mosi, tunapotembelewa na wageni ambao wao wenyewe hawatumii Lugha ya Kiingereza, ingelikuwa fursa nzuri na sisi kutumia Lugha yetu.
Kama mgeni wa Kichina au Kijerumani anakuja nchini na kutumia lugha yake, kwa nini wenyeji wake tutumie lugha nyingine ya kigeni kuwasiliana naye?
Mjerumani au Mchina anapokwenda Uingereza au Marekani, anatumia Kijerumani au Kichina chake huku mwenyeji wake akitumia Kiingereza chake. Inakuwaje Mjerumani na Mchina huyo huyo anapokuja Tanzania, mwenyeji wake anatumia Lugha ya Waingereza kuwasiliana naye.
Ni lini Afrika itajikomboa na utumwa wa Kilugha? Mjerumani ambaye alitutawala anajua sana Watanzania tunayo lugha yetu ya Kiswahili, na kwa kuheshimu nafasi ya Kiswahili ulimwenguni, Ujerumani ina Shirika kubwa la Habari linaloendesha matangazo yake kwa Lugha ya Kiswahili.
Isitoshe, kuna Wajerumani kadhaa wanaozungumza au kujifunza Kiswahili. Ni dhahiri mgeni wa kidiplomasia wa Ujerumani angetarajia kukutana na Kiswahili katika mawasiliano na mwenyeji wake.
Yawezekana kuna tatizo la ukalimani lakini kwa nini? Miaka mingi ya uhuru ingeliweza kabisa kutupatia wakalimani wa angalau lugha zote kubwa za Ulimwengu kikiwemo Kijerumani.
Kwa kuwa Mjerumani hakuja kwenye Kiingereza basi na sisi tusingekuja katika lugha hiyo. Tungebaki na yetu, na bila shaka na yeye angetuelewa. Hata kama tunabanwa na ukweli kuwa sisi ndio wahitaji, na wenzetu ndio wahisani, lakini kwa kuwa muhisani huyu ana lugha yake, lugha yetu nayo ingekuwa na nafasi.
Kama angelikuwa Obama au Cameron, hapo tungebaki na Lugha yao ambayo kwetu pia ni lugha rasmi ya mawasiliano. Hatuna tatizo na Kiingereza, na wala viongozi wetu hawafanyi kosa lolote kukitumia, lazima tukubali nayo pia ni lugha yetu kuu ya kufundishia sekondari na vyuoni, hatuna namna ya kukwepa.
Lakini katika kujaribu kukipandisha hadhi ya Kimataifa Kiswahili, ipo mianya ambayo tunaweza kuitumia kupenyeza Kiswahili iwe katika dhifa za kidiplomasia au penginepo. Hasa pale tunapofikiwa na wageni wasiotumia Kiingereza.
Siku alipokuja Rais wa Ujerumani, waandishi wetu wengi wenye udhaifu mkubwa wa Lugha ya Kiingereza wangeweza kutumia Kiswahili chao kuuliza maswali, na kisha Mkalimani wa Kijerumani kutafsiri.
Lakini ule utambulisho tu wa Ikulu ulitosha kuwanyamazisha wale wasioujua Kiingereza. Kwamba ni umombo uliohitajika! Wasiokimanya Kiingereza wakabaki na maswali yao huku wakiwakilishwa na watu ambao maswali yao hayakulenga maeneo ambayo wengi wangeyatarajia.
Tunajifunza kutokana na makosa, na kwa hili si kwamba tunalaumiana lakini tuyasome upya mazingira ya kidiplomasia na kuona wapi tunaweza kubaki Waswahili kilugha, na wapi tunalazimika kutumia Kiingereza.
Pili, tuna miiko yetu ya Kimaadili katika eneo hilohilo la utamaduni. Mswahili ana miiko ambayo, pengine, Mzungu hana. Na Mataifa yamekubaliana kuheshimiana kwa tamaduni zao.
Hivyo, mgongano wa utamaduni angalau unaweza kupunguzwa kama si kuepukwa. Viongozi wa Kimataifa huwa na kawaida ya kupiga picha za pamoja. Lakini upigaji picha nao wakati mwingine huzingatia utamaduni.
Kwa utamaduni wetu wa Waswahili, kupiga picha na mke au mume wa mtu ni mtihani kidogo! Japo inatokea hata Kitaifa lakini pale ambapo mume wa mtu yupo, na mke wa mtu yupo, ni vema picha ikazingatia hisia za unyumba wao.
Tusifiche, na sidhani kama nitamuudhi yoyote kwamba, Mama yetu alibabaika kidogo Siku tulipotembelewa na mgeni wa Ujerumani. Alikuwa nyuma ya baba, na mwenziwe naye alikuwa nyuma ya baba mgeni.
Mwenzio hakuwa na tatizo kwa sababu kwao wao mume kupiga picha na mke wa mwenziwe si tatizo. Tatizo likawa kwetu. Ulikuwa ni mgongano wa hadharani wa kiutamaduni. Baba alipogeuka nyuma akaona, mama wa Kizungu kishasogea.
Baba hakuwa na namna ila kumwita mama wa Kizungu. Mamaetu akapata majibu ya haraka aende wapi. Picha ikapigwa kwa utamaduni wa Kizungu, si utamaduni wetu wa Kiswahili. Bila shaka hii nayo ni changamoto.
Inaweza kutafutiwa njia mbili; ya kwanza Ikulu yetu ianze kutangaza utamaduni wetu wa kupiga picha kwa kuzingatia hisia za unyumba. Kila mtu asimame na mkewe. Au pili, waume wapige yao, na wake wapige yao. Sijui nje huko tutafanyaje lakini hapa ndani tujitahidi kuzingatia utamaduni wetu.

Print this item