MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 02

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 02
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU
SEHEMU YA 02
Kwakweli kwa Zamda usiku wa siku ile  ulikuwa ni usiku wa Yeye kujikuta kama ni mlinzi wa Nyumbani kwao.Kwasababu hata Usingizi kwake Kwakweli ulikwea mbali sana hata kubembelezeka haubembelezeki kabisa.Akawa anasema Hivi akiwa mda huo kitandani giza kote Yaani mda huo taa zimezimwa.
Ni Kweli Yaani nikiwaangalia wale mashoga zangu Kwakweli hadi wananitamanisha.Angalia huyo Kidawa anavaa saa kali vile nywele anaenda kunyoa hadi Raha Jamani.Huyo Mwantumu naye ndiyo usiseme Yaani namna anavyozitafuna hizo Hela za hao wanaume na kawapanga hadi Raha kwa akili tu.Yaani mtoto mdogo tu vile anawapanga wavulana namna ile.Duuu sijui Jamani na Mimi nijiunge na mawazo ya Hawa mashoga zangu Au mawazo ya mama.Kwanza Hawa ndiyo wakati wao haya mawazo ya mama yeye anaongea hivyo kwa vile ameshapita hiki kipindi cha usichana.Huu ndiyo Wakati wetu bana na sisi wasichana."Lakini anapoendelea kuyachuja maneno ya  Hao shoga zake Zamda Lakini na maneno ya mama yako yalimuijia masikioni mwake huku akiwa anavutia picha ya siku ile wakiwa wamekaa jikoni hapo. Zamda akaanza tena kusema hivi ".
Hapana..... Hapana..... Hapana lazima nifuatilie mawazo ya mama yangu.Kwasababu mama yangu Kwakweli Kwa namna alivyoongea siku ile,Kwakweli aliongea kwakuweza kunipatia faida Mimi Au ni kumpatia faida nani zaidi ya Mimi. Embu huu ushetani utoke humu kichwani mwangu kabisaaaaaaa. Sitaki cha mawazo ya Huyo Kidawa wala huyo Mwantumu. Kama ni ushoga bora tuuvunje na kuufutilia mbali kabisaaaaaaa. Wale siyo marafiki wazuri kabisaaaaaaa. Bora nife na umasikini wangu hivi hivi.Yaani nilivyo  mdogo hivi na nilivyo mlembwende hivi afu ndiyo nije nipate huo ugonjwa wa UKIMWI nitakuwa mgeni wa nani miyeeeeeeeeeeeee Jamani.Acha nibaki hivi hivi Bali si kuendelea kujiunga na lile Kundi. Yaani lile Kundi wala siyo kundi kabisa Lakusema kila mmoja wapo pale akupatie ushauri."Kwakweli usiku wa Zamda kwa siku ile ulikuwa ni usiku wa Yeye Kuwaza na kuwazua tu.Lakini baada ya kupita mda kidogo Hivi akawa tayari naye Usingizi  ukawa umeshampitia na akawa amelala Usingizi uliokuwa ni mzito kwelikweli".
kwakweli kwa usiku ule baada ya Zamda kupitiwa na Usingizi mkali kwelikweli kuna ndoto fulani ilimwijia. Ambapo ndoto Hiyo inaonesha kwamba Zamda yuko sehemu fulani hivi ambayo ni kama mtoni hivi.Eneo hilo nalo kuna watu wako hapo mojawapo wakiwa ni Shoga zake Zamda yaani Kidawa na Mwantumu. Lakini sehemu hiyo inaonesha kwamba Zamda amebeba mtoto ambapo inaonesha kabisa Zamda ameshakuwa vya kutosha haswaaaa.Anaonekana akiwa anamtoto mgongoni wa kike analia kwelikweli huku akawa anasema kwamba hivi
Daaaa Jamani hii ndiyo tabu ya kuwa na mtoto. Yaani wanasumbua kwelikweli."Baada ya Zamda kuzungumza namna hiyo Kidawa na Mwantumu wakiwa wanaonekana wako pembeni Hapo wakawa wamecheka kicheko cha moja kwa moja kilichofanya hadi yule Mtoto kuweza kunyamaza kimyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa baada ya kusikia sauti zile za shoga zake Zamda.Baada kucheka kwa sekunde kazaa wakaambatanisha na maneno kwaajili ya huyo rafiki yao kwakusema ".
Heheeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!..!!!.Mwanafunzi kapewa tunzo ya ufundishaji bora na Mwalimu kawekwa pembeni."Baada ya wote kuzungumza maneno Yale Zamda anaonekana ameshika ndoo ya kuchotea maji hadi akawa ameiachia na kubaki anawasikiliza hao shoga zake.Kisha Kidawa akawa anaendelea kuyatema hayo maneno kwa huyo Zamda".
Watu na degree zao za kuwa na wanaume wengi hawajapata watoto nashangaa wewe sijui uliweka style gani ikajipenyesha tu.Tulikuambia shoga yetu Lakini wewe ukajifanya pembe la tembo kumbe Hamna chochote. Sikiliza ya wahenga wewe.Ila ndiyo hivyo maji yakishamwagika hayazoleki."Ndoto ile ikawa inaendelea Zamda akawa na sura ya kihuzuni palepale kwa maneno ya huyo Kidawa anavyoyatoa Lakini wala huyo Kidawa hatishiwi na hiyo sura ya kihudhuni ya Zamda.Kidawa anasema".
Ulijifanya eti ooooo Mimi siwezichezewa na Kila mwanaume mwanaume. Mbona huyo mmoja kakuchezea na tayari kakupa mimba na mtoto Huyo. Tena huyo si mtoto wa pili."Hapo ndipo Zamda akashangaa kabisaaaaaaa huku akiwa anaongea kimoyomoyo akisema Hivi".
Hawa wanajuaje kwamba Mimi Nina watoto  wawili. Kwasababu hata Hiyo mimba ya kwanza tu sikuwahi kuja hapa.Kujifungua sijajifungulia hapa nyumbani kwetu Mimi nimejifungulia sehemu nyingine tu.wamejuaje Hawa."Kidawa akaendelea na maneno yake ya kumchambua Zamda".
Heheeeeeeeeeeeeeeeeee unashangaa nini Sasa Unajua kwamba hatuelewi kuhusiana na gazeti Lako. Hohoooooooooo umeula wa chuya Zamda Yaaani kama ulikuwa unajipa hayo mawazo yatafutie kifutio kikubwa kabisaaaaaaa uyafute Hayo mawazo.Watu tunajua kuanzia gazeti lilipoanzia hadi lilipoishia na hadi mda huu tuko na wewe hapa.Yaani gazeti Lako limesomeka Kweli Kweli kuliko hata ya magazeti mengine huku kwetu.Kwasababu wewe ulijifanya nyooonyoo mwisho wa siku wajanja wa mjini  wakakuonesha shooooshooo na hayo ndiyo matokeo ya shoooshooo zile za kujificha.Pole sana shoga Wetu."Mwantumu naye akaingilia baada ya kuona Kidawa kaishiwa na maneno ya kusema. Ilikuwa hivi ".
Ule uzuri wako uko wapi sasa. Angalia Sasa umeruka mkojo na kwenda kukanyaga mavi Kabisaaaaaaa. Duuuuuuuuuuuu wanuka Mbona. Angalia Sasa afadhali huyo jamaa hata angekuwa na uwezo wa kukuoa kumbe naye shombo tu.Yaani mwanamke ulikuwa unawagoganisha hao wanaume hapa mtaani kwelikweli enzi zako Lakini kwasasa hiyo ndiyo kwishiney kabisaaaaaaa.Yaani kila mwanaume alikuja na style yake ya kukutongoza na waliokuwa wakija walikuwa ni wajanja wa mjini watu na hela zao.Lakini wewe ukawa unajifanya unawapangua yaani unawawekea mgomo baridi tu.Sasa ule mgomo baridi dada sijui kwasasa tusemeje.Labda tusubiri tu kama wahenga walivyosema kwamba Ng'ombe hazeeki maini."Lakini kwa pembeni panaonekana pia kuna Bibi anaonekana naye yuko hapo anawasikiliza huyo Kidawa na Mwantumu wanavyombubujikia maneno ya nguoni kwelikweli. Bibi yule Kwakweli aliyavumilia maneno Yale Lakini ikabidi aingilie mada kwakusema Hivi".
