09-08-2022, 10:08 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI''
Neno *buriani* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:
1. Maagano yanayoonesha kuwa wanaoagana wataachana kwa muda mrefu au kutoonana kabisa.
2. Salamu za kutakiana heri ambayo watu hupeana wanapoagana.
3. Msamaha au radhi ambayo watu hutakiana huku wakiagana.
*Nahau:*
*Peana buriani:* agana.
Katika lugha ya Kiarabu, hakuna neno *buriani* na neno lililo karibu ni neno *barawah*, neno la msimu lililotumika katika baadhi ya nyimbo za Kiarabu likiwa na maana zifuatazo:
1. Neno la kushukuru; ahsante.
2. Hali ya kukamilika; timamu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *buriani* halina asili ya Kiarabu kinyume na madai yaliyosajiliwa makamusini.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *buriani* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:
1. Maagano yanayoonesha kuwa wanaoagana wataachana kwa muda mrefu au kutoonana kabisa.
2. Salamu za kutakiana heri ambayo watu hupeana wanapoagana.
3. Msamaha au radhi ambayo watu hutakiana huku wakiagana.
*Nahau:*
*Peana buriani:* agana.
Katika lugha ya Kiarabu, hakuna neno *buriani* na neno lililo karibu ni neno *barawah*, neno la msimu lililotumika katika baadhi ya nyimbo za Kiarabu likiwa na maana zifuatazo:
1. Neno la kushukuru; ahsante.
2. Hali ya kukamilika; timamu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *buriani* halina asili ya Kiarabu kinyume na madai yaliyosajiliwa makamusini.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda