MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABTADI' NA 'ABTALI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABTADI' NA 'ABTALI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABTADI' NA 'ABTALI'

Neno *abtadi* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino: [Ngeli: a-/wa-]* shujaa wa vita.

2. *Kitenzi elekezi* fanya jambo kwa mara ya kwanza ili wengine wafuate; tangulia, anza.

3. *Kitenzi elekezi* alika kitu au shughuli *_Ninaabtadi safari yangu kwa kumuomba Mola; Bismillaahi n'abtadi*_ ninaanza kwa jina la Mwenyeezi Mungu.

Katika lugha ya Kiarabu, neno *abtadi* ni kitenzi cha Kiarabu  *abtadiu ابتدئ* chenye maana ya 'ninaanza'.

Neno *abtali* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino: [Ngeli: a-/wa-, wingi: maabtali]* yenye maana ya askari au mpiganaji ambaye ni shujaa na mzoefu wa kupigana.

2. *Nomino: [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana ya *wapiganaji.*

Katika lugha ya Kiarabu, neno *abtali* (soma: *abtwaalun/abtwaalan/abtwaalin ابطال* ) ni nomino iliyo wingi wa neno la Kiarabu *batwalun/batwalan/batwalin  بطل* lenye maana zifuatazo:

1. *Batwalun fil Maarik*  *بطل في المعارك* askari wa mstari wa mbele vitani; shujaa.

2. Mshindi wa kwanza katika mashindano ya michezo kama ndondi, riadha, mieleka na mingineyo.

3. Muhusika mkuu katika riwaya, tamthilia au filamu.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *abtadi* linalotokana na kitenzi cha Kiarabu *abtadiu ابتدئ)* *ninaanza*, lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa *abtadi* maana yake katika lugha ya asili - Kiarabu haikubadilika ingawa iliongezwa maana ya kufanya jambo kwa mara ya kwanza ili wengine wafuate.

Kuhusu neno abtali (soma: *abtwaalun/abtwaalan/abtwaalin ابطال*) lenye maana ya wapiganaji nalo halikuacha maana yake katika lugha ya asili - Kiarabu  ingawa lilipewa maana mpya ya askari au mpiganaji ambaye ni shujaa na mzoefu wa kupigana na kuziacha maana zingine katika lugha ya asili - Kiarabu.

Ni muhimu kuzingatia kuwa neno *abtadi* *ninaanza* limesajiliwa kamusini kwa maana ya *shujaa wa vita* na jambo hili yumkini ni kosa lililotokana na kukaribiana kwa maneno *abtadi* na *abtali* .

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)