MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: UMASKINI WA MAWAZO

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: UMASKINI WA MAWAZO
#1
UMASKINI WA MAWAZO
*****************************
Hini la Nyerere wazo, ni tamko'le makini,
wa umaskini mawazo, mbaya mno jameni,
unapita si mchezo, wowote hii yakini,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
------------------
Busara'ye h'itakufa, na itadumu milele,
maneno'ye yatufaa, yakigonga ja kengele,
fikira'ze zina sifa, Mwalimu mbele kwa mbele,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
-------------------
Kale hadi enzi hizi, umasikini tatizo,
wa halisi ukombozi, ni ule wa kimawazo,
kama haupo ni wazi, kinakuwa ni kikwazo,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
------------------
Kula kiundwacho kitu, huanza waza malengo,
vyombo tumizi kwa watu, hutokana na ubongo,
tunapata zana zetu, kwa kufinyanga udongo,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
-------------------
Na hauwezi kushinda, bila ushindi ku'waza,
huwezi kitu kuunda, pasi kwanza kukiwaza,
huwezi safari kwenda, uendako hukuwaza,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
-------------------
Uongozi bora upo, ikiwa safi siasa,
ardhi ya kutosha ipo, watu salama kabisa,
zahanati shule zipo, miundombinu h'ijakosa,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
-------------------
Fikiria uno baba, mwenyi shamba kubwa sana,
linayo nyingi rutuba, na mvua yapatikana,
siha'ye ni marhaba, 'ti ni fukara anena,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
--------------------
Wa mawazo mkosefu, na huwa hajiamini,
hujisikia dhaifu, hajuwi yake thamani,
m'endeleo ayahofu, ya duni ndo atamani,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
-------------------
Bongo tuzitumikishe, mbele tuweze kusonga,
ili tuzikamilishe, njozi zetu kuzijenga,
uzembe Mola tupishe, tuachane na ujinga,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.
-------------------
Za mwalimu ninakiri, fikira'ze ni makini,
sana tuzitafakari, tuzienzi wajameni,
Nyerere ni mshauri, zama zote wa thamani,
umaskini wa mawazo, umasikini mbaya.

_________________________________

Rwaka rwa Kagarama, Mshairi Mnyarwanda.
Jimbo la Mashariki, Wilaya ya Nyagatare,
JAMHURI YA RWANDA.       
????????????
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)