MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
TOFAUTI YA UKUMUSHI NA UVUMISHI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
TOFAUTI YA UKUMUSHI NA UVUMISHI
#1
“Kwa hakika hakuna tofauti kati ya vivumishi na vikumushi.” Vikumushi na vivumishi ni dhana mbili ambazo zimekuwa zikileta mkanganyiko mkubwa sana katika taaluma ya isimu. Maneno haya huweza kufanana na kufanya kazi sawa, lakini kwa upande mwingine huweza kutofautiana. Kama inavyojadiliwa hapa chini.
Chuo kikuu cha Oxford (2005) wamefasili kikumushi kuwa ni neno ambalo linaweza kuwa kivumishi au kielezi ambacho kinaelezea neno au kundi la maneno mengine (tafsiri). Katika fasili hii maana ya kikumishi imetolewa kiupana kwa kiasi fulani, lakini bado kikumushi kinaweza kuwa zaidi ya kivumishi au kielezi, na kuwa kitenzi na aina
nyingine za maneno. Khamisi na Kiango (2002:58) wameeleza maana ya kikumishi kuwa ni maneno ambayo siyo
vivumishi asilia, lakini hufanya kazi kama vivumishi, yaani kazi ya kukumusha (kuongeza sifa au taarifa muhimu) nomino.
Wanaendelea kusema kuwa vikumishi siyo vipashio vilivyo katika kiwango cha neno tu, bali ni pamoja na makundi ya maneno ambayo yamo katika kiwango cha kirai au kishazi. Mfano; Kikumushi nomino: baba watoto ; Kikumushi Kirai: baba wa taifa (KH) Kikumushi Kishazi: mtoto aliyeshinda . Hivyo basi kutokana na fasili hizo mbili zilizotolewa tunaweza kusema kuwa kikumushi huweza kufasiliwa katika mawanda finyu na mawanda mapana. Katika mawanda finyu; kikumushi ni maneno yanayotoa taarifa ya ziada kuhusu nomino. Mfano; watoto wangu , mtoto wa juma . Maneno wangu na wa Juma ni vikumushi vya nomino watoto na mtoto. Katika mawanda mapana: kikumushi ni maneno yanayotoa taarifa ya ziada kuhusu aina nyingi ne yoyote ya maneno yaani
nomino, kitenzi, kielezi.
Mfano; aliyeimba kwa madaha, Mfano wa pili; Anacheza vizuri sana. Neno kwa madaha na vizuri sana yanakumumusha vitenzi aliyeimba na anacheza vizuri. Kwa upande mwingine kivumishi kama aina mojawapo ya aina za maneno imefasiliwa na wataalamu kama ifuatavyo; Matei (2009:43) anasema kuwa “kivumishi ni neno ambalo hutoa maelezo zaidi kuhusu nomino au kiwakilishi cha nonimo. Ni neno ambalo huonesha sifa
mojawapo ya nomino/kiwakilishi cha nonimo.” Fasili hii inajitosheleza kwani mara nyingi kazi kubwa ya kivumishi ni kutoa sifa juu ya nonimo au kiwakilishi.
Mfano, Mtoto mzuri. Neno mzuri ni kivumishi kinachovumisha nomino mtoto. Baada ya kuelezea fasili mbalimbali za maneno makuu, maelezo yafuatayo huelezea kwa kina ni jinsi gani kivumishi ni kikumushi. Katika fasili ya kivumishi na kikumushi, huweza kuleta ufanano fulani kwani kivumishi hutoa maelezo zaidi kuhusu nomino. Pia
kwa maana finyu ya kikumushi ni kwamba kinatoa taarifa ya ziada kuhusu nomino. Hivyo basi kivumishi na kikumushi huelezea juu ya nomino.
 Mfano, Kijana mtanashati, mchezaji mashuhuri . Kwa muktadha huu neno mtanashati na mashuhuri huelezea
juu ya nomino, hivyo maneno hayo yote ni vikumushi au vivumishi kwani vivumishi na vikumushi vyote hufanya kazi ya kutoa maelezo ya ziada juu ya nomino. Kutokana na kufanya kazi sawa katika sentensi, tofauti inaweza
isiwepo. Mfano, mwanafunzi msafi . Mwanafunzi aliyeugua amepona. Hivyo neno msafi katika sentensi ya kwanza ambayo ni kivumishi na aliyeugua katika sentensi ya pili ambayo ni kikumushi hufanya kazi sawa ya kutoa taarifa juu ya nomino.
Hata hivyo ufanano unaoonekana kati ya kivumishi na kikumushi ni pale tu kikumushi kitakapofasiliwa kiufinyu, lakini kikumushi kwa maana pana hudhihirisha tofauti kubwa sana kati ya kivumishi na kikumushi kama inavyooneshwa hapa chini. Kivumishi huwa ni neno moja lakini kikumushi huwa ni neno moja au zaidi. Mfano; ng’ombe mweusi anakunywa maji. Neno mweusi ni kivumishi ambapo ni neno moja. Mwalimu aliyenipa kalamu ameondoka. Katika sentensi hii neno aliyenipa kalamu ni kikumushi chenye zaidi ya neno moja. Hivyo kivumishi ni neno moja tu lakini kikumushi huweza kuwa neno moja au zaidi, kirai au kishazi.
Kivumishi hutoa taarifa kuhusu nomino au kiwakilishi tu lakini kikumushi hutoa taarifa zaidi juu ya nomino, viwakilishi na aina zingine za maneno. Mfano; kiongozi muadilifu huongoza kwa busara, wewe ni msafi kuliko wote.
Maneno muadilifu na msafi hutoa taarifa juu ya nomino na kiwakilishi. Mfano; anayetembea kwa maringo . Neno kwa maringo ni kikumishi kirai kihusishi ambacho hutoa taarifa juu ya kitenzi anayetembea. Mara nyingi neno kivumishi hutumika kuelezea aina ya maneno hayo katika muktadha wa kimuundo na kileksika lakini kikumushi hutumika kuelezea maneno hayo hayo (ambayo ni kivumishi) na maneno mengine katika muktadha wa kidhima,
huangalia kazi ya neno hilo. Mfano; mtoto mpole hulelewa vizuri. Neno mpole katika muktadha wa kimuundo ni
kivumishi lakini katika muktadha wa kidhima ni kikumushi kwani hufanya kazi ya kutoa taarifa juu ya nomino mtoto. Mfano mwingine, mwanafunzi mtukutu hafaulu vizuri. Neno mtukutu ni kivumishi kimuundo na kikumushi
kidhima. Kivumishi huweza kuwa katika ngazi ya neno na kirai katika tungo. Mfano; mchezaji mashuhuri . Neno mashuhuri ni aina ya tungo neno ambalo ni kivumishi na ni aina ya tungo kirai ambalo ni kirai kivumishi. Hivyo kivumishi hakiwezi kuvuka ngazi hizo mbili za tungo, lakini kikumushi huweza kuwa katika ngazi ya tungo neno,
kirai, kishazi na hata sentensi. Mfano; mwanafunzi anayesoma kwa bidii atafaulu mtihani . Neno mtihani limesimama kama kikumushi cha kitenzi atafaulu kama tungo neno. Kwa bidii ni kikumushi kirai, anayesoma ni kikumushi kishazi.
Utofauti mwingine hujitokeza katika dhana kwamba kila kivumishi ni kikumushi, lakini si kila kikumushi ni kivumishi. Hivyo basi kwa muktadha huu siyo dhahiri kuwa kivumishi ni kikumushi. Mfano; kijana mtukutu anaadhibiwa na mwalimu . Neno mtukutu ni kivumishi na ni kikumushi, lakini neno na mwalimu ni kikumushi na siyo kivumishi, hivyo ni kwa kiasi kidogo sana juu ya ufanano wa kivumishi na kikumushi.
Kwa kuhitimisha, kauli kuwa kivumishi ni kikumishi huthibitika tu endapo fasili ya kivumishi itakuwa katika muktadha wa maana finyu ambapo vyote huelezea juu ya nomino na hufanya kazi ya kutoa taarifa ya ziada juu ya nomino. Lakini kwa upande mwingine wa fasili ya kikumushi katika muktadha wa maana pana, kuna utofauti mkubwa kimuundo na kazi kati ya vikumishi na vivumishi. Hivyo basi kwa kiasi fulani vivumishi ni vikumushi na
kwa kiasi fulani vikumushi si vivumishi.
MAREJEO:
Khamisi, A.M na John, G.K. (2002). Uchanganuzi wa Sarufi ya Kiswahili . TUKI. Dar es salaam.
Chou Kikuu cha Oxford (2005). Advanced Learners Dictionary . Oxford University Press. U.S.A.
Matei, A.K. (2008). Darubini ya Sarufi. Phoenix Publishers. Nairobi.
TUKI. (2010). English – Swahili Dictionary . (3 rd Edition). MSM L.t.d. Mauritius.
Mwl Maeda
Reply
#2
Somo zuri sana hili. Linasaidia katika ufundishaji na uchanganuzi wa sentensi changamano
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)