MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI: JENEZA LA AJABU **SEHEMU YA 01*

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI: JENEZA LA AJABU **SEHEMU YA 01*
#1
SIMULIZI: JENEZA
LA AJABU
Mtunzi: HAKIKA JONATHAN
**SEHEMU YA 01*
Ikulu kwa mfalme ;
“Siwezi kufa
kirahisi namna hii, dunia tamu bwanaaa weeeh, mali zangu hizi nitamuachia
nani?? “,yalikuwa ni maneno ya kejeli kutoka kwa mfalme wa nchi ya
Mwamutapa, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa mganga wake wa kienyeji kuwa
kashindwa kumtibu maradhi yaliyokuwa yakimsumbua, hivyo asubili kufa tu. Hali
iliyopelekea mganga yule kujuta kauli yake kwani, mfalme aliamuru auawe kwa
kukatwa kichwa chake, na kisha kiwiliwili chake kitupwe ndani ya bwawa la mamba
waliofugwa na mfalme kwa ajili ya kula watu waliomchukiza na kumpinga katika
uongozi wake. “Yani mimi nife, siwezi kufa mimi, labda utangulie mpuuzi
wewe “,mfalme Mutapa, alijitamba kwa mala nyingine tena, huku akishuhudia
kichwa cha mganga wake kikitenganishwa na kiwiliwili,kutokana na kushindwa
kumtibu mfalme na kumwambia asubili kifo tu, jambo ambalo mfalme alilichukulia
kama katukanwa na kudharauliwa.
Mitaani katika nchi ya
Mwamutapa;
       Hali ngumu ya maisha inazikumba familia
nyingi katika ardhi ya Mwamutapa, huku lawama nyingi zikitupwa kwa mfalme,
kwani wanaume wengi wenye nguvu na vichwa vya familia, walitumikishwa kwa nguvu
katika mashamba ya mfalme na kisha kulipwa ujira mdogo,jambo ambalo
lilimchukiza kila raia wa Mwamutapa. Kelele zao za mateso hasikusaidia
chochote, kwani kila mtu aliyejifanya kupinga kunyanyaswa, alijikuta akiuawa
kikatili, hali iliyowaogopesha wengine na kujikuta wakikubaliana na manyanyaso
kutoka kwa mfalme, kwani waliogopa kifo.
“Naamini ipo siku
yatakwisha, usilie mama yangu “,ilikua ni sauti kutoka kwa kijana mkakamavu
Njoshi, akimunyamanzisha mama yake, baada ya kupokea taarifa za kifo cha mume
wake kwani alishindwa kumtibu mfalme. “Mwanangu baba yako kaondoka,
tumebaki wawili tu, nakuomba uachane na Grace, mfalme atakuua  na wewe, tegemeo na faraja langu lililobakia
“,mama Njoshi alizidi kulia kwa uchungu, huku akimusisitiza mwanae
kuachana na Grace,msichana mrembo sana na mtoto pekee wa kike wa mfalme. Jambo
ambalo kwake aliliona ni gumu sana na halitowezekana, kwani alimpenda sana
Grace licha ya kupokea vitisho  mala
kadhaa kutoka kwa mfalme ili aachane na Grace. Na kila mala mfalme alipojaribu
kumuua Njoshi alishindwa, kwani alifanikiwa kutegua mitego yote aliyotegewa ili
aweze kufa, kwani alikua ni hodari sana na aliweza kulishinda jeshi la mfalme
mala nyingi, moja ya sababu ambazo Grace zilimfanya ampende sana Njoshi, kwani
alihitaji mwanaume atakaye muoa awe ni shujaa na si mwanaume suruali tu,
asiyeweza kumlinda na hatari yoyote.
“Usjali mama, mimi
nipo siku zote, nitakulinda, lakini naamini ipo siku Mwamutapa itakua huru, na
mimi nitakuwa kiongozi wake “,kijana Njoshi aliongea kwa ujasiri na
kujiamini kwani ziku zote alifanya mazoezi ya kila aina, ili tu siku moja
afanye mapinduzi na kuokoa wananchi dhaifu kutoka kwenye utumwa na uongozi wa
mabavu wa mfalme Mutapa, jambo ambalo mama yake aliliona kama ndoto ya mchana,
ambayo Njoshi alikuwa akiota.
