MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
METHALI NA MAANA ZAKE

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
METHALI NA MAANA ZAKE
#1

  1. Aliye juu mngoje chini: Inatukumbusha kuwa na subira na kukubali pale ambapo mwenzio amekuzidi nafasi fulani basi hauna budi kumheshimu.
  2. Kamba hukatikia pembamba: Kamba ni kitu chochote kinachotumika kufungia vitu mathalani kuni n.k. Ili uweze kulitatua jambo fulani ni vyema ukaangalia penye udhaifu ili usitumie nguvu kubwa.
  3. Jungu kuu halikosi ukoko: Ni kawaida kuona chakula kikipikiwa kwenye vyungu vikubwa na masalia ya chakula hasa ukoko kubaki. Watu wenye hekima na wazee hawakosi neno la kutia kwenye mazungumzo. Watu wanapaswa kuomba ushauri kwa watu wazima wakati wowote ili wapate msaada wa mawazo kwa watu wazima au viongozi watakuwa na jambo la kusema.
  4. Akumulikaye usiku, mchana atakuchoma:Mzaha unaweza kusababisha jambo halisi kutokea. Katika maisha kuna watu wanaweza kukutishia halafu ukapuuzia, usipuuze kwa sababu anaweza kuwa anamaanisha au kama mtu ana uwezo wa kukusema vibaya mbele yako basi anaweza kukusema zaidi ukiwa ufahamu
  5. Kidole kimoja hakivunji chawa: Ushirikiano ni jambo la msingi katika kufanikisha jambo lolote lile. Ukifanya peke yako mambo yanakuwa magumu kama vile ambayo ni vigumu kumchukua chawa ukataka kumuua kumuua kwa kidole kimoja.
  6. Mwenda pole hajikwai: Kufanya jambo bila haraka kunasababisha jambo kufanyika kwa ufanisi zaidi kwa kuwa mawazo kufikiria vyema.
  7. Figa moja haliinjiki chungu: Figa ni jiwe kitu kinachotengenezwa ili kushikilia chungu au sufuria ikiwa jikoni. Huhitajika mafiga matatu na si moja. Hivyo, ili kufanya jambo ni sharti kuwe na ushirikiano wa watu. Ona pia methali kama; kidole kimoja hakivunji chawa
  8. Akiba haiozi: Methali inasisitiza umuhimu wa kuweka akiba ya kitu mathali fedha, chakula na vingine kwa matumizi ya baadaye.
  9. Aliyeshiba hamjui mwenye njaa: Njaa ni hali ya kuhitaji chakula au haja ya kufanya kitu fulani. Mtu asiye na haja ya jambo fulani haoni umuhimu wa kitu hicho kama ambavyo mwenye haja nacho aonavyo haja ya kukipata. Maana yake ni kwamba watu huwa hawajali haja na mahitaji ya watu wengi. Ni vyema kujali watu wengine.
  10. Sikio la kufa halisikii dawa: Hakuna awezaye kukizuia kifo, hivyo kikitaka kuja hakuna namna ya kukizua. Kuna mambo ambayo hufikia katika kiwango ambacho hayawezi kubadilika bila kujali nguvu itakayotumika, kwahiyo huachwa kama lilivyo.
  11. Lisemwalo lipo, kama halipo laja: Kuna maneno husemwa na wakati mwingine sio ya kweli. Hata hivyo ni vigumu kusema tu mambo ambayo hayapo, kwahiyo ni vyema kuyatilia maanani mambo yasemwayo kwani huwa na ukweli fulani ndani yake.
  12. Mwacha asili ni mtumwa: Ni vyema mtu akapathamini kwao kwa sababu ndipo alipotokea na kumemfanya kuwa vile alivyo. Ni vyema kuendelea kulinda yanayohusiana na wewe badala ya kukumbatia mambo yasiyo ya asili yako. Ni vyema kukumbuka kwenu.
  13. Ukitaka kuruka, agana na nyonga: Nyonga ni viungo muhimu katika ya miguu na kiuno. Viungo hivi hushirikiana katika jambo lolote mathalani kutembea, kukimbia n.k. Unashauriwa kufanya maandalizi ya kutosha kabla ya kufanya jambo au kitu chochote. Hakikisha umelichunguza jambo au maamuzi unayotaka kuyachukua ili baadaye usijutie uliyofanya.
  14. Adhabu ya kaburi aijua maiti: Hakuna mtu yeyote anayefahamu maswahibu ya kaburi isipokuwa maiti iliyozikwa mule. Kuna mambo ni vigumu mtu kuyafahamu kama si mhanga wa jambo hilo. Mathalani, kuna watu hupitia changamoto kama maradhi ambayo maumivu yake hakuna anayeweza kuyahisi zaidi yake kwa sababu yeye ndiye mhusika.
  15. Mficha uchi hazai: Uchi ni siri. Ni sehemu ambazo hazipaswi kuwa hadharani hivyo zinapaswa kuficha kama sehemu za siri. Hata uchi ni kuwa wazi kwa hiyo, ni vyema kuwa muwazi katika mambo mbalimbali ili uweze kupata msaada. Si vyema kuwa na jambo linakuumiza halafu usileweke wazi ili usaidiwe.
  16. Zimwi likujualo halikuli likamaliza: Ndugu au rafiki anaweza kukuonea katika jambo fulani hasa adhabu, kukudhulum na mengine kwa sababu anakufahamu.
  17. Ukubwa ni jalala: Jalala ni mahali ambapo uchafu na takataka za aina mbalimbali hutupwa. Ukiwa mtu mzima au mwenye mamlaka fulani kuna mambo mengi yatasemwa kukuhusu. Utapongezwa, wakati mwingine utalaumiwa, utakejeliwa na mambo yanayofanana na hayo. Usitetereke wala kukata tamaa, ni hali ya kawaida.
  18. Kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa uhunzi: Uhunzi ni kazi ya kufua na kutengeneza vyuma na koleo ni kifaa kinachotumika kuchotea maka na kuweka kwenye tanuru. Kuna mambo, vitu na watu ambao huwezesha na kuwa mhimili shughuli au kazi fulani na yanapotoweka basi hudhaniwa kuwa ndiyo mwisho jambo ambalo si sahihi. Ikitokea changamoto ni vyema kuitatua na kusonga mbele. Mfano, katika kampuni au familia mtu muhimu akiondoka haimaanishi na shughuli zikome. Itafutwe namna nyingine ya shughuli na majukumu mengine kuendelea.
  19. Baada ya dhiki, faraja: Dhiki ni matokeo ya hali ngumu ya maisha au tukio fulani. Licha ya mambo magumu mtu anayopita hakuna shaka kwamba hayo yatapita na wakati wa furaha utafika. Kuna wakati unatafuta mafanikio katika mazingira magumu bila kupata, usikate tamaa kwani ipo siku utayapata na utakuwa katika wakati wa furaha.
  20. Dua la kuku halimpati mwewe: Kwa kawaida mwewe ni adui wa kuku kwa kuwa hula vifaranga. Inawezekana kuku humuombea mabaya mwewe ili asiwadhuru vifaranga lakini huwa ni vigumu yale anayoyaomba. Kuna mambo watu huwaombea wengine mabaya au wakati mwingine kuwalaani, ukweli ni kwamba mambo hayo hayawezi kutokea ikiwa Mungu hajapanga yakutokee.
  21. Mtegemea cha ndugu hufa maskini: Sio tabia nzuri kutegemea kusaidiwa kila wakati hasa na ndugu au rafiki au watu wengine. Ni vyema kuinuka na kufanya kazi au chochote kuwezesha kupata kipato au kitu chake kuliko kutegemea kupewa kila mara kwa sababu havutakusaidia sana.
  22. Usimwage mtama kwenye kuku wengi: Ni wazi kuwa ukimwaga mtama penye kuku wengine ni lazima kutatoka mtafaruku wa hali juu na pengine wasiweze kuufaidi huo mtama. Kuna mambo ambayo ni siri, hivyo si vyema kuyasema mahali penye watu wengi. Ikiwa kuna siri au jambo ambalo si la kuweka wazi mbele ya watu basi mtoe mhusika pembeni umwambie.
  23. Penye wengi pana mengi: Kila binadamu ana utashi wake na tabia yake humfanya afanye tukio au jambo fulani. Kwasababu kila mtu ana tabia yake, matukio pia yatatofautiana. Wakikutana watu wengi wenye tabia tofautitofauti, mambo mengi yanaweza kutokea mathalani, wizi, ugomvi, ushirikina, ulevi na mambo kama hayo.
  24. Haba na haba, hujaza kibaba: Haba ni kiasi kidogo. Ukikusanya kiasi kidogokidogo mwisho kitakuwa kikubwa. Methali hii inataka watu kuwa wavumilivu na kujiwekea akiba kidogokidogo mpaka pale ambapo kiasi kikubwa kitakapotokea.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)