Eeeeeeee tuuuuuuuuuuu "Akatema mate ikiashiria kwamba amechukizwa na maneno Yale.Akawa anasema Hivi."Nyiye watoto Nyiye kama wewe ni kuku usimcheke mwenzako akiwa anachinjwa Kwasababu na wewe utapita kwenye hicho hicho kisu.Yawezekana kwanza mchinjaji wa kuku wa kwanza tena alikuwa na roho nzuri. Lakini ikaja kwako ambaye ni kuku wa pili akaja mchinjaji ambaye ni Hana huruma katika Maisha yake.kwanza anaanza kukuchinja na Kisu kibutuuuuuu.Wajukuu zangu msitukane mamba kabla hamja vuka mto.Mnanisikia.....Hivi nyiye mnamtukana mkunga angali mu wazazi mwaja.Afadhali huyu mwenzenu anajua Ana watoto wawili na anajua anakizazi kulikoni nyiye wanasheitwani wakubwa nyiye mliofanya mapenzi kuliko hata wazazi wenu afu mnajisifia kabisa Yaani nyiye ambao kila kona za mtaa wa Kwanza, wa pili,watatu,wanne na hata watano na kuendelea zinawajua.Afadhali mwezenu ni mwanamama kwasasa anajulikana kwamba ana sherehe yake duniani lakini je kwa nyiye mnasherehe gani duniani?.Au siki hizi kuna siku ya makahaba duniani.Labda kama itakuwa imeanzishwa hivi karibuni.Yaani mnaongea kwa kujitapa kabisa na midomo yenu kama kunguru wa pwani kwa wale wala urojo.Nyiye wakati Hamjijui hata kama mna vizazi.Etiiiii kabisaaaaaaa mnajitapa wataalamu wa kuruka fimbo ikitaka kuangusha mate meupe mazito.Wakati mate hayo meupe umeyameza na baadaye ukanywa maji malaini na magumu mengine ya mviringo tayari yakawa yametoa hayo mate meupe ya fimbo ambayo ilikuwa nyeusi Au nyeupe. Nyiyeeeee wajukuu zangu laiti mngejua mama zenu walivyolia siku ile ya kujifungua Basi mngempa pongezi huyu mwanadada mnayemzonga hapa kwamba Ana watoto wawili hata umri wa kufikia watoto wawili haujafika.Yawezekana wewe unayemwambia mwezako kwamba jamaa yake ananuka shombo.Afadhali huyo anajua ananuka shombo ila ni mchumba wake halali iko siku tu maisha yanaweza kumbadilikia na kujikuta shombo zimeenza Kunukia marashi kama hamjaanza kumfuatilia huyo mme wake ili muweze kumchuna vizuri.Sasa kulikoni nyiye ambao mnasema kwamba mna mabahasha wenu huko huko mtaani,mjini Kumbe waume wa watu.Nyoooooooooo....Shwaiiini nyiye hamjui cha mtu mavi.Embu ondokeni hapa hata sitaki kuwaona hapa machoni mwangu.Wanakulaaniwa nyiye.Yaaani mnavyoongea mtafikiri mnajua hata litakalotokea kesho kumbe hata litakalotokea baada sekunde chache zijazo hamjui.
Baada Bibi yule kuwafukuza pale na Zamda naye akaamua kujitwisha ndoa yake na kisha ndoto Hiyo inaonesha Kwamba Zamda Anaonekana anamuaga Bibi yule japokuwa hamjui kabisaa.
Ndoto ile ikawa imeishia pale na Hapo hapo tayari Zamda akawa ameshituka  na akatoka kitandani pale kisha akaenda sehemu taa ile ya kuwaka kwa kuchajishwa na nguvu ya jua.Kufika pale mezani akawa amewasha taa ile na akawa amerudi kukaa kitandani pale akiwa amekaa kitako huku akiwa kajifunika shuka lake la bluu.Lakini huku anaonekana anahema kwelikweli kwa ndoto ile aliyokuwa akiiota.Mda huo ikiwa ni usiku wa manani Kabisa Huko nje pamenyamaza kimyaaaaaa na kutulia tuliiiiiiii Yaani hata ukiangusha Sindano Kwakweli unaweza kusikia mlio wa Sauti yake.Kisha akaanza kuongea peke yake
Mama Yangu ndoto gani hii mungu wangu embu niepushie hili balaa nililoliota Lahaula eeeeeeeee mbona kama sielewi. Yaani Nina watoto wawili alafu Mwantumu na Kidawa hawana mtoto hata wakusingiziwa tu.Eeee mungu weeeeeeee niepushie mbali kabisaaaaaaa hili balaa.Yaani kabisa nimepewa mimba na mtu ambaye hata maisha kwake hayafai.Sasa hii ndoto inamaanisha nini."Mda huo anavyoongea hivyo akawa hata anajisahau yuko ndani ambapo chumba kinachofuatia hapo ni chumba ambacho wanalala baba na mama Zamda. Kwahiyo Baba Zamda akawa anasikilizia sauti ile kwa mbali sana ndipo akaja akajua kwamba sauti ile inatoka hapo ndani kwa Zamda. Baada ya baba Zamda kutambua hivyo ndipo akawa anamuamsha mama Zamda kwakusema Hivi ".
