MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
Vidahizo vya Fani ya Usindikaji Mafuta na Matunda, na Utengenezaji wa Sabuni

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
Vidahizo vya Fani ya Usindikaji Mafuta na Matunda, na Utengenezaji wa Sabuni
#1
Bb
besi ji base: kemikali ambayo ikitendana na asidi hutoa chumvi na maji, na hubadili litimasi kuwa buluu.
Cc

chachuka kt ferment: kubadilika kikemikali kwa vitu vya kikaboni kwa kutendana na viumbe hai kama bakteria, n.k.
Ff
fua kt dehydrate: ondoa maji yote yaliyomo ndani ya kitu.
Hh
hasi kt sterilize: 1. ua vijidudu na viumbe vinavyosababisha maradhi. 2. fanya kiumbe kisiwe na uwezo wa kuzaa.
hatimiliki ji patent: kibali anachopewa mtu na serikali cha kumruhusu kutengeneza, kuuza kitu kwa muda maalum.
Kk
kabohidrati ji carbohydrate: msombo wa kaboni, hidrojeni na oksijeni, kama vile uwanga, sukari na selulosi.
kakamaza kt stabilize: fanya kitu tepetepe kuwa kigiumu kwa kutulizana.
kichochezi ji catalyst: dutu inayozidisha kasi ya mmenyuko.
kihawilijoto ji heat exchanger: kitumi cha kuhamisha joto la kioevu kimoja kwenda kwenye kioevu kingine bila ya kuchanganyika pamoja.
kihifadhi ji preservative: kitu kinachozuia uharibikaji au udhurikaji wa dutu.
kimeng’enya ji enzime: kichochezi ambacho kwa kawaida ni protini kinachotengenezwa na selihai.
kimeng’enywa ji substrate: dutu inayosahilishwa kwa ajili ya matumizi ya kujenga, kulinda na kutia joto mwilini.
kindaoksidishi ji antioxidant: kemikali inayozuia athari za ubabuzi wa metali, k.m., kupata kutu kwa chuma.
kinu ji mill: mashine itumikayo kuponda au kusaga mbegu za mafuta au nafaka.
kioevu ji liguid: kitu kama maji, maziwa, mafuta, au soda kinachoweza kumiminwa.
kioevu babuzi ji caustic lye: kioevu kinachotumika kutengeneza sabuni, nacho huunguza au huharibu kwa amali ya kemikali.
kiolwa ji object: kitu kinachoweza kuonekana, kusikika, kuhisika au kuguswa.
kitako ji base: sehemu ya chini kabisa ya kitu, hasa ile sehemu ambayo kitu husimamia.
kitako
kitambulisho ji label: kipande cha karatasi au maunzi kinachoambatishwa ili kukijulisha kitu fulani ni nini, cha nani au wapi kinatoka au kinapelekwa.
kiwangomchemko ji boiling point: halijoto ya kioevu kinapoanza kuchemka. Hali hii hutofautiana kutegemea kanieneo ya angahewa ya mazingira.
kiwangomyeyuko ji melting point: halijoto ambapo dutu hubadilika kutoka mango kuwa kioevu.
koleza kt concentrate: fanya kioevu kuwa thabiti kwa kuongeza kumumunyishwaji au kwa kupunguza kiasi fulani cha maji.
Mm
mafutaghafi ji crude oil: mafuta ambayo hayajapitia mchakato wowote wa usafishaji.
mafuta haradali ji mustard oil: mafuta yaliyokamuliwa kutokana na mbegu za haradali.
mafuta laini ji soft oil: mafuta ambayo yamesafishwa sana.
mafuta mahindi ji corn oil: mafuta yaliyotengenezwa kutokana na kukamua mahindi.
mafuta mimea ji vegetable oil: mafuta yanayotokana na usindikaji wa mbegu za mimea, k.m., alizeti, n.k.
mafutauto ji oil: mafuta ya majimaji yasiyoganda kwenye baridi.
magadi ji soda ash: kemikali inayounguza; inayochoma; inayomomonyoa mwili na vitu vingine. Fomula NaCh.
magadi babuzi ji sodium hydroxide: aina ya kemikali inayounguza, inayochoma, inayomomonyoa mwili au vitu vingine.
majinyongo ji brine: maji yenye madini mengi ya chumvi.
mango ji solid: kitu kisichokuwa kioevu au gesi.
maunzi ji material: chochote ambacho kutokana nacho kitu chaweza kutengenezwa.
menyu kv pure: isiyo na uchafu au mchanganyiko wa dutu yoyote nyingine.
midia ji medium: dutu inayoingilia kati ambayo inabidi kani au athari fulani ipite ndani yake, mathalani, hewa maji, metali, n.k.
mikrobiolojia ji microbiology: mtaala wa kisayansi wa viumbehai vidogovidogo sana kama vile bakteria, virusi, protozoa, kuvu, n.k.
mituamo ji statics: elimu ya jinsi ya vitu vinavyokaa katika hali tuli na kani za msawazisho.
mjao ji volume: kipimo cha nafasi kinachokaliwa na kitu.
msibiko ji contamination: hali ya kuwa chafu kutokana na kuguswa au kuingiwa na kitu.
mtovu kv centripetal: -enye kuelekea kwenye nukta.
mumunyisha kt disssolve: fanya kioevu kwa kutia ndani ya kioevu.
mvuke ji vapour: hali mojawapo ya mata ambapo dutu inakuwa katika hali ya gesi.
mvukemaji ji steam: maji katika hali ya gesi inayotokana na kuchemka.
myuko ji convection: msogeo ndani ya gesi au kioevu unaosababishwa na kioevu au gesi fukuto inayopanda juu na gesi au kioevu baridi kinachoshuka chini.
Nn
neli ji tube: mrija mwembamba
nishati ji energy: nguvu, na uwezo wa kufanya kazi.
nururisha kt radiate: piga kiolwa kwa miali ya nuru, joto, n.k.
Oo
ombwe ji vacuum: nafasi bila ya hewa au gesi ndani yake.
Pp
pimamchepuko ji refractometer: chombo cha kupimia kiasi cha mchepuko na kipeomchapuko.
pimamchepuko
pepetaka ji foreign matters: takataka ambazo huvunwa pamoja na mbegu zinazotoa mafuta; nazo hutolewa kabla ya ubanguaji.
Rr
regesha kt recycle: rudisha katika hali ya kwanza ili kitumike tena.
Ss
sabuni ya kimetali ji metallic soap: chumvi isiyomumunyika iundwayo na metali pamoja na asidi shahamu. Hutumika kuvifanya vitambaa visipenyeke na maji kwa urahisi na pia kama kikaushio cha rangi.
safisha kt refine: toa uchafu, k.m., kutoka kwenye sukari, metali, na mafuta.
shahamu ji fats: mafuta yanayotokana na wanyama, aghalabu ya kuganda.
Tt
themometa ji thermometer: ala ya kupimia halijoto.
themometa
Uu
uchepukaji ji refraction: badiliko la uelekeo wa mnururisho wakati wa kupita, kutoka na kuingia midia nyingine kutokana na mnururisho kuwa na kasi tofauti katika midia hizo.
ujazo ji capacity: nafasi inayopimwa kwa kuzidisha urefu kwa upana kwa kina.
ukebeshaji ji canning: hifadhi ya chakula katika makopo.
uoksidishaji ji oxidation: utaratibu au kitendo cha kuongeza oksijeni, kupunguza hirojeni au kupunguza eleletroni kwenye kemikali yoyote.
upasterizaji ji pasteurilization: kuua bakteria katika maziwa kwa kuchemsha hadi kufikia halijoto ya 60°C.
usindikaji ji milling: ukamuaji wa mbegu au tunda ili kutoa umajimaji uliomo.
utokaji ji emission: kutoka kwa kitu katika kitu kingine.
uvukizaji ji evaporation: ubadilishaji wa kioevu kuwa mvuke.
uzito wiani ji relative desinty: uwiano kati ya masi ya mata katika mjao fulani na masi ya maji yenye mjao sawa.
Vv
vitamini bandia ji artificial vitamin: taz. vitamini: SAYANSI KIMU.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)