MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
KILA KITU KINA UPANDE WAKE WA PILI KATIKA MAISHA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
KILA KITU KINA UPANDE WAKE WA PILI KATIKA MAISHA
#1
Tunaishi katika dunia ambayo watu wasio na pesa wanatafuta pesa ili wapate furaha, wakati huo watu wenye pesa wala hawana furaha na pesa zao.
Hii ni dunia ambayo maskini anakula chochote anachokipata akisononeka kuwa angekuwa na hela, labda angekula vizuri zaidi. Lakini yupo tajiri anayekula mchicha wa kutandika kwa sababu ya maradhi yanayoushambulia mwili wake.
Kuna mtu yupo hospitali anazungumza na daktari kwa siri amsaidie kutoa mimba, halafu kuna mwingine yupo chumba cha pili anamuomba daktari amsaidie mwaka wa saba huu hajapata mtoto.
Kuna mtu yupo sehemu fulani ya dunia anatia saini hati ya talaka kuwa haitaki tena ndoa yake. Lakini kuna mtu yupo kanisani amepiga magoti anamuomba Mungu ampatie mume.
Nimejionea sana kipindi nasoma, kuna wanafunzi wanatamani kusoma lakini wanaondoka shule kwa sababu wazazi wamekosa ada kama ilivyo kwa Watoto wa Mama N'tilie katika ile riwaya maarufu ya Emmanuel Mbogo, lakini kuna wanafunzi wanaondoka shule kwa sababu wazazi wanawataka wakasimamie biashara zao.
Kuna mtu sasa hivi anaandika barua ya kuacha kazi kwa sababu kazi yake imemchosha. Halafu kuna mtu anabadilisha bahasha ya kuhifadhi vyeti vyake, mwaka wa sita huu hana ajira.
Nimejifunza sana kutoka kwa watu maarufu. Kuna mtu sasa hivi anaumiza kichwa usiku na mchana atakuwaje maarufu afahamike na kila mtu mjini halafu yupo staa anayetamani kushuka kwenye gari aingie japo mtaani kuzurura lakini hana hiyo nafasi tena.
Kuna mzazi sasa hivi anatamani muda urudi nyuma ili akamfunze mtoto wake maadili, halafu kuna mzazi analia amempoteza mwanawe, baada ya kumlipia ada na kumpatia malezi mazuri kwa miaka yote, leo amekunywa sumu kwa sababu ya mpenzi aliyekutana naye mwaka jana.
Nilijionea nilipokuwa shule, kuna mwanafunzi analia kupata "C" akiamini amefeli sana lakini kuna mwanafunzi anayerisiti mwaka wa tatu sasa anaitafuta hiyo "C".
Hata ninapomaliza kuandika haya, kuna mtu anasoma akiamini hiki ni kitu chema kwake lakini yupo anayeona hili andiko ni ujinga na upuuzi tu.
Lakini ninachojaribu kusema hapa ni kuwa, kila kitu kina upande wake wa pili wa maisha. Unachoona bora kwako kwa mwingine kinaweza kuwa takataka. Kinachoweza kuwa takataka kwako kwa mwingine kinaweza kuwa bora. Kwa hiyo, tuishi maisha yetu tuliyopewa na Mwenyenzi Mungu.....?

Imenukuliwa mtandaoni.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)