MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
UKWELI na KWELI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
UKWELI na KWELI
#1
UKWELI na KWELI

Kama alivyoeleza Sheikh Khamisi Mataka, kwa upande mmoja kuna tafauti baina ya maneno "ukweli" (kwamba ni nomino/ jina: Huu ni ukweli) na "kweli" (kwamba ni kielezi: Ni kweli leo ni Ijumaa?).  Lakini kwa upande mwengine, na kwa maeneo mengine kuzungumzwako Kiswahili, neno "kweli" ni kielezi na ni nomino/jina pia. Kwa mfano, tuna misemo kama vile, "Kweli ikidhihiri, uongo hujitenga"; "Msema kweli ni mpenzi wa Mngu"; na mengineyo.

Mfano mwengine twauona kwenye tafsiri ya Qur'ani, Aya ya 81 ya Sura Israa (Banuw Israiyl). Sheikh Abdullah Farsy katika Kurani Tukufu amelifasiri neno la Kiarabu alhaqq (الحق) kuwa ni "ukweli"; na Sheikh Ali Muhsin Barwaniy katika tafsiri yake ya Al-Muntakhab  amelifasiri "kweli."?

Naye mshairi Shaaban Robert katika mashairi yake amelitumia neno "kweli" kuwa ni nomino/jina.?
Nami pia nimelitumia hivyo.?

Kwa hivyo, kwa ufupi, mtu ana hiari ya kutumia "ukweli" au "kweli" kuwa ni nomino/jina, na atakuwa hakukipotoa Kiswahili.
-Abdilatif Abdalla,
London,
22.10.2021
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 2 Guest(s)