MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
NADHARIA YA UHUSIANO: DHANA YA PROPOSISHENI (2)

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
NADHARIA YA UHUSIANO: DHANA YA PROPOSISHENI (2)
#1
DHANA YA PROPOSISHENI
Katie Wales (2001),
anasema kuwa proposisheni ni neno lililoazimwa kutoka kwa elimu ya falsafa.
Maana kiproposisheni katika kauli au sentensi ndio ya kimsingi akilini na
wakati huohuo maana katika proposisheni ni ya kidhahania ambayo huhusisha kiima
na kiarifu. Proposisheni hufanana na vitendo usemi vya kauli. Hulingana
kisarufi na sentensi arifu ambayo huwa na kiima na kiarifu. Hata hivyo, kuna
tofauti baina ya viwango tofauti vya sarufi na maana. Kama vile, sentensi
katika kauli tendaji na katika kauli tendwa zaweza kueleza proposisheni ambayo
yaonekana kuwa moja hata kama zina kiima na kiarifu tofauti.
Kwa mfano:
Mpira
ulichezwa na watoto.
Watoto
waliucheza mpira.
Vilevile, proposisheni
yaweza kuwa na maana zaidi ya moja, kama ina utata. Kwa mfano:
Joy
amepigia Judy mpira.
Maelezo katika mfano , yana maana kuwa labda Joy alimpiga Judy kwa sababu ya Mpira au pengine
alimpigia mpira ili wacheze pamoja, vilevile huenda ikawa Joy aliupiga mpira
kwa niaba ya Judy. Hivyo basi, proposisheni katika sentensi hii tabainika kama
msemaji ataeleza bayana maana aliyoikusudia katika kutamka kauli hii.
Kulingana na Halliday
(1985), proposisheni hukubaliwa au kukataliwa. Hii ina maana kuwa kama ni ya
ukweli ambao unaweza kuthibitika, basi itabidi washiriki katika mazungumzo
kuikubali na kuamini jambo lililomo katika proposisheni hiyo. Kwingineko, kama
itakuwa haina ukweli ambao unaweza kuthibiti, basi washiriki katika mazungumzo
wataikataa na kutoiamini kuwa ya kweli. Hivyo basi, ni lazima proposisheni
ithibitiwe katika misingi ya kweli au uongo.
Kwa mfano:  ‘Nchi ya
Kenya ni huru.’
Proposisheni katika
kauli hii itakubalika kwa sababu ni jambo lililo wazi na kila mtu anafahamu
kuwa ni nchi yetu ilijinyakulia uhuru na kujikomboa kutoka kwa utawala wa
wakoloni
Larson (1984:89 -197),
anasema kuwa proposisheni ni mkusanyiko wa dhana katika kundi la watu ambalo
huwasiliana. Hivi anamaanisha kuwa Proposisheni hutegemea uhusiano uliopo baina
ya dhana zilizomo.
Kwa mfano:  John,
Peter, alimpiga.
Kama John ndiye
aliyetenda kitendo cha kumpiga Peter, basi proposisheni itakuwa: John alimpiga Peter. Vivyo hivyo, Kama
Peter ndiye aliyetenda kitendo cha kumpiga John, basi proposisheni itakuwa: Peter alimpiga John. Muundo wa
semantiki katika proposisheni waweza kuonyeshwa kwa njia zifuatazo
tunazoziangazia hapa chini.
Kwa mfano: Proposisheni
katika
1) Mtenda -.John … kitendo : kumpiga… mwathiriwa :
Peter
2) Mtenda : Peter … kitendo : kumpiga … mwathiriwa :
Joh
M fuatano wa maneno
katika sarufi utabainisha ni nani aliyempiga mwingine. Proposisheni yaweza
kuzua maana kadha.
Kwa mfano:
1) John aiimpiga Peter.
2) Peter alipigwa na
John.
3) Kupigwa kwa Peter
kulifanywa na John.
4) Peter ndiye alipigwa
na John.
5) John ambaye aiimpiga
Peter.
Kuna proposisheni za
matukio ambazo hubainishwa kwa dhana ambazo huwakilishwa na maneno tofauti.
Kama vile:
[Image: SAM_1544.JPG]
Sentensi hiyo hapo juu
kwanza itachanganuliwa kwa kutambua dhana ambazo huwakilishwa na maneno
tofauti. Kisha, sentensi hii ya kisarufi kuelezwa kama proposisheni ambapo
matukio yatakuwa msingi wa proposisheni hizo. Hivyo basi, matukio hayo
yatakuwa; kuharibu na kupanga.
Proposisheni zitakuwa: Mtu aliharibu mji
                                       Mtu
alipanga vyema.
Proposisheni huelezwa
kwa kujumlisha wahusika. Nomino Mtu
imetumika katika proposisheni hizi kuwakilisha mtenda ambaye alitenda kitendo.
Kwa mfano:  “John
alikataa ahadi ya Peter.’
Matukio basi ni kukataa na ahadi kisha Wahusika ni John
na Peter.
Hivyo basi, John
alikataa naye Peter alikuwa ameahidi kufanya kitu fulani na Peter aliahidi
kabla ya John kukataa. Hatimaye tunafahamu kuwa tukio la kuahidi lilifanyika
kabla ya tukio la kukataa.
Proposisheni ndicho
kitengo kidogo zaidi katika mawasiliano. Dhana moja hutokea pamoja na dhana
zingine ili kuwepo na mawasiliano yenye maana. Kila tukio huwakilisha proposisheni.
Kwa mfano: “Joy aliruka ukuta,
alikimbia na kutumbukia ndani ya ziwa’.
Sentensi hizi zina
proposisheni tatu ambazo ni:
1) Joy aliruka ukuta.
2)
Joy alikimbia.
3)
Joy alitumbukia ziwani.
Matini chanzi katika
lugha yoyote yaweza kuwa proposisheni. Kwa mfano:
1) Lugha chanzi: Kutotii husababisha kuteseka sana.
      Proposisheni: Mtu hukosa kutii.
                              Mtu huteseka.
2) Lugha chanzi: Sifa hiyo ilipokelewa vyema na Maria.
     Proposisheni: Mtu alimsifu Maria.
                           Maria aliitikia vyema.
3) Lugha chanzi: Watu wanaofikiria kuwania kiti cha Urais,
wataanzisha kampeni zao hivi
                               karibuni.
Proposisheni: Kuna watu wanaolifikiria tendo.
                       Wanataka kuwa Rais.
                      Watafanya kampeni hivi karibuni.
Tukio laweza kuwa; tendo, tajriba au mfanyiko.
Kwa mfano:  Tendo:
Wavulana walikimbia.
                                  Paul alikula.
                       Tajriba: Maria
alisikiaJilimbi.
                                     John aliona ng ‘ombe.
                     Mfanyiko: Barafu iliyeyuka.
                                        Paka alikufa.
Kuna proposisheni za
hali ambazo kitu au matokeo ndio msingi wake. Proposisheni ya hali huwa na
sehemu mbili kuu: Sehemu hizo ni mada
na maoni. Tukianza na mada, hii ni dhana itakayozungumziwa,
ilhali maoni yahusu kitu au matokeo katika kueleza mada na uhusiano katika hali
yake.
Kwa mfano:  ‘Kitabu
ni cha Peter.’
Mada ni kitabu na chahusishwa na dhana Peter kwa uhusiano wa kuwa Peter anakimiliki kitabu kile. Kwa mintarafu hii Peter ndiye mwenye kitabu.
Proposisheni za hali huelezwa
kwa kitenzi cha kuwa ni. Kama vile:
Proposisheni ya hali;
Maelezo;
Gari …umiliki…
mimi
gari
ni langu.
Mbwa
…jin a … fido                                            Jina
la mbwa ni fido.
Msimamizi
…kitambulisho… Bwana John       Msimamizi
ni Bwana John.
John
…mahali …nyumba                                  John yumo
nyumbani.
John
.. maelezo…mkubwa                               John ndiye mkubwa.
Maana ya proposisheni
yaweza kuwa katika matumizi. Mzungumzaji anaweza kuuliza swali, kutoa arifa au
kuamrisha. Proposisheni huwa ni moja lakini matumizi tofauti.
