MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
KEJELI KATIKA FASIHI YA KISWAHILI – TANZANIA (7)

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
KEJELI KATIKA FASIHI YA KISWAHILI – TANZANIA (7)
#1
4. Hitimisho
Tumeona
kwamba kejeli haitumiki tu katika kuukosoa uongozi katika jamii, ni mzaha wenye
kuweza kuwasema, kuwasengenya, kuwakebehi wanajamii wote kwa lengo la
kuwarekebisha, kuwaonya na kuwaelimisha ili waende sambamba na wanajamii
wengine. Kejeli haitumiki kwa lengo la kuwakosoa viongozi na watu wa tabaka la
chini tu, bali hutumika kuwakosoa hata wanazuoni wenye kwenda kinyume na
taaluma.
Kejeli
ni mojawapo ya mbinu ambazo hutumiwa na wasanii na waandishi katika muktadha wa
kuelimisha, kukosoa na kuburudisha jamii. Aidha, kejeli hutumika kwa malengo ya
kuyaweka wazi mambo yaliyopo katika jamii, kulingana na mabadiliko na matukio
yaliyopo na yanayotokea.
Kejeli
hutoa uhuru wa waandishi na wasanii. Kwa hakika hii ni njia ya pekee sana
ambazo inawapa wanajamii nafasi ya kushiriki kwa katika kuwakosoa walioko
madarakani na kuifanya kazi yao kuwa nyepesi kueleweka.
Katika
kipindi cha ukoloni, kipindi cha baada ya ukoloni na kipindi tulichonacho hivi
sasa cha utandawazi, mbinu za kejeli zimekuwa zikibadilika badilika. Hii
inawezekana kwamba ni kwa sababu kadri ya mfumo wa maisha na mbinu mbalimbali
za kupambana na mabadiliko hayo ya maisha zinavyobadilika, ndivyo na mbinu za
kejeli zinavyobadilika. Kwa mfano hivi asa vijana wamebuni michezo ya
kuchekesha inayorushwa katika baadhi ya vituo vya televisheni vya Tanzania kama
vile Ze Komedi iliyokuwa ikionyeshwa
kwenye EATV chaneli 5, The Original
Komedi inayoonyeshwa na TBC Mizengwe
inayooneshwa kwenye kituo cha ITV; na baadhi ya vituo vya televisheni vya Kenya
kama Vitimbi au Vioja Mahakamani vinavyooneshwa na kituo cha KBC wanaitumia kejeli
kuusema uozo, ufisadi, unyama, udhalilishwaji, unyanyapaa na ukandamizwaji
ulioshika kasi katika jamii. Aidha vikundi hivi hutumia kejeli kuwasema
wafanyakazi, wala-rushwa na wanajamii vigeugeu walioko na wanaoziongoza nchi na
jumuiya mbalimbali. Kufanya hivyo kunaisaidia jamii iliyoko mbali na miji mikuu
kufahamu kinachotokea ndani na nje ya nchi yao.
Vikundi
vya vichekesho na dhana yao ya kejeli husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza
uchovu wa wanajamii baada ya shughuli nyingi na nzito za mchana kutwa. Hii ina
maana kwamba jamii inapokusanyika pamoja na kuburudishwa kwa kuviangalia
vikundi hivi vya vichekesho, inapunguza uchovu kwa kucheka na kufurahi. Hii pia
ni kwa sababu, maigizo yanayo manufaa kwani yanabeba ujumbe muhimu ambao kwa
hali ya kawaida hauwezi kubebwa na sanaa nyingine. Kwa mfano, suala la UKIMWI
ni vigumu kuliongelea kwa urahisi bila kuigiza au kwa kuonyesha picha. Kwa
kupitia vichekesho vyenye kejeli wana- jamii hujikuta wakiwa na shughuli za
kufanya baada ya kazi na kujiepusha na mambo mengi yenye kusababisha maambukizo
na usambazaji wa Virusi vya UKIMWI.
Ifahamike
wazi kwamba, kejeli katika fasihi ya Kiswahili na kumbo zake hubeba ujumbe
mzima wa kazi ya msanii au mwandishi kisaikolojia, kifani na kimaudhui katika
kujikamilisha kwake.
Kwa
mfano, wanamuziki wetu wa kizazi kipya, wana taarabu, wacheza maigizo,
wachekeshaji, wanakomedia, wanakomiki na vikundi vingine vingi vya kisanii.
hutumia kejeli kuielimisha jamii juu ya janga la madawa ya kulevya. Wasanii
wetu hawa wamefanikiwa kwa kuiangazia misuguano iliyopo katika serikali,
jitihada za kuinua uchumi, maisha bora, n.k..
Hivyo
ni wajibu wa wasanii, waandishi na wanazuoni wengine kuhakikisha kuwa
wanaitumia mbinu hii na kuiendeleza ili kufichua uozo, ubadhirifu, ufisadi,
ufidhuli uliopo, unaojitokeza na unaozidi kujikita katika jamii na taifa zima
kwa ujumla.
MAREJELEO
 
