MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
HII NDIO MAANA YA “UTAKIONA CHA MTEMA KUNI!”

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
HII NDIO MAANA YA “UTAKIONA CHA MTEMA KUNI!”
#1
Nimeambiwa msemo huu wahenga waliupata katika kisa kimoja cha zama za kale.
Wanasema kulikuwa na msitu jirani na kijiji, ndani ya msitu kulikuwa na miti mingi sana. Ilitokea kuwa katika msitu ule, kulikuwa na miti inapishana sana kwa uzuri, na kati yao ulikuwepo ule ambao ni mzuri sana!
Mtema kuni (Mtemakuni maana yake ni Mkatakuni) alienda katika msitu ule katika shughuli zake za kila siku za kukata kuni!
Alipofika jirani na ule mti mzuri, huku akiwa na shoka mkononi, ule mti zuri sana ulikuwa jirani na mti mbaya sana!
Katika hali ya kufedhehesha (kwa nyodo na maringo) ule mti mzuri sana ukawa unamcheka na kumdhihaki ule mti mbaya, kwamba hauna mvuto na ndio maana kuanzia mbali kabisa, Mtemakuni amaonyesha kuvutiwa na (yeye) Mti mzuri! Huku Mtemakuni akizidi kuusogelea mti mzuri, mti mbaya sana ukajifariji kwa kumwambia mti mzuri basi subiri “utakiona cha mtema kuni”
Kilichofuata ni kweli, Mtema kuni aliukata na kuucharanga Mti mzuri sana kiasi cha kuugeuza kuni za kumfaa kubeba na kuondoka nazo, huku akiuacha ule mti mbaya salama salmini pale msituni!
Yakawa ni majuto kwa Mti mzuri na furaha kwa Mti mbaya!
Hivo ndio nilivyopokea kisa cha “mtema kuni”
UJUMBE WAKE KWA JAMII
[Image: 1f447_1f3fd.png]??
1. Mliobarikiwa uzuri punguzeni maringo na nyodo!
2. Usijutie ubaya wa maumbile yako, Mungu ana maana kubwa sana kukuumba hivyo!
3. Shukuru Mungu kwa kila ulichonacho!
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)