05-06-2022, 06:04 AM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AMANA'
Neno *amana* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana zifuatazo:
1. Kitu anachokabidhiwa mtu kwa utaratibu maalumu ili akihifadhi kwa muda na kukirejesha kwa mmiliki kitakapohitajika.
2. Kiasi cha fedha kilichowekwa benki; *akiba* .
3. Kitu chenye thamani kubwa.
Katika lugha ya Kiarabu neno *amana* linatokana na neno la Kiarabu *amaanah (soma: amaanatun/amaanatan/amaanatin امانة)* lenye maana zifuatazo:
1. Kusalimika, nomino inayotokana na kitenzi cha Kiarabu *amina امن* amesalimika.
2. Akiba.
3. Hali ya kuhifadhi upendo na kutekeleza ahadi kwa namna inavyopasa.
4. Alichokifaradhisha (alichokifanya lazima/wajibu) Mwenyeezi Mungu kwa watu.
5. Msimamo thabiti na ukweli.
6. Chombo cha uendeshaji na usimamizi wa shughuli za taasisi, chama, jumuiya *al-amaanatul aamah الأمانة العامة* ofisi ya Katibu Mkuu; *Sekretarieti*.
7. Mamlaka ya usimamizi wa mji mkuu, *amaanatul aaswimah عاصمة العاصمة.*
Kinachodhihiri ni kuwa neno *amaanatun امانة* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *amana* lilichukua baadhi ya maana za neno hili katika lugha asili - Kiarabu na kuyaacha mengine.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *amana* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana zifuatazo:
1. Kitu anachokabidhiwa mtu kwa utaratibu maalumu ili akihifadhi kwa muda na kukirejesha kwa mmiliki kitakapohitajika.
2. Kiasi cha fedha kilichowekwa benki; *akiba* .
3. Kitu chenye thamani kubwa.
Katika lugha ya Kiarabu neno *amana* linatokana na neno la Kiarabu *amaanah (soma: amaanatun/amaanatan/amaanatin امانة)* lenye maana zifuatazo:
1. Kusalimika, nomino inayotokana na kitenzi cha Kiarabu *amina امن* amesalimika.
2. Akiba.
3. Hali ya kuhifadhi upendo na kutekeleza ahadi kwa namna inavyopasa.
4. Alichokifaradhisha (alichokifanya lazima/wajibu) Mwenyeezi Mungu kwa watu.
5. Msimamo thabiti na ukweli.
6. Chombo cha uendeshaji na usimamizi wa shughuli za taasisi, chama, jumuiya *al-amaanatul aamah الأمانة العامة* ofisi ya Katibu Mkuu; *Sekretarieti*.
7. Mamlaka ya usimamizi wa mji mkuu, *amaanatul aaswimah عاصمة العاصمة.*
Kinachodhihiri ni kuwa neno *amaanatun امانة* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *amana* lilichukua baadhi ya maana za neno hili katika lugha asili - Kiarabu na kuyaacha mengine.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda