MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
TABIA NA SIFA ZA LUGHA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
TABIA NA SIFA ZA LUGHA
#1
Tabia ya Lugha
Zifuatazo ndizo tabia zinazojitokeza kwa kila lugha; tabia ambazo zinaihalalisha
lugha yo yote kuwa lugha na si vinginevyo.

(i) Lugha Ina Tabia ya Kukua

Lugha hukua kadri inavyoendelea kutumiwa na jamii. Maneno ya zamani

yanabadilika, yote haya ni kutokana na mahitaji ya umma au jamii katika harakati za wana-jamii wake kujiboresha kimaendeleo ambako wakati mwingine si rahisi kutokana na misukosuko duniani. Kwa hiyo, kama lugha itakosa watumiaji.
(ii) Lugha Ina Tabia ya Kuathiriwa
Lugha inaweza kuathiriwa na lugha nyingine au inaweza kuathiri lugha nyingine.

Mfano lugha ya Kiswahili imeathiriwa sana na lugha ya Kiarabu, Kibantu na Kiingereza. Vile vile Kiswahili kimeathiri lugha hizo.

(iii) Hakuna Lugha Bora
Lugha zote ni bora. Ubora wa lugha upo kwa wale wanaotumia. Lakini pia kuna

lugha bora na bora lugha. Bora lugha hujitokeza kwenye misimbo na/au rejesta.

(iv) Kujitosheleza
Kila lugha inajitosheleza kulingana na mahitaji ya jamii ambayo inatumia lugha

yenyewe katika kipindi husika cha maisha yake hiyo jamii.

Sifa za Lugha
Zifuatazo ndizo sifa zinazojitokeza kwa kila lugha; sifa ambazo zinaihalalisha
lugha yo yote kuwa lugha na si vinginevyo.

(i) Lugha ni Lazima Imuhusu Mwanadamu
Kimsingi hakuna kiumbe kisicho mwanadamu (mtu) kinachoweza kuzungumza

lugha. Lugha ni chombo maalum wanachokitumia binadamu kwa lengo la

mawasiliano.

(ii) Sauti
Lugha huambatana na sauti za binadamu kutoka kinywani mwake binadamu

lazima atamke jambo kwa sauti.

(iii) Lugha Huzingatia Utaratibu Maalum
Lugha ni Sauti Zenye Utaratibu Maalumu

Sauti za lugha yoyote huwa zimepangwa kwa kufuata utaratibu fulani

unaokubaliwa na jamii hiyo ya watu. Kwa maneno mengine si kila sauti itokayo

kinywani mwa mwanadamu ni lugha. Mtoto anapolia hatusemi

anaongea au anazungumza. Utaratibu huo huitwa sarufi.

Mfano:

(a) Hatusemi
(i) John embe ana [joniembeana] au [joninaembea].

(ii) Kisu changu mimi nimepoteza
[kisuchangumiminimepoteza]

(b) Jamii imepatana kusema
(i) John ana embe [jonianaembe]

(ii) Mimi nimepoteza kisu changu
[miminimepotezakisuchangu]

(iv) Lugha Hufuata Misingi ya Fonimu
Lugha ina vitamkwa/vipashio ambavyo huitwa fonimu. Wana-Isimu wanakubaliana

kwa ujumla kwamba fonimu ni sauti yenye uwezo wa kuleta tofauti katika

maana ikipachikwa katika neno la lugha husika. Fonimu itazungumziwa kwa kirefu

katika Mhadhara wa Tatu.

Kwa mfano, baadhi ya fonimu za Kiswahili ni:
· /a/, /e/, /i/, /o/, /u/,
Katika: [tata] ~ [teta] ~ [tita] ~ [tota] ~ [tuta].

· /p/, /b/, /t/, /d/, /c/, / ɟ /, /k/, /g/, /s/, /z/, nk.
Katika:

pawa~bawa~tawa~dawa~chawa~jawa

kawa~gawa~sawa~zawa, nk.

(v) Lugha Hufuata Mpangilio wa Vipashio Unaoleta Maana
Muundo wa Lugha inayohusika kwa mujibu wa mpangilio wa vipashio vyake lazima ufahamike. Mpangilio huo huanza na fonimu, neno, kirai, kishazi, sentensi.

(vi) Lugha Inajizalisha
Vipashio vinavyoiunda lugha husika huwa na sifa ya kuweza kunyumbulishwa ili kupata maneno mapya. Kwa mfano, vitenzi hunyumbulishwa kwa

kuongezewa viambishi na kwa hiyo, lugha hujiongezea maneno mapya. Ona:

(i) chez-a => ku-chez-a => ku-m-chez-a > tu-li-m-chez-a.
(ii) chez-e-a=>chez-esh—a=> chez-esh-an-a => chez-esh-an-ik-a.

(iii) chez-e-a =>chez-ek-a.

(vii) Lugha Husharabu

Lugha husharabu kwa maana ya kwamba lugha huchukua maneno kutoka

lugha nyingine ili kujiongezea msamiati wake. Tabia hii inazisaidia sana lugha zinazokua. Lugha husharabu kwa namna mbili ambazo ni kuchukua na kutohoa

(i) Kuchukua hutokea pale lugha inapojiongezea maneno toka lugha nyingine

na kuyatumia kama yalivyo. Uchukuaji hutokea kwa lugha zinazoendana kisarufi

kama Kiswahili na lugha za Kibantu.

(ii) Kutohoa hutokea pale lugha inapoyachukua maneno toka lugha nyingine

na kuyarekebisha kimaandishi na kimatamshi ili yaendane na sarufi ya lugha

inayotohoa mf Kiswahili na Lugha za kigeni.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)