MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO "MAHABA''

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO "MAHABA''
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO "MAHABA''

Neno mahaba katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: ya-/ya-] yenye maana zifuatazo:

1. Hisia za mvuto zinazojengeka kwa mtu mwengine kutokana na kupendezwa naye. (Chanzo: Kamusi Kuu ya Kiswahili).

2. Hali ya kuvutiwa na kitu au mtu kutokana na uzuri wake ambao huingia moyoni na kumfanya ampende. (Chanzo: Kamusi ya Karne ya 21).

3. Hali ya kuingiwa moyoni na mtu au kitu na kukuthamini zaidi ya vingine; mapenzi .(Chanzo: Kamusi ya Kiswahili Sanifu - TUKI).

4. Matandu ya wali yaliyoandaliwa maalumu kama tunu kwa mume.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili mahaba linatokana na neno la Kiarabu mahabbah محبة  ( soma: mahabbatun/mahabbatan/mahabbatin محبة) lenye maana zifuatazo:

1. Kupendana na kuthaminiana moyoni.

2. Ashiki inayojenga ubinafsi wa pendo na wivu.

3. Kinachotakiwa na moyo.

4. Ki-Falsafa, mahaba ni sababu inayoleta pamoja vitu mbalimbali.

Kinachodhihiri ni kuwa neno mahabbatun  محبة lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno mahaba lilichukua maana jumla ya mapenzi na kuleta maana mpya ya matandu ya wali yaliyoandaliwa kama tunu kwa mume.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)