MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: UTU

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: UTU
#1
UTU
Siku hizi ukitaka kupona utapona kwa pesa,
Utakufa bure,
Kufa ni rahisi kuliko kupona!
Wakati ukipambana na afya ya mwili,
Wao hupambana na afya ya mifuko yao,
Heri ufe kuliko kudhoofisha mifukoni!

Pesa ndio huongoza hatua za binadamu,
Bila pesa hufiki popote,
Ukitaka kupumua huulizwa una bei gani?
Pesa huamua upumue au ufe,
Na ikisema kufa utakufa.

Watu hawajali vyeti na ujuzi wako,
unamjua nani ndio mpango,
Humjui mtu, rudi na vyeti vyako panya wakafanye mazalia
Ndivyo yalivyo maisha,
Kila jambo limeshapigiwa mstari,
Ukibishana nalo unagonga ngumi ukutani lazima utachubuka.

Wanasema sisi watakatifu
Hatuna chembe ya ukabila
Bado hamjatembea, Kuna watu maarufu wa kubebana.
Eti hizo ni konekisheni,
haina haja uzoefu wako,
Umesoma wapi na lini utaambiwa kajiajiri

Wanatangaza watu wajiajiri
Wao wameajiriwa
Wanabadilisha VAT hawana karaha Kama zetu
Basi wanazidi kuhubiri jiajirini!

Wengine hawana vyeo, Wala ukiranja
Ila matendo ya kinyama yamewatawala,
Hao huparamia vichanga na kuvibaka
Maagizo ya waganga wa jadi kuwa watatajirika
Wengine hawalali hupita huku na kule kuvizia mikoba ya Wanawake
Kila mtu huwaza mkono unaendaje kinywani!


Wengine hukata tamaa na kukatisha maisha yao,
Wanaona haiwezekani, Bora nife nikapumzike
Wengine wamejenga mahekalu Sasa tuwaibie watu sadaka,
Mambo ni mengi!
Wanaookota makopo,
Wanaouza miili
Watu hawajali

Wakati ukipambana umshinde adui umasikini,
Mwanga anakuwangia,
Raha yake uendelee kujitundika viraka mwilini,
Yupo radhi asilale
Usiku kucha aje akatike viuno katika chumba chako
ukiamka umetenguliwa mgongo.

Wengine huweka kando jitihada zao
Mume na mke vitani
Wapendanao huuana
Mara tunasikia mke ameuawa na mumewe
Hapo madhila yanawaangukia watoto
Baba jela mama kaburini
Watoto mtaani!

Binadamu hatupendani
Yupo radhi kumtesa mtoto wa mwenzake eti hakumzaa
Atamchubua kwa bakora
Na kumchoma Moto
bila faida ni chuki

Utu! Utu! Utu!
hakuna utu!

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)