MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI : KIMZINYI LAHAJA YA WAPI ?

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI : KIMZINYI LAHAJA YA WAPI ?
#1
SHAIRI : KIMZINYI
Hodi hodi na salamu, wa ushairi Mamwinyi.
Nna wasaili kwa hamu, wenye jawabu ni nyinyi.
Miye msinilaumu, akina Gakurya Mwinyi.
Mengi sijayangamua, hebu nifundeni ninyi.
 
Hususan pwani huko, Kiswahili kulikoni.
Yaliko yake mashiko, na miziziye kwa ndani.
Lahaja nyingi ziliko, kama vile Kibajuni.
Jamani huko mliko, Kimzinyi lahaja gani?
 
Kiswahili lugha tamu, kinazo nyingi lahaja.
Mathalani kihadimu, Kingwana na kiunguja.
Ninakipata kiamu, Kimgao na Kingadzija.
Kimzinyi mwafahamu, ya wapi hii lahaja?
 
Chibalonzi na Kimvita, Chimiini na Kimwani.
Kingozi na Kimtangata, nazielewa makini.
Hino lahaja ni tata, jama nitatulieni.
Kimzinyi wapi ntapata, manaye hii lahaja?
 
Zipo zingine lahaja, ni nyingi za Kiswahili,
Miye yangu moja haja, nijuzeni jambo hili.
Wasanii tu wamoja, nipeni yenu kauli.
Kimzinyi ni lahaja, ya cha nani Kiswahili?
 
Subukhana shukurani, tamati menifikisha.
Ya ushairi makini, hoja umepeperusha.
Baraka wajalieni, pia kuwaneemesha.
Wote hapa Kisimani, wape maisha marefu.
 
*****************************
 
Rwaka rwa Kagarama, (Mshairi Mnyarwanda)
Jimbo la Mashariki, Wilaya ya Nyagatare,RWANDA.
rwakakagarama2020gmail.com

Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)