MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JINSI YA KUTAMBUA MZIZI/KIINI KATIKA NENO

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
JINSI YA KUTAMBUA MZIZI/KIINI KATIKA NENO
#1
Mzizi au kiini cha neno huweza kubainika kwa kutumia mbinu zifuatazo:
  • Mbinu ya mnyambuliko/unyambulishaji
Neno husika hufanyiwa mnyambuliko kwa kubadili viambishi kadiri iwezekanavyo na kisha kuchunguza sehemu isiyobadilika katika maneno yaliyotokana na mnyambuliko (vinyambuo).
Mf:
Cheza ——- Mchezo
Mchezaji
Michezo                                   -chez-
Tumecheza
Walivyotuchezesha
 
  • Kuzingatia umoja na wingi
Mbinu hii hufaa zaidi kwa maneno ambayo ni nomino. Nomino zisizo na umoja na wingi aghalabu huwa ni maneno yaliyoundwa kwa mofimu moja hivyo si rahisi kupata mzizi na viambishi.
Mf:
Mtoto ——– watoto  (toto)
Mzee ——— wazee (zee)
Kifaranga —– vifaranga (faranga)
  • Kuzingatia muundo ndani wa neno
Vitenzi vingi vya Kiswahili huwa na muundo ndani na muundo nje. Ili kutambua mzizi wa kitenzi kwa urahisi ni vyema kukirudisha kitenzi katika muundo wake wa ndani. Kitenzi chenye asili ya kibantu muundo wake wa ndani huishia na irabu “a”. Kitenzi kikiwa katika muundo ndani na kuishia na irabu “a” basi hiyo irabu ikiondolewa kinachobakia huwa ndio mzizi.
Mfano:
Walipigana —————- piga ——– pig-
Tumemuimbia ———— imba ——- imb-
Wanasomeshwa ———- soma ——- som-
Iwapo kitenzi katika muundo wake wa ndani kitaishia na irabu tofauti na “a” basi yawezekana neno zima likawa mzizi au shina. Hali hiyo hutokea kwa vitenzi vyenye asili ya kigeni.
Mfano:
Waliosaliana ———- Sali
Walivyostarehe ——- starehe
Tulimuarifu ———— arif
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)