MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'BAATHI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO 'BAATHI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'BAATHI'

Neno *baathi* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Bath.i* [Kitenzi elekezi] chenye maana ya 'rejesha uhai wa mtu au kiumbe aliyekuwa amekufa; fufua.

*Kisawe* : huisha.

*Minyambuliko:*
baathia, baathika, baathiwa, baathisha.

2. *Bath.i* [Kitenzi elekezi] chenye maana ya -pa mtu uwezo na mamlaka ya kwenda kufanya kazi au jambo kwa niaba ya mtu mwengine.

3. *Nomino [Ngeli:-a/-wa]* yenye maana ya kiongozi wa dini; mtume. 

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *baathi* limechukuliwa kutoka neno la Kiarabu  *'ba-aath*( *soma: ba-athun/ba-athan/ba-athin بعث )* ambalo ni nomino ya Kiarabu yenye maana zifuatazo:

1. Kufufua, kufufuliwa, kuhuisha *yawmul ba-athi يوم البعث* siku ya Kiyama.

2. Mtume, mitume.

3. Kumuamsha mtu toka usingizini.

4. Kikundi cha askari wapiganaji; jeshi.

5. Mtu asiyeweza kupata usingizi kutokana mazonge aliyokuwa nayo.

6. Furaha, utulivu.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *'ba-athun بعث* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *baathi* lilichukua baadhi ya maana kutoka Kiarabu na kuziacha zingine.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)