08-08-2022, 08:08 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BILADI ''
Neno *biladi* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya *mji* .
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *biladi* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu *'bilaad* *(soma: bilaadun/bilaadan/bilaadin بلاد)** likiwa ni wingi wa neno la Kiarabu *baldah (soma: baldatun/baldatan/baldatin بلدة)* lenye maana zifuatazo:
1. Eneo kubwa la ardhi.
2. Eneo maalumu la ardhi wanalokaa watu fulani lenye miji, vijiji na mipaka inayotambulika; *nchi*.
*Yaa baladii, yaa bilaadii يا بلادي، يا بلدي* Ee nchi yangu!
3. Sehemu ya nchi au mji.
4. Mji mdogo.
5. Chanzo.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *'bilaadun بلاد* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *biladi* lilichukua kutoka lugha ya Kiarabu maana ya *mji* na kuziacha maana nyingine.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *biladi* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya *mji* .
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *biladi* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu *'bilaad* *(soma: bilaadun/bilaadan/bilaadin بلاد)** likiwa ni wingi wa neno la Kiarabu *baldah (soma: baldatun/baldatan/baldatin بلدة)* lenye maana zifuatazo:
1. Eneo kubwa la ardhi.
2. Eneo maalumu la ardhi wanalokaa watu fulani lenye miji, vijiji na mipaka inayotambulika; *nchi*.
*Yaa baladii, yaa bilaadii يا بلادي، يا بلدي* Ee nchi yangu!
3. Sehemu ya nchi au mji.
4. Mji mdogo.
5. Chanzo.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *'bilaadun بلاد* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *biladi* lilichukua kutoka lugha ya Kiarabu maana ya *mji* na kuziacha maana nyingine.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda