12-15-2021, 08:22 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO ' HEKIMA'
Neno *hekima* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo:
1. Maarifa, uwezo wa akili alionao mtu unaomuwezesha kufikiri kwa kina na kutoa uamuzi unaokubalika; busara.
2. Uwezo wa akili katika kutoa maamuzi kutokana na tajiriba na uzoefu wa muda mrefu.
3. Akili inayomuwezesha mtu kufikiri na kuweza kutoa uamuzi unaofaa.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *hekima* ( soma: *hikmatun/hikmatan/hikmatin* *حكمة* ) lina maana zifuatazo:
1. Uamuzi, *masdar* *مصدر* *tendo-jina* kutokana na *kitenzi* cha Kiarabu *hakama* *حكم* (ameamua/ametoa uamuzi).
2. Maarifa ya kujua kilicho bora zaidi kwa kutumia njia bora za kielimu; falsafa.
3. Taaluma ya kujua uhalisia wa mambo.
4. Uwezo wa kudhibiti nafsi na mihemko wakati wa kupandwa na ghadhabu/hasira.
5. Haki, uadilifu.
6. Sababu ya kutokea jambo fulani.
7. Maneno machache yenye maana kubwa na pana.
Kinachodhihiri ni kuwa neno hili ( *hikmatun* *حكمة* ) lilipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa likawa *hekima* maana yake katika lugha yake ya asili - Kiarabu - haikubadilika ingawa imejifunga katika uwezo wa akili wa kufikiri na kutoa uamuzi unaofaa.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *hekima* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo:
1. Maarifa, uwezo wa akili alionao mtu unaomuwezesha kufikiri kwa kina na kutoa uamuzi unaokubalika; busara.
2. Uwezo wa akili katika kutoa maamuzi kutokana na tajiriba na uzoefu wa muda mrefu.
3. Akili inayomuwezesha mtu kufikiri na kuweza kutoa uamuzi unaofaa.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *hekima* ( soma: *hikmatun/hikmatan/hikmatin* *حكمة* ) lina maana zifuatazo:
1. Uamuzi, *masdar* *مصدر* *tendo-jina* kutokana na *kitenzi* cha Kiarabu *hakama* *حكم* (ameamua/ametoa uamuzi).
2. Maarifa ya kujua kilicho bora zaidi kwa kutumia njia bora za kielimu; falsafa.
3. Taaluma ya kujua uhalisia wa mambo.
4. Uwezo wa kudhibiti nafsi na mihemko wakati wa kupandwa na ghadhabu/hasira.
5. Haki, uadilifu.
6. Sababu ya kutokea jambo fulani.
7. Maneno machache yenye maana kubwa na pana.
Kinachodhihiri ni kuwa neno hili ( *hikmatun* *حكمة* ) lilipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa likawa *hekima* maana yake katika lugha yake ya asili - Kiarabu - haikubadilika ingawa imejifunga katika uwezo wa akili wa kufikiri na kutoa uamuzi unaofaa.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda