MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU ” *SEHEMU YA 06**

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU ” *SEHEMU YA 06**
#1
SIMULIZI : “JENEZA
LA AJABU “
*SEHEMU YA 06**
Msitu wa majini;
Viumbe hatari wa msituni ghafla
wanasikia kishindo katika moja ya mitego waliyokuwa wametega, hali hii
inawafanya wagundue kuwa tayali adui yao alikuwa ameshaingia msituni, kwani
hawakuweza kumuona katika ramani zao, na hata walipotumia uwezo wao wa kijini,
walishindwa kumuona adui yao, mala baada ya Njoshi kujifunga kiunoni kitambaa
cheusi alichopewa na mama yake. “Jamani tayali adui alishaingia msituni,
fanyeni kila njia mumkamate akiwa hai au amekufa “,jini mweupe, kiongozi
wa askari wa msituni, alitoa amli ya kuanza kumtafuta adui, baada ya kufika
katika eneo ambalo kishindo kikubwa kilisikika, na sehemu ambayo walitega mtego
wao, na kukuta kamba ya mtego ikiwa inaning’inia baada ya kukatwa huku adui
akiwa ameshatoweka.
“Nazani mnaisikia
harufu ya binadamu, hayuko mbali, mtafuteni haraka sana ” ,jini mweupe
alizidi kuongea na kuliamlisha jeshi lake la msituni, kumtafuta adui baada ya
kuhisi harufu yake katika eneo lile la mtego, eneo ambalo lilizungukwa na vichaka
pamoja na miti mirefu.
********
Baada ya Njoshi kuponea
chupuchupu kutoka katika mtego, haraka sana anaingia ndani ya kichaka chenye
majani marefu, kwani alitambua kuwa majini wa msituni lazima wafike katika eneo
lile muda sio mrefu baada ya kusikia kishindo kile kikubwa, hivyo asingeweza
kukimbia na kufika umbali mrefu bila kukamatwa.
Lakini ukistaajabu ya
Musa, utayaona ya firauni, Njoshi alishangaa sana baada ya kuliona kundi kubwa
la majini, likifika eneo lile haraka sana huku akiwa hata hajajificha vizuri
kwenye majani. Kwani viumbe wale walikuwa na uwezo wa kupotea na kufika eneo
lolote walilolitaka wao, ndani ya sekunde tu, kwani hawakuwa binadamu bali
majini, tena majini hatari wa msituni, msitu ambao ulikuwa maarufu katika nchi
ya Mwamutapa, pamoja na ulimwengu mzima, kutokana na utajiri wake.
“Mungu wangu,
mbona hawanioni “,Njoshi alistaajabu sana kwani kiongozi wa askari wale,
jini mweupe alisimama karibu sana na kichaka kile, na ilikuwa imebakia kidogo
amkanyage Njoshi kwani alikuwa hata hajajificha vizuri katika kichaka, eneo
ambalo mtego ulikuwepo.
Njoshi ujasiri ukiwa
umetoweka, alianza kutetemeka kwa woga kwani majini wale walitisha sana kwa
kuwatazama, wengine walikuwa na mguu mmoja huku wakiwa na vichwa vingi sana,
pamoja na mikono zaidi ya miwili. Njoshi akiwa anatetemeka aliamua kufumba
kinywa chake asiweze kupiga kelele, kwani jini mweupe, aliyekuwa na kichwa cha
nyoka aina ya koboko, huku akiwa na mwili mweupe tena wa binadamu, alitoa amli
ya kumsaka Njoshi katika kichaka kile, kwani waliweza kuhisi harufu yake.
“Asante mizimu ya
mababu, sionekani, leo nilikuwa nimekwisha “,Njoshi akiwa amejifumba mdomo
wake kwa kutumia viganja vya mikono, aliishukuru mizimu, kwani majini waliokuwa
wanatisha sana walipita karibu yake bila kumwona, jambo ambalo lilimshangaza
sana kwani sehemu kubwa ya mwili wake ilikuwa wazi na hakufunikwa vizuri na
majani, bila kutambua kuwa mkanda ule wa kitambaa cheusi aliouvaa kiunoni,
ndiyo uliyosababisha majini wasiweze kumuona.
“Msitu huu niliuskia
tu, leo nimejionea mwenyewe “,Njoshi aliongea moyoni huku akiwa
anamshangaa askari mmoja wa msituni,mwili wake ukiwa umebakia mifupa tu,huku
akiwa ameshika mshale, na kusonga mbele, lakini Njoshi alishindwa kutumia hata
panga lake kuwaangamiza majini wale kwani hakutambua matumizi yake, huku yeye
akiwa anashangaa muonekano wa majini wale na kuzidi kumuongezea woga.