Kwa mfano:
Maana
clekezi: John …
mtenda … aliupiga .. mwathiriwa…mpira
               Arifa:
John alipiga mpira.
              Swali: Je, John alipiga
mpira?.
             Amri: John, piga mpira!
Maana elekezi
haibadiliki lakini matumizi huwa ni tofauti katika kila proposisheni. Matumizi
hayo yapo katika proposisheni za matukio na vilevile katika proposisheni za
hali, ambayo hujulikana kama misukumo ya kiilokusheni katika proposisheni.
Sentensi sahihi, mfuatano wa maneno na uakifishaji ni mambo ambayo huonyesha msukumo
wa kiilokusheni katika proposisheni. Mara nyingi kiimbo huonyesha msukumo wa
kiilokusheni katika mazungumzo. Kwa mfano:
1) Proposisheni ya hali
ambayo inaamrisha: Uwe hapa karibu!
2) Proposisheni ya hali
ambayo yauliza: Je, Maria ni dadake?
3) Proposisheni ya hali
ambayo yaarifu: Mbwa yumo katika chumba
chake.
4) Proposisheni ya
tukio ambayo yauliza swali katika kufanyika: Je, maziwa yaliganda?
5) Proposisheni ya
tukio ambayo yaonyesha tendo la kuamrisha: Wewe,
kimbia haraka!
6) Proposisheni ya
tukio ambayo yatoa arifa katika tajriba: Tulisikia
sauti.
Msukumo wa kiilokusheni
waweza kuoneshwa kwa mfuatano wa maneno, viambishi au  maneno na huibuka hasa kupitia kwa dhamira.
Matumizi ya proposisheni ni muhimu katika kuleta maana kwa sababu mtu huenda
asifahamu maana iliyokusudiwa na msemaji.
Kwa mfano:
Tukio
– kula, mtenda – chui, mwathiriwa – msafiri.
Katika mfano; maana
haiwezi kueleweka ila msemaji afafanue lile jambo analolitamka kuwa sentensi
yenyewe ni Arifa: Kama vile; Kauli: ”Chui alimla msafiri’ au ni sentensi ya
kutaka kuhakikishiwa jambo: Kama vile; Swali:
‘Je, chui alimla msafiri. Jinsi
msemaji anavyosema jambo huchangia katika kuelewa maana. Kuna wakati ambapo
msemaji hutaja msukumo wa kiilokushcni.
Kwa mfano:  Nenda
– Nakuamrisha uende!…Amri.
                     Alikwenda – Nasema kuwa
alikwenda: Arifa.
                    Kwa nini alikwenda? –Nauliza
ni kwa nini alikwenda?: Swali.
Arifa hukusudia kumpa
msikilizaji ujumbe. Swali hukusudia kumpa msikilizaji ujumbe kutoka kwa
msemaji, ilhali amri hukusudia kutoa sheria itakayofuatwa na msikilizaji. Kama
vile: Nakuamrisha, nasema na nauliza ni proposisheni tendaji kwa sababu huonesha kitendo
kinachofanyika, yaani ni maana iliyopo katika proposisheni, ili mawasiliano
yaweze kufaulu.
Maana ya proposisheini
hujumlisha maana kadiri ya vitendo katika kishazi.
Kwa mfano: : “Jengo refu ambalo ni adhimu lilianguka”.
Yadhihirisha proposisheni kuwa:
1) Jengo ni refu.
2)
Jengo ni adhimu.
3)
Jengo lilianguka.
Katika Kiswahili, kila
mojawapo ya kauli hizi zifuatazo ni proposisheni.
Kwa mfano:
                     ‘Alex alikula ndizi.’
                    ‘Ndizi ililiwa na Alex.’
                     ‘Je, Alex, alikula ndizi?’
Matamshi yaliyo katika
mfano hapo juu, yaweza kuchanganuliwa kuwa na kiarifu kinachotaja kundi au hali
na mijadala kadha na wahusika katika tukio au hali fulani. Shughuli ni ya kula.
Mtenda ni Alex. Mtcndwa ni ndizi
Proposisheni ya
uhusiano huzua maana ya umaanisho kati ya proposisheni mbili au makundi ya
proposisheni ambayo yahusiana katika mwingiliano wa kiproposisheni ulipo katika
kauli. Huleta uamuzi na mshikamano mkubwa kuhusu yaliyozugumzwa.
