MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA MANENO 'AJILA' NA 'AJILANI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA MANENO 'AJILA' NA 'AJILANI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO 'AJILA' NA 'AJILANI'

Neno *ajila* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* hali ya kufanya kitu kwa haraka; fanya jambo himahima.

2. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* utendaji jambo bila kukawia.

3. *Nomino [Ngeli: i-/zi-]* umuhimu.

Katika lugha ya Kiarabu, neno *ajila* limekopwa kutoka nomino ya Kiarabu  *aajilun/aajilan/aajilin عاجل*  yenye maana zifuatazo:

1. Mwenye kufanya haraka.

2. Hali ya kutokea jambo kwa haraka.

3. Jina lingine la dunia; mahali pa kupita kwa haraka.

Neno *ajilani* katika lugha ya Kiswahili ni kielezi chenye maana ya bila kukawia, mara moja, hivi sasa.

Katika lugha ya Kiarabu, neno *ajilani* limekopwa kutoka nomino ya Kiarabu  *ajlaanu/ajlaana  عجلان*  yenye maana zifuatazo:

1. Mwenye kufanya mambo yake haraka haraka.

2. Mwenye kutembea kwa haraka kuwahi shughuli zake.

Kinachodhihiri ni kuwa maneno *ajila* na *ajilani* yalipokopwa kutoka Kiarabu hayakuacha maana zake katika lugha ya asili - Kiarabu isipokuwa Waswahili waliliweka neno *ajilani*  katika kategori mpya - *kielezi*  na kulipa neno *ajila* maana mpya - umuhimu

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)