MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI : TUCHAGUE KWA MAKINI VIONGOZI TANZANIA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI : TUCHAGUE KWA MAKINI VIONGOZI TANZANIA
#1

  1. Hoja ninaieleza, uchaguzi Tanzania
    Ni yupi anyeweza, usukukani kuchukua?
    Pasi kutudidimiza, tupate kumchagua
    Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  2. Wengi wamejitokeza, nafasi kuziwania
    Sera wanatueleza, watakazozitumia
    Ahadi zinapendeza, wanazotutangazia
    Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  3. Wengi wamejitokeza, ikulu kugombania
    Mazuri wayatangaza, tupate kuwachagua
    Kama ukiwachunguza, ni vigumu kuamua
    Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  4. Ugumu ninaowaza, ni jinsi ya kuchagua
    Kila mtu atangaza, ndiye anayetufaa
    Kutuondolea giza, na kutuletea taa
    Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  5. Sera wanazoeleza, wakiwa kwenye jukwaa
    Kama wakitekeleza, tuendako kunang’aa
    Swali ninajiuliza, ni nani anotufaa
    Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  6. Nataka kupendekeza, jambo la kuzingatia
    Umakini natangaza, ndio wa kutegemea
    Lisijekutuumiza, maamuzi kujutia
    Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  7. Mola pekee anaweza, kutupatia “Kifaa”
    Maombi tukiongeza, Yeye atatusikia
    Kamwe hatutateleza, Mungu kumtegemea
    Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  8. Asiyejitanguliza, kwake kujipakulia
        Awezae kufukuza, wanaotuharibia
        Mwenye kuitekeleza, katiba ya Tanzania
       Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

    9. Yule asiyewabeza, fukara kuwabagua

         Aweza kuwatangaza, mali wanotuibia
        Vijana nao ajuza, aweze kuwatetea
       Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

   10. Awezae kuzitunza, mali zote zaraia
        Wageni wanowekeza, wazingatie sheria
       Aweze kuwahimiza, kodi zetu kulipia
       Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

   11. Ninarudia kukaza, jibu la Watanzania
        Maombi jambo la kwanza, Mola asikie dua
       Mmoja kumchomoza, hata wangekuwa mia
      Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  12. Tumuombeni Muweza, hekima kutujalia
       Tusipate makengeza, wakati wa kuchagua
       Kalamu isijecheza, na kisha tukakosea
       Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

  13. Naomba kuwahimiza, tuombee wagombea
        Mungu aweze watunza, afya usalama pia
       Kampeni kumaliza, bila baya kutokea
      Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

 14. Maadui wanaweza, Uchaguzi kutumia
       Mabaya kuyapenyeza. ili kutuchafulia
      Lakini Mungu aweza, mabaya kutukingia
      Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

15. Jingine linaloweza, majanga kutuletea
     “Media” zikitangaza, upande kuegemea
      Au zikitueleza, mambo yanayochochea
     Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania

 16. Shairi nalikatiza, hapa sitaendelea
       Maneno niloeleza, nibudi kuzingatia
      Mungu uliye Muweza, ibariki Tanzania
     Tuchague kwa makini, viongozi Tanzania
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)