Mke  wangu.....mke wangu embu inuka."Baba Zamda akiwa anaongea kwa sauti ya chinichini.Mama Zamda akiwa anaonekana yuko katika Bahari ya Usingizi mzito kwelikweli.Akawa ameitika kwakusema Hivi".
Mmmmmh nini mme wangu usiku huu?.
Wewe inuka ndipo utajua ninini usiku huu.
Lakini Jamani mme wangu ."Baada ya kuamka mda huo Zamda bado anaongea huko chumbani kwake. Kisha baba Zamda akawa anamwambia hivi mama Zamda".
Sasa hivi ni kama saa nane na midakika hivi Lakini huko chumbani kwa Zamda huko nasikia sauti kabisaaaaaaa ya mtu akiongea na taa hiyo iko imewashawa."Kisha mama akarukia Mada kwakusema Hivi".
Sidhani kweli.
Hudhani Kitu gani wewe inawezekana huyo Zamda kaingiza mwanaume huko ndani.
Hapana haiwezekani mme wangu Zamda hawezi kufanya hivyo.
Embu mke wangu nenda kamuangalie inawezekana ni janga limemkuta huko alafu sisi tunaanza kujibunia tu hapa.Nenda kamuangalie Neenda."Nakweli mda huo Mama Zamda Anaonekana anainuka Haraka Haraka ili kwenda kumuangalia huyo Zamda.
Siku iliyofuatia ilikuwa ni siku ya Jumamosi Hivi ambapo siku hiyo kwa Zamda na shoga zake huwa hawaendi shuleni. Lakini Zamda ,Mwantumu na Kidawa huwa wanaishi mtaa mmoja.Basi siku Hiyo walienda Kabisa Nyumbani kwa akina Zamda .Ambapo mama na Zamda huwa naye anajishughulisha na shughuli za kijungu Jiko tu huko mjini Kwahiyo kwanzia asubuhi hadi Jioni huwa hapatikani nyumbani na hata baba Zamda pia anajishughulisha na vishughuli vidogovidogo tu huko mjini.
Basi wakiwa wamekaa hapo nje maongezi yao yalikuwa hivi.
Mhhh shoga yangu maamzi yamefikia wapi Kwasababu natamani niyajue kwelikweli."Huyo ni Kidawa Ndiye aliyekuwa amemuuliza swali hilo.Kisha Zamda akajibu hivi".
Maamuzi ni ya kawaida tu.Kwakweli Kidawa na Mwantumu huo ushauri wenu sidhani kama utanifaa."Kisha Kidawa akasema Hivi ".
Yaani tuseme Jana  tulifanya kazi bureeeee Kabisaaaaaaa. Umeona sisi kwamba ushauri wetu wala haufai kuandikika. haya."Mwantumu naye akasema Hivi".
Sawa Basi wewe fuata huo wa mama yako na wewe hujui sijui na mama yako naye kipindi kama hiki alikuwaje."Zamda akawajibu Hivi".
Sawasawa haina shida acha tu nibaki mjinga mjinga tu Hivi Hivi.
Baada ya Kidawa na Mwantumu kuona kwamba huyo Zamda haelekei katika mstari wao wakawa wameamua kuondoka nyumbani kwao.
Lakini baada ya miezi kuzidi kwenda zaidi na tabia za Zamda kidogo nazo uvumilivu ulianza kufikia ukingoni. Ambapo kipindi hicho bado kama mwezi mmoja wafanye Mtihani wa Taifa wa kidato cha pili.
Siku hiyo ikiwa ni mishale ya saa sita za Usiku sehemu fulani katika club fulani Hivi iliyoko katikati ya jiji Mda huo  Kidawa na Mwantumu wakiwa nao wanaingia ili watafute eneo maalumu la kujikita.Lakini kwa mbali Kidawa anaona kama vile sura ya Zamda ila haamini ni kama ni Zamda kweli au kama vile ni changa la la macho.Kwahiyo wakaamua wanyooshe njia moja kwa moja hadi hapo wanapomuona huyo Zamda baada ya Kidawa kumshitua Mwantumu kwamba kama ile sura wanaijua.
Kidawa na Mwantumu Kwakweli walivyovaa ni mithili ya wanadada wanaotaka kwenda kuigiza nyimbo fulani ya mahadhi ya kimagharibi.Huyo Mwantumu kutokana na kaurefu fulani alikojaaliwa ndiyo haswaa akawa anaonekana kama vile mzungu ukichanganya na weupe wake Fulani hivi. Kavaa kinguo ambacho kimefunika huko Nyumba tu Lakini huku Mbele ya uke wake kama vile kimetobolewa tobolewa Fulani hivi na kikiwa ni kifupi Kweli Kweli. Kiatu cha bei ghali.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)