MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'ARIDHIO'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO 'ARIDHIO'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'ARIDHIO'

Neno *aridhio* katika lugha Kiswahili ni *Nomino* inayotokana na kitenzi elekezi *aridh.i* chenye maana zifuatazo:

1. Ingilia mtu katika jambo analolisimamia.

*Mnyumbuliko: aridhia, aridhika  aridhiwa, aridhiana, aridhisha.*

*Visawe: kera, sumbua, udhi, ghasi.*

2. Orodhesha vitu; weka vitu kwa mpangilio kuanzia kimoja hadi kingine.

3. Soma kwa kukariri bila ya kuangalia maandishi mbele ya mwalimu aghalabu Qur'aan Tukufu.

4. Kitenzi elekezi *aridhi.a* fafanua jambo fulani.

*Visawe: arifu, juvya, fahamisha, julisha.*

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *aridhi* linafanana na kitenzi cha Kiarabu  *aaridh عارض* kitenzi cha kuamrisha/kutaka tendo kutendeka, kinachotokana na kitenzi cha msingi cha Kiarabu *aaradhwa  عارض* chenye maana zifuatazo:

1.  Ingilia mtu kati kwa kuhoji au kupinga anachokisema.

2. Epuka jambo fulani.

3. Yapinge maandishi kwa kutoa maandishi dhidi yake.

4. Tembea pembezoni mwa njia.

5. Dhihirisha/weka wazi jambo/taarifa fulani; soma kwa kukariri bila ya kuangalia maandishi.

6. Onesha kitu fulani kwa wengine.

Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiswahili *aridhio* halina mfano wake katika Kiarabu na *si neno la Kiarabu* bali limebuniwa kutokana na kitenzi cha Kiarabu *aaridhi عارض* kinachotokana na kitenzi cha msingi cha Kiarabu *aaradha عارض* kilichofafanuliwa hapo juu.

Katika Kiarabu tendo-jina *masdar  مصدر* la kitenzi cha Kiarabu  *aaradha* ni *muaradha معارضة* lenye maana ya kuweka wazi taarifa; *onesho* .

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)