MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'BAFTA'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO 'BAFTA'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BAFTA'

Neno *bafta* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana ya kitambaa cheupe kinachotengenezwa kwa nyuzi za pamba.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *bafta* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'baftah*( *soma: baftatun/baftatan/baftatin بفتة )* ambalo ni nomino ya Kiarabu yenye maana kitambaa cha hali ya juu kilichotengenezwa kutokana na nyuzi za pamba.

Vitambaa vya *bafta* ni mashuhuri sana nchini India na hutumika kushona suruali na mashati.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *'baftatun بفتة* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *bafta* halikubadili maana yake katika lugha ya Kiarabu.

*TANBIHI:*
Nomino *bafta* ni neno *lililoarabishwa* kutoka lugha ya Kifaransa likiwa na maana ya nguo iliyoshonwa, nyuzi zilizosokotwa, busati, aina ya nguo iliyotengenezwa kutokana na pamba, kitambaa kinachotokana na sufi.

Nchini Misri *bafta* ni kitambaa cha hali ya juu kilichotengenezwa kutokana na pamba nyeupe.

Nchini Syria *bafta* ni kitambaa kilichotokana na hariri.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)