Kwa mfano: “Nina njaa. Twende Westlands”. Kauli hii
ina proposisheni kuwa:
1) Msemaji anahisi njaa.
2)
Msemaji anaonelea wacnde Westlands wapate chakula.
Uhuasiano wa
proposisheni hizi mbili ni kuwa kuna suluhisho la njaa na jinsi ya kusuluhisha.
‘Kwenda kwetu Westlands‘ ni sehemu ya
suluhisho la tatizo langu kuwa ‘naona
njaa’
Leech (1974:18-23),
anasema kuwa hisia za mtu binafsi huwepo kama zinazomhusu mtu anayepokea ujumbe
au kuhusu kitu fulani zitabainika wazi. Maana hisivu yaweza kuibushwa na
proposisheni.
Kwa mfano:: “Samahani kwa kuwakatiza mazungumzo yenu
lakini, ni vyema kama mngepunguza sauti zenu“.
Msemaji wa kauli hii
alikuwa ana hasira kwa sababu ya kelele kutoka kwao, kisha alijaribu kuwa mpole
katika kuwaambia kuwa sauti zao za juu hazimfurahishi kamwe. Vilevile, proposisheni
yaweza kuzua maana katika dhamira. Jinsi mzungumzaji anavyoupanga ujumbe wake
katika mpangilio wake wa maneno na kusisitiza jambo.
 Kwa mfano: 2 .19: (A)
1) ‘Bi Smith ali/adhili
tuzo la kwanza
2) ‘Tuzo la kwanza
lilifadhiliwa na Bi. Smith’
Sentensi ya kwanza ni
katika kauli tendi ilhali sentensi ya pili ni katika kauli tendwa.
Kwa mfano: 2.20: (B)
1)
‘Ndugu yangu amemiliki duka lililo kubwa zaidi mjini Nairobi’
2)
‘Duka lililo kubwa zaidi katika mji wa Nairobi limemilikiwa na ndugu yangu’
Maana ni tofauti
kulingana na kauli zilizotumika, kulingana na mpangilio wa maneno na msisitizo.
Mfano; (A), sentensi ya kwanza ina proposisheni kuwa Bi.Smith ni mtu mabaye ni
muhimu sana ili ufadhili wa tuzo la kwanza uwepo, sentensi ya pili ina
proposisheni kuwa tuzo la kwanza ni lenye umuhimu na sio lazima lifadhiliwe na
Bi. Smith, mbali pia mtu mwingine yeyote anaweza kufadhili. Mfano; (B),
sentensi ya kwanza ina proposisheni kuwa ni ndugu yangu aliye na uwezo wa
kumiliki lile duka kubwa zaidi mjini Nairobi, ilhali katika sentensi ya pili
mtu mwingine yeyote isipokuwa ndugu yangu hana uwezo wa kumiliki duka kubwa
zaidi mjini Nairobi.





MAREJELEO
Abraham, S.
(1996). A Theory o f Structural Semantics’. Mouton and Company Publishers.
Akmajian, A. na
Wenzake. (2004) Linguistics. An lntrodution to Language and Communication. Fifth
Edition: MIT Press, Cambridge.
Atichi, A.R. (2004) The
Semantic Distinctiveness of Kenyan English: UON. Unpublished MA
Thesis.
Atoh, F.O. (2001)
Semantics Analysis of Dholuo Nowns: The Semantics Field Approach. UON.
Unpublished MA Thesis.
Blass, R. (1990)
Relevance Relations in Discource. A Study in Special Reference to Sissala:
Cambidge University
Press.
Brown, G. na Yule, G.
(1983) Discource Analysis: Cambridge University Press.
Bussman, H. (1996)
Route ledge Dictionary o f Language and Linguistics: International
Thompson Publishing
Company.
Cambridge (2008)
Cambridge Advanced Learners Dictionary. Cambridge University.
Carston, R. (2002)
Thoughts and Utterances. The Pragmatics of Explicit Communication. MA:
Blackwell Publishers
Ltd.