Mwamutapa
Asubuhi mida kama ya saa moja, kijana
Ngesha aliamka kutoka usingizini, na kunawa uso ili aelekee nyumbani kwa rafiki
yake, ili asikute wameshaondoka kwenda shambani.
“Mwanangu mbona
haraka sana asubuhi hii, unaenda wapi ” ,ilikuwa ni sauti ya mama yake
Ngesha, mama ambaye alibaki mjane baada ya mume wake kuitwa na mfalme,na
alipokwenda huko hakuweza kurudi.Kwani alipofika ikulu kwa mfalme,alikuta kundi
kubwa la wanaume wakiwa huko wanasaga unga wa mahindi kwa kutwanga kwenye
vinu,lakini baada ya kumaliza kazi hiyo na kudai malipo yao ,kundi lote
lilitupwa kwenye bwawa la mamba bila huruma ,amli iliyotoka kwa mtoto mkubwa wa
kiume wa mfalme.
Lakini mama Ngesha kila
alipojaribu kuulizia kwa mfalme kuhusu mumewe ,hakuweza kupatiwa jibu sahii
zaidi ya vitisho.Kitendo kilichomfanya mama Ngesha pamoja na mwanae kuweka
msiba nyumbani kwani tayali waliamini mzee wao aliyejulikana kwa jina la
Mugina,alikuwa ameuawa,jambo ambalo lilikuwa kweli.
“Naenda kumsalimia
rafiki yangu Njoshi,mara moja,” Ngesha alimjibu mama yake na kisha
kutokomea huku akikimbia ili kumuwahi Njoshi,kwani  ilikuwa ndio mida  ya Njoshi na mama yake kwenda shambani.
Ikulu kwa mfalme;
       Asubuhi na mapema siku ya jumanne,siku
ambayo usiku uliopita kijana Njoshi alitoweka ikulu kuelekea katika msitu wa
majini,kwenda kuchukua jeneza la ajabu kwa ajili ya kumzikia mfalme atakapokufa
,na kisha  kufufuka ndani ya wiki moja.
Vilio vinatawala katika
ngome yote ya mfalme,huku familia nzima ya mfalme pamoja na wafanyakazi wote
wakilia kwa kwikwi,ama kweli mkuki kwa ngurue kwa binadamu mchungu,leo hii
maneno haya yalijidhirisha waziwazi.Walizoea kuona wengine wakilia,lakini leo
ilikuwa ni zamu ya familia ya mfalme kulia.
“Baba rudi,baba
rudi baba yangu nakupenda”,msichana Grace alilia kwa huzuni,huku akitamka
maneno ambayo yaliongeza uchungu katika familia nzima ya mfalme.Walitamani sana
Njoshi afanikiwe kurudi na jeneza salama,ili mfalme afufuke ndani ya wiki moja
na kuishi milele,lakini hawakuamini kama kweli Njoshi atafanikiwa kurudi
salama,kwani huko msituni alikoenda ni hatari sana.
Nyumbani kwa kina
Njoshi;
        Mama yake Njoshi,akiwa ameshika jembe
kama kawaida yake tayali kuelekea shambani,huku kichwani akiwa na mawazo mengi
juu ya hatma ya mwanae.
Akiwa anatoka nje ya
uzio wake wa nyumba,uzio ambao ulitengenezwa kwa nyasi,Kwa mbali alishangaa
kumuona kijana akija uelekeo wa nyumba yake huku akikimbia.Kitendo hicho
kilimfanya aweze kuweka jembe lake chini,pamoja na kikapu kilichokuwa na maji
ya kunywa pamoja na chakula kwa matumizi ya shambani siku nzima.
“Aiweee…mama
,Njoshi ni memkuta…aiweeh”,Ngesha alimsalimia mama yake Njoshi na kumuulza
kuhusu rafiki yake,huku mama akipumua baada ya kumtambua kijana aliyekuja
nyumbani kwake,na pia hakuweza kuleta taarifa mbaya.
“Aiweeeh
mwanangu,rafiki yako aliitwa na mfalme tangu jana asubuhi,mpaka sasa sina
taarifa yoyote,aiweeeh”,mama Njoshi alimjibu rafiki yake mwanae,na kumtia
hofu sana,kitendo ambacho kilimfanya Ngesha kutoweka bila hata kuaga kuelekea
ikulu,kwani alitambua kuwa rafiki yake lazima atakua hatarini kama kweli
alienda ikulu tangu siku iliyopita na hajarudi mpaka wakati ule.
Kifo cha
mfalme,haitakiwi wananchi wa Mwamutapa wafahamu,zaidi ya familia ya mfalme na
mtu aliyelifuata jeneza msituni,lakini Ngesha kaelekea ikulu kwenda kujua nini
kinaendelea kwa rafiki yake Njoshi.…
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)