MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'AMANI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO 'AMANI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AMANI'

Neno amani  katika lugha ya Kiswahili ni Nomino [Ngeli: i-/zi-] yenye maana zifuatazo:

1. Hali ya kuwapo utulivu dhidi ya usumbufu

2. Hali ya kuwa na usalama na utulivu; kutokuwa na vita au vurugu (machafuko) yoyote.

3. Makubaliano ya usalama baina  ya nchi zenye vita.

Katika lugha ya Kiarabu neno amani linatokana na neno la Kiarabu  amaanun (soma: amaanun/amaanan/amaanin أمان) lenye maana  zifuatazo:

1. Kusalimika; usalama; jina linalotokana na Kitenzi cha Kiarabu amina امن amesalimika.

2. Hali ya kuwapo utulivu.

3. Ahadi; makubaliano baina ya watu wawili au watu wengi.

4. Ulinzi.

5. Ukweli; kutokuwapo udanganyifu au dhulma.

Kinachodhihiri ni kuwa neno amaanun  امان  lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa  kuwa neno amani maana yake katika lugha ya asili - Kiarabu inayohusu usalama na utulivu haikubadilika na maana ya makubaliano baina ya nchi zenye vita iliongezwa.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda
Reply


Messages In This Thread
ETIMOLOJIA YA NENO 'AMANI' - by MwlMaeda - 04-20-2022, 02:01 PM

Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)