02-27-2022, 08:33 AM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'ARAFA'
Neno *arafa* katika lugha Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. *Nomino [Ngeli: i-/i-]* siku ya tisa ya mwezi Dhulhija (Mfungo Tatu) katika Kalenda ya Kiislamu - Hijiriyyah.
2. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* ujumbe mfupi wa maandishi unaotumwa na kupokewa katika simu ya mkononi.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *arafa*( *soma: arafatu/arafata عرفة)* ni nomino ya Kiarabu, wingi wake ni *arafaat عرفات* yenye maana zifuatazo:
1. Mahali penye mchanga paliponyanyuka.
2. Kizuizi kati ya vitu viwili.
3. Tendo-jina la Kitenzi cha Kiarabu *arafa/ya-arifu عرف/يعرف* chenye maana ya : -metafuta habari, -meuliza.
4. Siku ya tisa ya mwezi Dhul-Hijjah (Mfungo Tatu) katika Kalenda ya Kiislamu - Hijiriyyah.
5. Jina la mlima maarufu karibu na mji wa Makkah, nchini Saudi Arabia.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *arafatu/arafata/عرفة)* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *arafa* lilichukua kutoka lugha ya asili - Kiarabu maana ya *siku ya tisa ya mwezi Dhul-Hijjah (Mfungo Tatu)* na kubeba maana mpya: *ujumbe mfupi wa maandishi inaotumwa na kupokewa katika simu ya mkononi.*
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *arafa* katika lugha Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. *Nomino [Ngeli: i-/i-]* siku ya tisa ya mwezi Dhulhija (Mfungo Tatu) katika Kalenda ya Kiislamu - Hijiriyyah.
2. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* ujumbe mfupi wa maandishi unaotumwa na kupokewa katika simu ya mkononi.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *arafa*( *soma: arafatu/arafata عرفة)* ni nomino ya Kiarabu, wingi wake ni *arafaat عرفات* yenye maana zifuatazo:
1. Mahali penye mchanga paliponyanyuka.
2. Kizuizi kati ya vitu viwili.
3. Tendo-jina la Kitenzi cha Kiarabu *arafa/ya-arifu عرف/يعرف* chenye maana ya : -metafuta habari, -meuliza.
4. Siku ya tisa ya mwezi Dhul-Hijjah (Mfungo Tatu) katika Kalenda ya Kiislamu - Hijiriyyah.
5. Jina la mlima maarufu karibu na mji wa Makkah, nchini Saudi Arabia.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *arafatu/arafata/عرفة)* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *arafa* lilichukua kutoka lugha ya asili - Kiarabu maana ya *siku ya tisa ya mwezi Dhul-Hijjah (Mfungo Tatu)* na kubeba maana mpya: *ujumbe mfupi wa maandishi inaotumwa na kupokewa katika simu ya mkononi.*
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda