MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'AKIBA' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA NENO 'AKIBA' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO 'AKIBA' (/showthread.php?tid=2454)



ETIMOLOJIA YA NENO 'AKIBA' - MwlMaeda - 03-13-2022

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AKIBA'

Neno *akiba* katika lugha Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya kitu kilichohifadhiwa/kilichowekwa ili kitumike baadaye. 

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *akiba* linafanana kimatamshi na neno *aaqiibatun عاقبة*  lakini limetoholewa kutoka neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة*.

Neno la Kiarabu *aaqibatun عاقبة*  lina maana zifuatazo:

1. Mwisho wa jambo; *hatima* .

2. Malipo anayolipwa mtu mwishoni mwa jambo.

Na neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة*  lina maana zifuatazo:

1. Chombo cha kuhifadhiwa vitu.

2. Kitu kinabebwa safarini ili kumfaa msafiri njiani au aendako.

3. Tumaini la mtu mwisho wa umri wake; mtoto, kizazi. 

Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiswahili *akiba* ingawa linafanana kimatamshi  na neno la Kiarabu *aaqibatun عاقبة* lenye maana ya mwisho wa jambo; hatima na malipo anayolipwa mtu mwishoni mwa jambo, limeazimwa na kutoholewa kutoka neno la Kiarabu *haqiibatun حقيبة* (mkoba) lenye maana ya: chombo cha kuhifadhiwa vitu; mkoba, kitu kinabebwa safarini ili kumfaa msafiri njiani au aendako na tumaini la mtu mwisho wa umri wake; mtoto, kizazi. 

Kupewa neno *akiba* maana iliyopewa katika Kiswahili bila shaka ni kuzingatiwa kutaja mkoba kwa kukusudia kilichobebwa mkobani, yaani *dhikrul  haamili Li-iraadatil Mahmuul Fiihi ذكر الحامل* لإرادة المحمول فيه yaani, badala ya kutajwa kilichobebwa mkobani ili kumfaa mbebaji ukatajwa mkoba wenyewe *akiba (haqiibatun حقيبة*).

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*