03-13-2022, 01:27 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AKIBA'
Neno *akiba* katika lugha Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya kitu kilichohifadhiwa/kilichowekwa ili kitumike baadaye.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *akiba* linafanana kimatamshi na neno *aaqiibatun عاقبة* lakini limetoholewa kutoka neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة*.
Neno la Kiarabu *aaqibatun عاقبة* lina maana zifuatazo:
1. Mwisho wa jambo; *hatima* .
2. Malipo anayolipwa mtu mwishoni mwa jambo.
Na neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة* lina maana zifuatazo:
1. Chombo cha kuhifadhiwa vitu.
2. Kitu kinabebwa safarini ili kumfaa msafiri njiani au aendako.
3. Tumaini la mtu mwisho wa umri wake; mtoto, kizazi.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiswahili *akiba* ingawa linafanana kimatamshi na neno la Kiarabu *aaqibatun عاقبة* lenye maana ya mwisho wa jambo; hatima na malipo anayolipwa mtu mwishoni mwa jambo, limeazimwa na kutoholewa kutoka neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة* (mkoba) lenye maana ya: chombo cha kuhifadhiwa vitu; mkoba, kitu kinabebwa safarini ili kumfaa msafiri njiani au aendako na tumaini la mtu mwisho wa umri wake; mtoto, kizazi.
Kupewa neno *akiba* maana iliyopewa katika Kiswahili bila shaka ni kuzingatiwa kutaja mkoba kwa kukusudia kilichobebwa mkobani, yaani *dhikrul haamili Li-iraadatil Mahmuul Fiihi ذكر الحامل* لإرادة المحمول فيه yaani, badala ya kutajwa kilichobebwa mkobani ili kumfaa mbebaji ukatajwa mkoba wenyewe *akiba (haqiibatun حقيبة*).
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *akiba* katika lugha Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya kitu kilichohifadhiwa/kilichowekwa ili kitumike baadaye.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *akiba* linafanana kimatamshi na neno *aaqiibatun عاقبة* lakini limetoholewa kutoka neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة*.
Neno la Kiarabu *aaqibatun عاقبة* lina maana zifuatazo:
1. Mwisho wa jambo; *hatima* .
2. Malipo anayolipwa mtu mwishoni mwa jambo.
Na neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة* lina maana zifuatazo:
1. Chombo cha kuhifadhiwa vitu.
2. Kitu kinabebwa safarini ili kumfaa msafiri njiani au aendako.
3. Tumaini la mtu mwisho wa umri wake; mtoto, kizazi.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiswahili *akiba* ingawa linafanana kimatamshi na neno la Kiarabu *aaqibatun عاقبة* lenye maana ya mwisho wa jambo; hatima na malipo anayolipwa mtu mwishoni mwa jambo, limeazimwa na kutoholewa kutoka neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة* (mkoba) lenye maana ya: chombo cha kuhifadhiwa vitu; mkoba, kitu kinabebwa safarini ili kumfaa msafiri njiani au aendako na tumaini la mtu mwisho wa umri wake; mtoto, kizazi.
Kupewa neno *akiba* maana iliyopewa katika Kiswahili bila shaka ni kuzingatiwa kutaja mkoba kwa kukusudia kilichobebwa mkobani, yaani *dhikrul haamili Li-iraadatil Mahmuul Fiihi ذكر الحامل* لإرادة المحمول فيه yaani, badala ya kutajwa kilichobebwa mkobani ili kumfaa mbebaji ukatajwa mkoba wenyewe *akiba (haqiibatun حقيبة*).
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda