MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI''

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI''
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI''

Neno *buriani* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo:

1. Maagano yanayoonesha kuwa wanaoagana wataachana kwa muda mrefu au kutoonana kabisa.

2. Salamu za kutakiana heri ambayo watu hupeana wanapoagana.

3. Msamaha au radhi ambayo watu hutakiana huku wakiagana.

*Nahau:*
*Peana buriani:* agana.

Katika lugha ya Kiarabu, hakuna neno *buriani* na neno lililo karibu ni neno *barawah*, neno la msimu lililotumika katika baadhi ya nyimbo za Kiarabu likiwa na maana zifuatazo:

1. Neno la kushukuru; ahsante.

2. Hali ya kukamilika; timamu.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *buriani* halina asili ya Kiarabu kinyume na madai yaliyosajiliwa makamusini.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*