01-25-2022, 01:50 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'SADFA'
Neno sadfa katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: i-/zi-] yenye maana ya hali ambapo mambo au matukio mawili au zaidi hutokea kwa wakati mmoja bila ya kupangwa au kutarajiwa .
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili sadfa( soma: swidfatun/swidfatan/swidfatin صدفة ) ni nomino ya Kiarabu yenye maana ya kukutana bila ya kukubaliana au kuwa na miadi.
Kinachodhihiri ni kuwa neno hili swidfatun/swidfatan/swidfatin صدفة lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno la Kiswahili ' sadfa ' halikubadili maana ya lugha asili - Kiarabu ya kutokea jambo au tukio bila ya kupangwa.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Neno sadfa katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: i-/zi-] yenye maana ya hali ambapo mambo au matukio mawili au zaidi hutokea kwa wakati mmoja bila ya kupangwa au kutarajiwa .
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili sadfa( soma: swidfatun/swidfatan/swidfatin صدفة ) ni nomino ya Kiarabu yenye maana ya kukutana bila ya kukubaliana au kuwa na miadi.
Kinachodhihiri ni kuwa neno hili swidfatun/swidfatan/swidfatin صدفة lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno la Kiswahili ' sadfa ' halikubadili maana ya lugha asili - Kiarabu ya kutokea jambo au tukio bila ya kupangwa.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda