MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
Chemsha Bongo

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
Chemsha Bongo
#1
Chemsha Bongo
  • Maswali ambayo huhitaji mtu kutumia akili na ujuzi kuyajibu.
  • Mafumbo ni kauli zenye maana iliyofichika na hujumuisha vitendawili na chemshabongo.
Mifano
  1. Kilo moja ya chuma na kilo moja ya nyama ipi nzito?
  2. Amada ana wafanyikazi saba, wanne hufanya kazi vizuri, wawili ni kama wamekufa, mmoja ni kama mwenda wazimu- miguu, pembe na mkia wa ng’ombe.
  3. Kipungu alipita juu, mama na ndege wawili wakamwangalia. Je macho mangapi yalimuona kipungu?- manne.
  4. Nina watu wangu watatu, wawili ni watoto na wawili ni baba- mtoto, baba na babu.
  5. Chura alitumbukia katika shimo la futi 30 na anaruka futi 10. Aruke mara ngapi ili atoke?- Hawezi.
  6. Watu watatu wanavuka mto. Mmoja aliyaona maji na kuyakanyaga. Wapili aliyaona lakini hakuyakanyaga. Watatu hakuyaona wala kuyakanyaga. Watu hao ni kina nani?
Sifa
  1. Ni kauli fupi au ndefu.
  2. Hutuia lugha ya kimafumbo.
  3. Hutumia ufananisho wa kijazanda.
  4. Huhitaji mtu kuwaza ili kupata jibu.
  5. Hujengwa na vitu vinavyotokana na mazingira.
  6. Hazina muundo maalum kama methali, nahau na vitendawili
  7. Hupima uwezo wa msikilizaji wa kutambua jambo lililofichwa.
Umuhimu
  1. Kuimarisha stadi ya kusikiliza.
  2. Kunoa uwezo wa kufahamu.
  3. Kutoa mawaidha.
  4. Kufunza kuhusu maumbile.
  5. Kuimarisha uwezo wa kukumbuka.
  6. Kufunza mambo kuhusu mazingira na maumbile.
  7. Kukuza uwezo wa kutumia lugha.
  8. Kukuza uwezo wa kufikiri.
  9. Kuburudisha na kuchekesha.
  10. Kukuza uwezo wa kubuni.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)