“Mwanangu banaa
unanifurahisha, hebu toa upuuzi wako huko “,mama Njoshi aliongea huku
akitabasamu kwa mbali kutokana na maneno aliyoambiwa na mwanae, na kumfanya
asahau machungu ya kumpoteza mume, japokuwa alikuwa ameshazoea na kuona kama
vifo ni jambo la kawaida katika familia yake, huku akikumbuka jinsi wanae
watatu walivyopoteza maisha kutokana na njaa kali iliyotokea miaka kadhaa
iliyopita, na kumuachia Njoshi pekee. “Nakuombea mwanangu, ndoto zako ziwe
kweli “,mama alizungumza huku akimkumbatia mwanae, bila kutambua kuwa
Njoshi alijawa na hasira, huzuni na machungu kwa kumpoteza baba yake na kuapa
kulipiza kisasi, kwani hakutaka mama yake agundue huzuni hiyo na kuzidi kumpa
machungu mama yake aliyempenda sana.
Ikulu kwa Mfalme :
Mganga maarufu wa kienyeji aliyesifika
katika nchi ya Mwamuyeshi, nchi iliyopakana na Mwamutapa, na kuongozwa na
mfalme Muyeshi ,anafika ikulu kumtibu mfalme maradhi yake, baada ya Muyeshi
kupata taarifa za rafiki yake mpendwa kuugua kwa muda mrefu, hali iliyopelekea
kumtafuta muganga katika ardhi yake ili amsaidie rafiki yake asiweze kupoteza
maisha. “Karibu sana katika ardhi ya Mwamutapa,,, naamini rafiki yangu
ndiyo kakutuma hapa “,mfalme Mutapa aliongea bila shida yoyote huku
akitabasamu,huku akiwa amelala katika kitanda chake kwa takribani mwezi mmoja
sasa bila kuamka kutoka kitandani, japo aliweza kuzungumza vizuri kama vile hakuwa
mgonjwa.
     “Ndiye mimi mtukufu mfalme, mganga
kutoka katika ardhi ya rafiki yako Muyeshi, nimekuja kukusaidia “,mganga
yule aliongea huku akijiamini, na kumfanya mfalme atabasamu kwani hakupenda
kufa, na alitamani aishi milele jambo ambalo mganga yule alikua ameshalitambua.
“Usjali mtukufu
mfalme, mpaka sasa nimeshachelewa siwezi kukutibu, muda wowote kuanzia sasa
utaweza kufa, lakini inatakiwa ukifa uzikwe ndani ya jeneza lililotengenezwa
kutoka katika miti iliyo katikati ya msitu hatari wa Majini, msitu ambao uko
katika ardhi yako ya Mwamutapa, ukizikwa ndani ya jeneza hilo, utaweza kufufuka
baada ya wiki moja na kuishi milele “,mganga yule alizungumza maelezo
marefu sana, huku jina la kijana Njoshi likijirudia rudia ndani ya kichwa cha
mfalme, kwani ndiye kijana pekee aliyemuona anafaa kufanikisha swala hilo, na
kutoka akiwa salama katika msitu hatari wa Majini, msitu ambao hakuna aliyewahi
kuingia humo akitaka mali, watoto au ufalme kutoka kwa mizimu ya msitu huo na
kutoka salama bila kupoteza maisha. “Na pia inatakiwa iwe siri, raia wako
wasifahamu labda tu atakayekwenda huko msituni “,mganga alizidi kuzungumza
huku mfalme mawazo yakiwa mbali sana, kwani mwanae Grace alishamuonya kuwa
Njoshi siku akipata matatizo yaliyosababishwa na yeye, ataweza kujiua, jambo
ambalo mfalme hakuwa tayali kumkosa mwanae wa kike pekee aliyenaye, kati ya
watoto arobaini kutoka kwa wake watano alionao ,mtoto ambaye alizaliwa na mke
wa tano baada ya wake zake wanne waliotangulia kushindwa kumzalia mtoto wa
kike.
       “Sawa …sawa sa…wa ni…me…kusikia
“,mfalme alijibu bila kujitambua huku mawazo na maswali lukuki
yakikisumbua kichwa chake .
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)