MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
KEJELI KATIKA FASIHI YA KISWAHILI - TANZANIA (6)

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
KEJELI KATIKA FASIHI YA KISWAHILI - TANZANIA (6)
#1
3.3. Kejeli wakati wa utandawazi
Karne ya ishirini na moja kwa hakika imeshuhudia kuingia kwa teknolojia mpya katika nyimbo za Kiswahili. Teknolojia hii ilijiimarisha kwa kiwango cha juu na kupata
mashiko na mwelekeo wa utandawazi. Utandawazi si mfumo mpya katika ulimwengu wa
sayansi ya habari na teknolojia mpya. Mfumo huu umekuwepo kwa karne nyingi japo
kwa viwango tofauti kutoka karne moja hadi nyingine.
Kuingia
kwa dhana ya utandawazi katika fasihi simulizi kumeleta maingiliano na
mabadiliko mengi Kitaifa na hata Kimataifa katika tanzu zake nyingi. Kwa upande
wa mashairi na nyimbo maingiliano haya yanaonekana dhahiri na kuleta mabadiliko
makubwa katika jamii. Vijana wengi hususan wale wa Afrika ya Mashariki
walizitumia mashairi yao kuielezea jamii juu ya matatizo wanayopambana nayo
kila siku. Mathalani ukosefu wa ajira, umaskini waliokuwa nao, athari za
ukosefu wa ajira kwa vijana, uongozi, polisi, mahakama, n.k..
Kutungwa,
kuimbwa na kuonekana majukwaani kwa wasanii na mashairi haya kumewezesha vijana
kuwa wabunifu, wajasiriamali na weledi wa kueleza kero zao na matatizo
wanayopambana nayo katika maisha ya kila siku. Kwa mfano, mashairi ya msanii Ras
Lion katika wimbo Umasikini Huu:
Umaskini
huu (x 3) Utaisha lini
Umaskini
huu (x 3) Utaisha lini
Umasikini
huu (x 3) Utaisha lini
Msanii
analalamikia kwa masikitiko makubwa umasikini uliokithiri tanzania bila ya
kupata jibu ya kuwa mwisho wake ni lini. Kwa upande mwingine anaikejeli nchi za
Tanzania pamoja na viongozi wake ambapo kila siku wanaulalamikia huku nchi ni
inao utajiri mkubwa wa raslimali. Hii inatuonyesha wazi kuwa msanii anaona
uchungu sana juu ya umasikini unaozikumba nchi zetu ilhali viongozi wake ni
matajiri.
Msanii
Jaffer Rhyme yaliyopo wimbo wake wa Niko Bize yaani nina shughuli nyingi,
anasema:
(…)
ndiyo pekee inayonifanya nipate ninachotaka
Umenipata
(brother) kaka ofisini hatujaliwi
Ndio
sababu hasa tunasafa, Kwenye muziki cash tunapata
Niko
Bize naandika rhyme kila time nnayopata
Sio
bize tu for nothing, Bize nageti something
Kwenye
life time hivi sasa kazi ni kazi afisa
Ili
mradi tu inalipa ukiifanya kiuhakika
Ni
mfano mwingine wa kejeli inayowasema viongozi wa siku hizi. Kiongozi kila siku
anakuwa safarini bila kujali nchi yake na wananchi wa eneo lake wanaishi namna
gani. Kila siku kiongozi anapoulizwa jambo fulani yeye anajibu kuwa hana nafasi
kwa kuwa ana kazi nyingi (Niko Bize).
Kuwa bize huko hakumsaidii yeye wala wananchi wake bali hutumika kama fimbo ya
kukwepea majukumu yake.
Kwa
upande mwingine, msanii Jaffer Rhyme anaongeza kwamba wapo viongozi wengine
ambao wako bize kwelikweli. Hawa ni wale waliomeza au walikunywa damu ya
bendera. Viongozi hawa ni wale wenye kuona uchungu kwa wananchi wake. Hawa ni
wale wenye kujitoa mhanga kwa ajili ya kuitetea jamii nzima bila kujali uwezo
walionao wanajamii. Pia hawa ni wale viongozi wanaokosa muda wa kuzurura ovyo
na kupata nafasi ya kuwasikiliza wananchi waliowachagua. Maudhui ya mashairi
haya ndio msingi mkuu wenye kujengwa na utandawazi.
Kwa
upande mwingine tunauona mashairi ya Mr
Ebbo katika wimbo wa Mi Mmasai Bana:
Mi
Mmasai bwana nasema mi Mmasai,
Nadumisha
mila zile wengine walishashindwa,
Mi
Mmasai bwana nasema mi Mmasai.
Naruhusu
kushangaa kwa wageni na wenyeji,
Mi
Mmasai bwana nasema mi Mmasai.
Tamaduni
asilia ilobaki Afirika…
Msanii
anatamba kwa kulisifia kabila lake la Kimasai, mila na desturi za Kimasai
zilizomzunguka na ambazo zinazomshangaza kila mtu. Anasema kuwa hata utandawazi
utandawae namna gani yeye hawezi kuuacha utamaduni wake huo. Mmasai huyu kwa
namna moja au nyingine anawasema wale wote wenye tabia ya kuukana utaifa wao na
kuufurahia utaifa wa wengine kuwa hawatafaidika lolote. Aidha mashairi haya
yanazisema nchi na makabila mengi kuwa yameshindwa kudumisha tamaduni zao na
kuiga tamaduni za kigeni.
Mashairi
ya wasanii wengi yamegubikwa na kasumba waliokuwa nayo wanajamii wengi ya kuwa
Kiingereza ni lugha ya wasomi. Kwa kasumba hiyo wasanii wanachanganya na lugha
za Kiingereza na Kiswahili/Kabila jingine kama mbinu za kuwapata wapenzi wengi
na wasomi. Kwa mfano mashairi ya msanii Lady JayDee katika wimbo wake What I need from you is understanding:
Ninachotaka
kutoka kwako maelewano
What
I need from you is understanding
nakupenda,
nakutaka nakuhitajiii
I
love you, I need you …
Nakupenda,
Nakutaka …
 
Msanii
huyu pamoja na wengine wamesahau kwamba lugha ni kitu cha kujivunia kwa sababu ndio
kielelezo cha utamaduni wa taifa. Aidha utamaduni ndio msingi na roho ya taifa
lolote. Nchi ambayo haina Utamaduni wake yenyewe ni sawa na mkusanyiko wa watu
wasio na roho ya kuwawezesha kujiita taifa.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)