ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI'' - Printable Version +- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz) +-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1) +--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16) +--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI'' (/showthread.php?tid=2825) |
ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI'' - MwlMaeda - 09-08-2022 HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "BURIANI'' Neno *buriani* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-*] yenye maana zifuatazo: 1. Maagano yanayoonesha kuwa wanaoagana wataachana kwa muda mrefu au kutoonana kabisa. 2. Salamu za kutakiana heri ambayo watu hupeana wanapoagana. 3. Msamaha au radhi ambayo watu hutakiana huku wakiagana. *Nahau:* *Peana buriani:* agana. Katika lugha ya Kiarabu, hakuna neno *buriani* na neno lililo karibu ni neno *barawah*, neno la msimu lililotumika katika baadhi ya nyimbo za Kiarabu likiwa na maana zifuatazo: 1. Neno la kushukuru; ahsante. 2. Hali ya kukamilika; timamu. Kinachodhihiri ni kuwa neno *buriani* halina asili ya Kiarabu kinyume na madai yaliyosajiliwa makamusini. *Shukran sana.* *Khamis S.M. Mataka.* |