MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
UTUNZI WA ABDILATIF ABDALLA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
UTUNZI WA ABDILATIF ABDALLA
#1
   
Je, mazingira yameathiri utunzi wa Sauti ya Dhiki kwa namna gani?
Mwandishi: ABDILATIF ABDALLA
Mhakiki: Prof. Mtarajiwa
Utangulizi
Nitaanza kwa kusema kuwa mazingira ni jumla ya vitu vinavyomzunguka binadamu au kiumbe. Pili, naomba wasomaji wangu watambue kuwa, Sauti ya Dhiki ina mashairi ambayo yanaweza kuingia katika makundi matatu yafuatayo:
(a) Yale yanayoonesha msimamo wa mwandishi katika jukumu la kutetea haki na maslahi ya umma.
(b) Yanayohusu yeye binafsi
© Yanayoonesha mikinzano ya ndani katika hisia za mtunzi
Ili kuelewa zaidi, itabidi niwakumbushe tu baadhi ya waandishi ambao waliwahi kujipata gerezani ili tuoanishe waliyopitia na yaliyompata mtunzi wa Sauti ya Dhiki. wa kwanza ni Dennis Brutus wa Afrika Kusini ambaye mashairi yake yanapatikana katika kusanyiko liitwalo Letters to Martha najua mmesoma kazi hiyo na kwa wale anbao bado, hebu niwape ubeti mmoja:
Aha moyo wangu, penzi la tumaini langu lililopotea,
Mwenzi wangu, kutokuwepo pamoja na njaa, vyasambaa katika vizio vyangu vya dunia
moyo wangu wafahamu sasa kumbo kama hilo
Mwandishi Wole Soyinka naye akaandika The Man Died baada ya kutiwa gerezani na serikali ya Naijeria.
Abdillatif Abdalla naye anajipata gerezani baada ya msimamo wake. Natumai mmesoma jambo lililosababisha yeye kutiwa gerezani. Katika gereza baridi la Kamiti, Mtunzi anapitia balaa ba balaa hii ndiyo inamfanya atunge mashairi mbalimbali. Katika utafiti huu, nitaangazia na kuchambua namna mazingira mbalimbali yalivyochangia utunzi wa mashairi mbalimbali.
mazingira ya upweke
Mazingira haya yalimpa mtunzi wasiwasi na woga. Mara nyingi alikuwa katika hali ya kufikiria tu. Shairi ambalo linadhihurisha kuwa mazingira ya upweke katika gereza ka Kamiti yalimwathiri ni shairi la Nakukumbuka ambapo anasema na mpenzi wake. Anasema:
mie nawe mbali tungawa, nakukumbuka
lau ningekuwa na mbawa, ningaliruka
ni muhali hilo kuwa, nasikitika
Shairi hiki ni thibitisho kuwa mtunzi alikuwa na upweke kiasi cha kuanza kumkumbuka mpenzi wake.
mazingira ya mateso
Haya ni mazingira mapana sana katika Sauti ya Dhiki. Katika hali ya mateso, Mtunzi anatunga mashairi kama Nishishiyelo ni Lilo yaani aliloshikilia ndilo hilo na hatobadili nia. Hebu tuone ubeti mmoja katika uk 2:
kweli menifunga ndani, ya chumba nde sitoki
kutwa kucha ni chumbani, juwa kuota ni dhiki
na mlinzi mlangoni, yu papo kattu handoki
nilindwavyo bilkhali, ni kama simba marara
Hapa tunaona kuwa mtunzi anateswa sana Haruhusiwi hata kuota jua na hivyo anatunga mashairi ya masikitiko.
mazingira ya vitisho
Ni bayana kuwa mtunzi alikuwa katika mazingira ya vitisho katika taifa lake na pia katika gereza ka Kamiti. Shairi lake moja la Semani wenye Kusema ni mfano bora wa shairi ambalo linaonyesha kuwa mtunzi alikuwa katika mazingira ya vitisho kwani hata wale ambai walikuwa naye, sasa hawasemi...ndipo anawaambia, waseme bila woga.
mazingira ya utabaka na mivutano ya kijamii
Mazingira haya ambayo ni mapana katika jamii pana yamemwathiri mtunzi. hebu tuangalie shairi kama Vuta N'kuvute ni shairi ambalo ni tokea la mazingira ya utabaka.
mazingira ya uongozi dhalimu, siasa duni
Hewaa, mtunzi anatunga mashairi ambayo yanaonyesha athari ya mazingira ya siasa duni. katika shairi kama Mamba, tunaona kuwa jazanda ya mamba ni jazanda ya viongozi ambao hawako tayari kung'oka mamlakani.Anasema kuwa yule mamba anadhani ataishi dahari, yaani miaka yote ....
mazingira ya usaliti
mazingira ya mateso
jadili mazingira zaidi kwa kutoa shairi la kuthibitisha.
Kwa swali au maoni, sema nami tuchangizane.
prof. Mtarajiwa
Dominic.
20/03/2020
Quote:>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>Soma historia yake hapa chini kwa lugha ya Kiingereza
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Abdilatif Abdalla (born 1946 in Mombasa) is a Kenyan writer and political activist. He was imprisoned for his support of the Kenya People's Union, and wrote the poems collected in Sauti ya Dhiki while in solitary confinement, which were subsequently awarded the Jomo Kenyatta Prize for Literature.
Early life
Political imprisonment and writing Edit
When the Kenyan Government of Jomo Kenyatta conducted a crackdown on KPU activists, Abdalla was imprisoned for conspiracy between 1969 and 1972. He was at first held in Kamiti Prison, and later in Shimo la Tewa Prison, where he was kept in solitary confinement. It was while imprisoned that he wrote the poems that would be collected in the 1973 work Sauti ya Dhiki. These were written in the Mombasa version of the Swahili language.[1] He later explained that writing the poems in solitary confinement had kept him sane.[2]
After he was awarded the Jomo Kenyatta Prize for Literature for Sauti ya Dhiki in 1972, he moved in exile to Tanzania. While there he worked as a senior researcher on Swahili at the University of Dar es Salaam and collaborated editing a Swahili dictionary. In 1979, he moved to London and worked for BBC Swahili department, later editing the news magazine Africa Events. Abdalla's only English language poem was published in 1988, entitled Peace, Love and Unity for Whom?. This was in response to an attempt by Daniel arap Moi's government to bribe Abdalla into no longer working with Ngũgĩ wa Thiong'o. Abdalla has since taught Swahili at Leipzig University.
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)