MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI : KUNANI?

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI : KUNANI?
#1
Kunani huko jamani, nauliza nambieni,
Kunani humo vichwani, mtoapo mawazoni,
Kunani humo vitini, enzi yenu mketini,
Kwa kiti Cha kuzunguka, ninauliza kunani?


Kunani majaridani, mema’nu ndiyo foleni,
Kunani huko jamvini, vibaya vi daharauni,
Kunani mwenu kinywani, vizuri vi ahadini,
Kwa kiti cha kuzunguka, ninauliza kunani?


Kunani mkutanoni, mwatuzuga akilini,
Kunani mwenu machoni, jema mbona silioni,
Kunani kwenu ndimini, au nd’o sumu sirini,
Kwa kiti Cha kuzunguka, ninauliza kunani?


Kunani kwenu nyumbani, mbona njaa siioni,
Kunani kwetu jamani, mbona Kama jalalani,
Kunani barabarani, Shida kwenu sizioni,
Kwa kiti Cha kuzunguka, ninauliza kunani?


Kunani kwenu tumboni, kwani yamevimbia’ni,
Kunani kwangu mwilini, kwani ninakondeani,
Kunani kwangu jamani, Uhuru u mafichoni,
Kwa kiti cha kuzunguka, ninauliza kunani?


MTUNZI;
Kingamkono, Enock,
(UDOM)
0764914583
enockkingson97@gmail.com

Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)