MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: NIMEONJA LADHA YAKE

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: NIMEONJA LADHA YAKE
#1
NIMEONJA LADHA YAKE
Mfano wake halua, kabichi na bilingani,
Hapana nimekosea, niseme ja kitu gani?
Vile mmeniambia, nifananishe na nini?
Amezidi nizuzua, maana namwita honey.

Yule bwana anajua, kunipa nyama laini,
Anipavyo kwa hatua, basi mie taabani,
Ai nimemzimia, kunishika niacheni,
Amezidi nizuzua, maana namwita honey.

Sio kujiropokea, nipeni heko jamani,
Siku hizi nasinzia, hali mwepesi mwilini,
Kama katoka Asia, penzi lake la fasheni,
Amezidi nizuzua, maana namwita honey.

Nyie mnojisifia, makelele mtaani,
Mnajipiga vifua, wachovu nimebani,
Amewazidi hatua, huyu kijana jamani,
Amezidi nizuzua, maana namwita honey.

Na huyu kumfikia, Kuna kazi tambueni,
Ni bado kumfikia, nendeni bara na pwani,
Mana nawasimulia, Kuna wajuzi jamani,
Amezidi nizuzua, maana namwita honey.

Ukimwona amepoa, yake kazi kitandani,
Kweli watu wanajua, na leo nimeamini,
Mtunzi namsifia, Wala haya si matani,
Amezidi nizuzua, Mana namwita honey.

Leo ninamuimbia, ameniweza fanani,
Ai ninawaambia, wake utamu acheni,
Kama wali kwa bamia, sijui niseme nini?
Amezidi nizuzua, maana namwita honey.

Mumeshikwa na tamaa, yenu macho yaoneni,
Mnaanza kulegea, hebu nenda kalaleni,
Nataka kumpigia, niongee na mwendani,
Amezidi nizuzua, maana namwita honey.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)