01-23-2022, 02:05 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AIBU'
Neno aibu katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: i-/zi-] yenye maana zifuatazo:
1. Jambo la kumtia mtu fedheha, jambo la kumvunjia mtu heshima.
2. Hali ya mtu kuvaa mavazi yasiyomsitiri vyema.
Kuna nahau: jitia aibu, tia mtu aibu: Alivua nguo mbele ya watu bila kuona aibu.
Kuna methali: Aibu ya maiti aijuaye mwosha: mtu anayezifahamu siri za mtu fulani ni yule aliyenaye karibu.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili aibu( soma: aybun/ayban/aybin عيب ) ni nomino ya Kiarabu yenye maana zifuatazo:
1. Kasoro, upungufu wa sifa: bidhwaa-atun laa aiba fiihaa بضاعة لا عيب فيها bidhaa isiyo kasoro yoyote.
2. Fedheha. Kuna msemo: Alfaqru Laysa Bi Aybin الفقر ليس بعيب ufukara si aibu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno hili aybun/ayban/aybin lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno la Kiswahili ' aibu ' halikubadili maana yake katika lugha yake asili - Kiarabu.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Neno aibu katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: i-/zi-] yenye maana zifuatazo:
1. Jambo la kumtia mtu fedheha, jambo la kumvunjia mtu heshima.
2. Hali ya mtu kuvaa mavazi yasiyomsitiri vyema.
Kuna nahau: jitia aibu, tia mtu aibu: Alivua nguo mbele ya watu bila kuona aibu.
Kuna methali: Aibu ya maiti aijuaye mwosha: mtu anayezifahamu siri za mtu fulani ni yule aliyenaye karibu.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili aibu( soma: aybun/ayban/aybin عيب ) ni nomino ya Kiarabu yenye maana zifuatazo:
1. Kasoro, upungufu wa sifa: bidhwaa-atun laa aiba fiihaa بضاعة لا عيب فيها bidhaa isiyo kasoro yoyote.
2. Fedheha. Kuna msemo: Alfaqru Laysa Bi Aybin الفقر ليس بعيب ufukara si aibu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno hili aybun/ayban/aybin lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno la Kiswahili ' aibu ' halikubadili maana yake katika lugha yake asili - Kiarabu.
Shukran sana.
Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda