MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'HEKIMA'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO 'HEKIMA'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO ' HEKIMA'

Neno *hekima* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo:

1. Maarifa, uwezo wa akili alionao mtu unaomuwezesha kufikiri kwa kina na kutoa uamuzi unaokubalika; busara.

2. Uwezo wa akili katika kutoa maamuzi kutokana na tajiriba na uzoefu wa muda mrefu.

3.  Akili inayomuwezesha mtu kufikiri na kuweza kutoa uamuzi unaofaa.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *hekima* ( soma: *hikmatun/hikmatan/hikmatin* *حكمة* ) lina maana zifuatazo:

1. Uamuzi, *masdar* *مصدر* *tendo-jina* kutokana na *kitenzi* cha Kiarabu *hakama* *حكم* (ameamua/ametoa uamuzi).

2. Maarifa ya kujua kilicho bora zaidi kwa kutumia njia bora za kielimu; falsafa.

3. Taaluma ya kujua uhalisia wa mambo.

4. Uwezo wa kudhibiti nafsi na mihemko wakati wa kupandwa na ghadhabu/hasira.

5. Haki, uadilifu.

6. Sababu ya kutokea jambo fulani.

7. Maneno machache yenye maana kubwa na pana.

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili ( *hikmatun* *حكمة*  ) lilipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa likawa *hekima* maana yake katika lugha yake ya asili - Kiarabu - haikubadilika ingawa imejifunga katika uwezo wa akili wa kufikiri na kutoa uamuzi unaofaa.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)