01-03-2022, 08:33 AM
SHAIRI: YUPO BINTI ANIGHURI
*********
Ninahisi vungevunge,
miye mwana Mnyarwanda,
lakini wacha nitunge,
beti zifikie kenda.
*****
Jama nawafahamisha,
yupo binti anighuli,
hili limenighumisha,
nakosa hata kauli.
*****
Kimwana aso na tenge,
uno badii jamali,
tenzi hili nilitunge,
liwe tuzo la kimwali.
*****
Uzuri we mdawari,
kidege Mtanzania,
kwake nimedadahari,
ni aje ‘tanifikia?
*****
Ipo siku alikuja,
anapaa ja tuyuri,
kumpokea nikaja,
akamficha khantwiri.
*****
Ni Purinsezi makini,
msanii mshairi,
ni mtunzi na aghani,
anikosha ninakiri.
*****
Nti yetu iko powa,
naja mwa hini qamari,
siyo kwa kuogopewa,
nikute uko tayari.
*****
Yeo ‘wache kupulika,
longo wanakuambia,
kwetu Rwanda ukifika,
uwe wangu Malikia.
*****
Beti kenda ni’shafika,
n’kushukuru Rahmani,
n’najisikia kuchoka,
kalamu natuwa chini.
*******
Rwaka rwa Kagarama
Mshairi Mnyarwanda.
*********
Ninahisi vungevunge,
miye mwana Mnyarwanda,
lakini wacha nitunge,
beti zifikie kenda.
*****
Jama nawafahamisha,
yupo binti anighuli,
hili limenighumisha,
nakosa hata kauli.
*****
Kimwana aso na tenge,
uno badii jamali,
tenzi hili nilitunge,
liwe tuzo la kimwali.
*****
Uzuri we mdawari,
kidege Mtanzania,
kwake nimedadahari,
ni aje ‘tanifikia?
*****
Ipo siku alikuja,
anapaa ja tuyuri,
kumpokea nikaja,
akamficha khantwiri.
*****
Ni Purinsezi makini,
msanii mshairi,
ni mtunzi na aghani,
anikosha ninakiri.
*****
Nti yetu iko powa,
naja mwa hini qamari,
siyo kwa kuogopewa,
nikute uko tayari.
*****
Yeo ‘wache kupulika,
longo wanakuambia,
kwetu Rwanda ukifika,
uwe wangu Malikia.
*****
Beti kenda ni’shafika,
n’kushukuru Rahmani,
n’najisikia kuchoka,
kalamu natuwa chini.
*******
Rwaka rwa Kagarama
Mshairi Mnyarwanda.
Mwl Maeda