Balisidya,
M. L. 1982. Uchunguzi katika fasihi simulizivizingiti na mkabala. Katika makala
za
semina
za TUKI na makala mbalimbali. Dar es Salaam. TUKI.
Gibbs,
R. W. 1994. The Poetics of Mind. Figurative thought, Language &
Understanding.
Cambridge:
Cambridge University Press.
Honero,
L. N. na wenzake. 1980. Matunda ya Azimio la Arusha, Mashairi ya Mwamko wa
Siasa.
Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili: Dar es Salaam.
Kezilahabi,
E. 1988. Karibu Ndani. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.
Kezilahabi,
E. 1999. Kaputula la Marx. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.
Khatibu,
M. S. 1988. Fungate ya uhuru. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.
Mbatiah,
M. 2001. Kamusi ya Fasihi. Nairobi: Fotoform Ltd.
Mbogo,
E. 1981. Morani. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.
Mtesigwa,
P. C. K. 1989. Methali ni nini? Katika Mulika juzuu Na. 56 Dar es Salaam: TUKI.
Muhando,
P. 1984. Lina Ubani. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.
Mvungi,
T. A. 1985. Chungu Tamu. Dar es Salaam: Tanzania Publishing House.
Mvungi,
T. A. 1978. Raha Karaha. Dar es Salaam: Continental Publishers.
Mvungi,
T. A. 1995. Chekacheka. Dar es Salaam: Continental Publishers.
Mwakyembe,
H. 1980. Pepo ya Mabwege. Dar es Salaam: Longman.
Mulokozi,
M. M. 1989. Tanzu za fasihi simulizi. Katika Mulika juzuu Na. 21 Dar es Salaam:
TUKI.
Ngahyoma,
N. 1975. Kijiji Chetu. Dar es Salaam: Tanzania Publishing House.
Penina,
M. M. 1984. Lina Ubani. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.
Ruhumbika,
G. 1995. Miradi Bubu ya Wazalendo. Dar es Salaam: Tanzania Publishing House.
Rutashobya,
M. G. R. 1980. Nuru Mpya. Dar es Salaam: Tanzania Publishing House.
Kandoro,
S. 1971 Mashairi ya Saadani. Dar es Salaam: Mwananchi Publishing Ltd
Shaaban,
R. 1951. Kusadikika. Nairobi: Nelson & Sons.
Shaaban,
R. 1968. Kufikirika. Nairobi: OUP.
Short,
M. 1980. Style in Fiction. London: Longman
Wales,
Katie 2001. A Dictionary of Stylistics. Harlow: Personal Education.
Wamitila,
K. W. 2008. Kanzi za Fasihi. Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi: Nairobi Vide Muwa
Publishers Ltd.
 
SHUKRANI
ZA PEKEE KWA:  STEVEN
E. MRIKARIA[url=http://www.qucosa.de/fileadmin/data/qucosa/documents/9089/17_09_Mrikaria.pdf][/url]
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)