Comford, F. M. (1957)
Platos Theory o f Knowledge: Routeledge and Kegan Paul Ltd.
Crystal, D. (2003) A
Dictionary o f Linguistics and Phonetics. Fifth Edition. Oxford: Blackwell
Publishers.
Falsod, R. W. (2002) An
lntrodution to Language and Linguistics. Cambridge University Press.
Fleming, (1998) Google
Search. Powered by The Ultimate Programming Weblog. Sil
lntematinal: http://
worldnet Princeton. Edu/Pert/Webwn.
Fodor, J. D. (1997)
Semantics: Theories o f Meaning in Generative in Generative Grammar:
Harper and Row ,
Publishers.
Fretheim, A. (2000)
Pragmatic Markers and Propositional Attitude: John Benjamin Publishing
Company.
Green, G. M (1996)
Pragmatics and Natural Language Understanding. Second Edition:
Lawrence Erlbaum
Associates Publishers.
Greenbaum, S. na
Wenzake. (1985) A comprehensive Grammar o f English Language: Longman
Group UK Ltd.
Griffin, E. M (1991) A
First look at Communication Theory. Wheaton College: Me Graw- Hill,
Inc. Company.
Hofmann, T. R. (1993)
Realms o f Meaning: An Introduction to Semantics: Longman Group UK
Ltd.
Ifantidou, E. (2001)
Evidentials and Relevance. Volume 86: John Benjamin Publishing
Company.
Kamau, S. K. (2008) An
Analysis o f Truth Conditions in Pragmatics: Relevance Theory
A p p r o a c h . UON.
Unpublished MA Thesis.
Kasher, A. (1998)
Pragmatics. Critical Concepts. Volume V: Communication, Interaction and
Discourse: Routeledge
Publishers.
Katie, W. (2001) A
Dictionary o f Stylistics: Longman Group UK Ltd.
Katz, J.J. (1977)
Propositional Structure and Illocutionary Force. A Study of the contribution of
Sentence meaning and
Speech Acts: The Harvest Press.
Kempson, R. M. (1975)
Pressuposition and The Delimination o f Semantics: Cambridge
University Press.
Larson, M. L. (1984)
Meaning-Based Translation: A Guide to Cross-Language Eqivalence:
University Press of
America, Inc.
Leech, G. (1974)
Semantics: Penguin Books Limited.
Leech, G. N. (1971)
Towards a Semantic Description o f English: Longman Group Ltd.
Linsky, L. (1952)
Semantics and the Philosophy o f Language: University of Illinois Press.
Longmans (1968)
Longmans English Larousse: Longmans, Green and Co. Ltd.
Munga, C. M. (2009)
Sence Relations in Gikuyu: A Lexical Pragmatics Approach. UON
Unpublished MA Thesis.
Ndug’u, M. N. (2009)
Mada na Fokasi katika Kiswahili: Mtazamo wa Muundo wa Taarifa.
UON. Unpublished MA
Thesis.
Ogola, C. A. (2006) A
Pragmatic Analysis of Intercultural Communication Failures. UON,
Unpublished MA Thesis.
Palmer, F. R. (2006) An
Introduction to Language and Linguistics: Cambridge University Press.
Rouchota, V, na Jucker,
H. (1998) Current Issues in Relevance Theory: John Benjamin
Publishing Company.
Saeed, J. L. (2003)
Semantics. Second Edition: Blackwell Publishing Ltd.
Schroeder, H. (2005) Do
we Speak the same Language? A cognitive Pragmatic Explanation of
Cultural
Misunderstanding. In Across Borders: Benefiting from Cultural Differences.
Conference Proceedings.
17^-18th March: 2005.
Sperber, D na Wilson,
D. (1995) Communication and Cognition, 2nd Edition: Blackwell
Publishers.
Sperber, D na Wilson,
D. (2004) A Handout on Relevance Theory (1985-2002): Blackwell
Publishers.
Tuki (1990). Kamusi ya
Isimu na Lugha. Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili: Educational
Publishers and
Distributors Ltd.

Tuki (2006)
English-Swahili Dictionary. Third Edition: Book Printing Services Ltd.
Chanzo>>>>>>>>
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)