MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI: “JENEZA LA AJABU ” **SEHEMU YA 04**

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI: “JENEZA LA AJABU ” **SEHEMU YA 04**
#1
SIMULIZI: “JENEZA
LA AJABU “
**SEHEMU YA 04**
Nyumbani kwa kina
Njoshi;
Jua likiwa tayali
linazama, huku sauti za ndege zikipungua na kuufanya mji wa Mwamutapa kuwa
kimya.Ukimya huo unatokea pia katika nyumba ya kina Njoshi, ukimya unatawala
tofauti na siku zote, kwani familia ilibakiwa na mtu mmoja tu,ambaye ni mama
yake Njoshi  huku mwanae akiwa hajarudi
kutoka kwa mfalme. Akiwa ameketi barazani, nje ya kibanda chao cha udongo,
kilichoezekwa kwa nyasi, aliendelea kupunga upepo huku akiwa na huzuni sana,
“Siamini,hatimaye
leo hii nimebaki peke yangu, sina cha kufanya ndio tayali imeshatokea ……,eeeh
mizimu ya babu zangu mlindeni mwanangu ” ,mama Njoshi aliongea peke yake
kwa huzuni huku akinyanyuka sehemu aliyokuwa ameketi, na kisha kuelekea ndani
kulala, hakuwa na njinsi kwani aliona kuketi pale nje kulizidi kumuongezea
machungu.
Ikulu kwa mfalme;
Giza likiwa tayali limeshaingia huku,
ukimya ukiwa umetawala katika ngome ya mfalme. Kijana Njoshi anamfuta machozi
Grace, huku akiwa amemkumbatia,
“Usijali Grace,
naamini nitarudi salama ndani ya siku tatu “,Njoshi alimtoa hofu binti
mfalme, msichana aliyempenda sana, na aliamini atamuoa atakaporudi kutoka
katika msitu hatari wa majini, msitu ambao aliambiwa na mama yake hana budi
kwenda huko, kwani huko ndiko angeupata ufalme na ukombozi wa Mwamutapa.
“Sawa Njoshi,
nakuamini wewe ni shujaa, nakuombea kwa mizimu yetu, urudi ukiwa mzima
“,Grace aliongea kwa huzuni huku akitoka mikononi mwa Njoshi aliyekuwa
amemkumbatia, na kumruhusu kuianza safari yake haraka sana, kwani alitakiwa
kuondoka usiku huo. Na bila kupoteza muda, kijana shupavu na hodari, kijana
pekee aliyeogopwa na askari pamoja na mfalme Mutapa kutokana na uhodari wake wa
kupambana, anatoka katika ngome ya mfalme iliyojengwa kwa ukuta mrefu, huku
wafanyakazi pamoja na familia nzima ya mfalme wakimtazama na kumtakia kila
laheri katika safari hiyo, bila kutambua kuwa Njoshi alikuwa na malengo
yaliyompeleka msituni huku swala la kuchukua jeneza la ajabu, likiwa la ziada
tu.
Mwamutapa
Kijana ambaye alikuwa ni rafiki yake
Njoshi, urafiki ambao ulitokana na kijana huyo kuokolewa katika kipigo kizito
kutoka kwa askari wa mfalme, mara tu alipofanya kazi asubuhi mpaka jioni katika
shamba la mfalme, na pale alipojaribu kudai haki yake, askari wale walimnyima
pesa, jambo ambalo kijana yule alishindwa kulivumilia, alijikuta akilusha
ngumi, na kuambulia kipigo kikali kwani asingeweza kuwashinda askari zaidi ya
kumi, huku yeye akiwa mmoja tu, lakini bila kutegemea ghafla alishangaa, askari
wale wakipigwa mateke ya haraka haraka na kutimua mbio.
“mimi naitwa
Njoshi, na pole sana ndugu yangu, hawa ndio askari wetu, inatakiwa tuungane
kuitafuta haki “,kijana yule aliikumbuka sauti ya mtu aliyemsaidia kutoka
mikononi mwa askari wa mfalme, ikijitambulisha na kisha kumuomba waungane
katika harakati za ukombozi wa Mwamutapa. Na huo ndio ukawa mwanzo wa urafiki
wao, urafiki ambao umedumu kwa muda mrefu na wamekuwa kama ndugu sasa.
“Inabidi kesho
niende kwao nikamuone rafiki yangu, tangu jana sijaonana naye “,rafiki
yake Njoshi, aliyejulikana kwa jina la Ngesha, alizungumza peke yake huku
akijifunika shuka lake na kisha kuuchapa usingizi, bila kutambua kuwa muda huo
ambao yeye analala, rafiki yake yuko safarini bila kujali giza wala hatari
yoyote usiku huo, akielekea katika msitu wa majini, msitu ambao ulipatikana
umbali wa kilomita arobaini kutoka katika makazi ya watu wa Mwamutapa.
Msitu wa majini;
Tangu asubuhi tetemeko lilipotokea, na
malikia kutangaza hali ya hatari katika msitu, mitego ya kila aina iliweza
kutegwa katika kila njia ya kuingilia msituni, huku jeshi la msituni likiwa
tayali limeshika dhana mbalimbali za kivita ikiwemo mishale, na kuuzunguka
msitu wote.
“Aiweeeh jini
mweupe, kiongozi wa askari wangu wa msituni, adui wetu yuko njiani anakuja,
nakuomba jiandae kwa mapambano, uko huru kutumia nguvu za kichawi na kijini
ulizonazo “,malikia alimpatia taarifa mkuu wa jeshi lake la ulinzi
msituni, na haraka bila kupoteza muda alitoweka mbele ya uso wa malikia, kwenda
kutekeleza amli aliyopewa ya kudumisha ulinzi kila kona ya msitu, na kujiandaa
kwa ajili ya kulipiza kisasi.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)