03-05-2022, 09:57 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO 'FIRASHA' NA 'FIRASHI'
Neno *firasha* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya aina ya godoro jembamba linalotengenezwa kwa vipande vya vitambaa.
Neno *firashi* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya mbao ndogondogo zinazotumika kuunda mashua au jahazi.
Katika lugha ya Kiarabu, maneno *firasha* na *firashi* yanatokana na nomino ya Kiarabu *firaashun/firaashan/firaaashin فراش* yenye maana zifuatazo:
1. Kinachotandikwa ili kulala juu yake; godoro.
2. Kiota cha ndege.
3. Sehemu ya chini ya ulimi.
4. Makazi ya mtu; nyumba.
Mbali ya maana hizi nne, neno hili la Kiarabu lina maana tofauti zipatazo kumi na moja.
Kinachodhihiri ni kuwa maneno *firasha* na *firashi* ambayo katika Kiswahili ni maneno mawili yenye maana tofauti, katika lugha ya Kiarabu ni neno moja tu lenye maana anuai.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *firasha* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya aina ya godoro jembamba linalotengenezwa kwa vipande vya vitambaa.
Neno *firashi* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya mbao ndogondogo zinazotumika kuunda mashua au jahazi.
Katika lugha ya Kiarabu, maneno *firasha* na *firashi* yanatokana na nomino ya Kiarabu *firaashun/firaashan/firaaashin فراش* yenye maana zifuatazo:
1. Kinachotandikwa ili kulala juu yake; godoro.
2. Kiota cha ndege.
3. Sehemu ya chini ya ulimi.
4. Makazi ya mtu; nyumba.
Mbali ya maana hizi nne, neno hili la Kiarabu lina maana tofauti zipatazo kumi na moja.
Kinachodhihiri ni kuwa maneno *firasha* na *firashi* ambayo katika Kiswahili ni maneno mawili yenye maana tofauti, katika lugha ya Kiarabu ni neno moja tu lenye maana anuai.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda