MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
UHAKIKI WA DIWANI YA MASHAIRI YA CHEKA CHEKA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
UHAKIKI WA DIWANI YA MASHAIRI YA CHEKA CHEKA
#1
UHAKIKI WA DIWANI YA MASHAIRI YA CHEKA CHEKA
MWANDISHI: Theobald A. Mvungi
MCHAPISHAJI: EDP
MWAKA : 1995
UTANGULIZI
MASHAIRI YA CHEKA CHEKA ni diwani inayoongelea masuala hayo ni pamoja na uongozi mbaya,mapenzi duni,Ukombozi.Mwandishi Theobald Mvungi amejadili kuwa kwa kinamasuala ya hayo na alipoanza alipendekeza namna ya kukubaliana nayo;mfano katika shairi la CHANZO CHA HUO UOZOamewashauri viongozi wa dini kuhimiza waumini watende matendo mema na wamrudie Mungu badala ya kuhimiza michango kwa ujumla Mvungi ametoa mchango mkubwa katika kujenga jamii mpya.
MAUDHUI
Maudhui ni mawazo yanayozungumzwa na msanii wa kazi ya kifasihi pamoja mtazamo wa mwandishi au msanii juu ya mawazo hayo.
   A)DHAMIRA
  1.  UKOMBOZI
Mwandishi anazungumzia suala la ukombozi kisiasa ambapo kupitia shairi lake la TAIFA WAMELIZIKA,msanii anaonyesha namna wananchi wasivyo na uhuru katika masuala mbalimbali,msanii anasema;
Ni sera zao tukufu, hangaiko la raia
Hao ndio maarufu, wajua kuhutubia,
Wajumbe mshiriki, katika huo uovu,
Pia mshauri anaendelea kusema kuwa hakuna demokrasia ya kweli kwani watu wanaamriwa kila jambo kama ubeti huu usemavyo,
Mezikwa demokrasia,chama kimoja ndio ngao
Watu hawana nafasi,kutetea nchi yao.
Mawazo ya ukakasi, mawazo ya mtitio,
Wapenda jibu mkato, wale waongo wa hoja.
Aidha mwandishi anaeleza kuwa ukombozi wa kweli utatekelezwa endapo kutakuwa na mshikamano wa dhati baina ya viongozi na wananchi, msanii amedhihirisha hayo kupitia shairi la MWINYI UMEWASHA MOTO:Angalia usizimwe.Hapa mshairi anaeleza kuwa wananchi wanategemea viongozi katika kuleta maendeleo, viongozi ni dira hivyo wapaswa wawe mstari wa mbele kwenye mambo ya maendeleo.
Kwa suala la ukombozi kiuchumi mshairi anasema ni vigumu kupata maendeleo kama viongozi wataendelea kutumia madaraka kwa manufaa yao binafsi kama shairi la MTOTO ASO RIZIKI lisemavyo;
Taifa wamelizika,mali zetu wamepora,
             Tena hawa wasifika,tunawapigia kura,
              Kwa hotuba wasifika,vitabu sura kwa sura,
              Uchafu ulivyojaa,dawa maji ya tufani
  1. MAPENZI
Mwandishi amejadili dhamira hii kupitia mashairi mbali mbali kama vile NJIWA KIUMBE MTINI,katika shairi hili mshairi anasema katika mahusiano ya kimapenzi kuna umuhim wa watu kuchnguzana na kupeana muda kwani papara husababisha watu kutoa majibu yasiyo sahihi na kama mtu ana mapenzi ya dhati hatakata tamaa asumbuliwapo na ampendaye.Katika ubeti huu msanii asema;
                 Matawi mkiyakwea,njia arukie kule,
                 Si kwamba anakimbia, ni mbinu zake teule,
                 Tabu kaniongezea,hata chakula nisile,
Vivyo hivyo katika shairi la PENZI LISILO HESHIMA,mshairi anaonyesha namna  mapenzi ya siku hizi yalivyogeuzwa bidhaa;
Penzi la umaskini, kwa hii yetu dunia
Ni penzi la nuksani,mpendwa hatapokea,
Mpendwa hamuelewani,kwa maneno ya kumwambia,
Mfukoni huna kitu,mpenda tahangaika.
  1. DEMOKRASIA
Mwandishi amejadili suala la kidemokrasia katika shairi la TAIFA WAMELIZIKA ambapo wanawatumia wakunga na wajumbe mbalimbali wahudhurie vikao mbalimbali vya kujadili masuala ya nchi,lakini wao wasiende kupiga porojo na kufanya mawazo ya wachache bali wawasilisha mawazo ya wananchi  Lakini Wabunge na wajumbe husinzia wawapo mikutanoni badala ya kuchangia hoja zenye kuleta tija kwa wananchi wanaowakalisha majumbani wengi hujali posho zao matokeo yake mawazo ya wananchi hupuuzwa. kama ubeti huu usemavyo;
Mezikwa demokrasia,chama kimoja ndio ngao,
Watu hawana nafasi,kutetea nchi yao,
Mawazo ya ukakasi,mawazo ya mtitio,
 Wapenda jibu mkato,wale waongo wa hoja.
Msanii anawataka viongozi wakumbuke kutekeleza majukumu au wajibu  wao kwa ufanisi na sio kwenda kusinzia wawapo mikutano kwani wao ni wawakilishi wa watu wao.
4.MATUMIZI MABAYA YA MALI YA UMMA
Katika shairi la GUNIA LA MIKUTANO,mwandishi ameonyesha namna ambavyo viongozi wengi hutumia fedha za umma kinyume na utaratibu. mfano; kujilipa posho wawapo vikaoni,hata vikao visivyo vya ulazima.Aidha huandaa sherehe mbalimbali zinazohitaji fedha nyingi na ambazo haziwanufaishi wananchi.msanii anasema;
Sherehe zenye utamu,raha ya wachache humu,
Ni mateso kwa kaumu, wasoweza kujikimu,
Sherehe si kipaumbele, mwelekeo uwe kazi
  1.  UZEMBE NA UKASUKU
Katika shairi la NI WAPI USHAURI msanii anakemea uzembe na kwamba watu hawafanyi kazi kwa kujituma bali wanataka wasukumwe,kwa mtazamo wake msanii anaona kufanya kazi kwa kusukumwa ni kama utumwa.Msanii anadhihirisha hili kwa kuwatumia wanaohusika na usafirishaji mazao toka kwa wakulima ambao huzembea na kufanya mazao yaoze mashambani ambapo hali hii huwakatisha tama wakulima ya kuendelea na kilimo.Msanii anasema;
Wanawe idadi sita,wakulima maarufu,
Pamba mahindi ufuta,tena wana watiifu,
                             Fedha wanazitafuta,wanunue maradufu
Mazao yamo nyumbani,hayana mnunuzi.
Pia katika shairi la TUAMBAE UKASUKU mwandishi anawaasa watu wanaoishi maisha yakufuata mkumbo kuwa maisha ya namna hiyo hayafai. Katika maisha mtu anatakiwa kuangalia jambo gani lina manufaa na lipi halina,lile lenye manufaa lifuatwe kwa lengo la kuboresha maisha.Hapa msanii anawazungumzia washairi kuwa watunge mashairi yenye lengo la kuleta maendeleo siyo kuwasifia viongozi wafanyapo mambo yasiyofaa kuwasifia.Mwandishi anaona kuwa mshairi bora ni yule anayesema ukweli asiyekubali kuwa kibaraka.Mwandishi  anasema;
Mshairi uwe huru,upige yako mafumbo,
Usiwe kama kunguru,woga umejaa tumbo,
Na usitoze ushuru,hapo utakwenda kombo,
Wataka wanyonge,so wale waheshimiwa.
Mwandishi anawataka waandishi na jamii kwa ujumla waishi kama vile walivyo na si kuishi maisha ya kuigiza kwa lengo la kuwafurahisha watu fulani.
6. DINI
Mwandishi katika diwani yake amezungumzia upotofu unaojitokeza kwenye madhehebu yetu ya dini.mfano; Dini ya kikristo madhehebu ya wakatoliki na walutheri viongozi huimiza sana michango badala ya kuimiza matendo mema kwa waumini.Watu wanatakiwa kumrudia Mungu na kuacha dhambi,kuhimiza upendo na mshikamano badala ya kutenda hayo waumini hujazwa chuki kwa kurundukiwa michango.Msanii anasema;
Nimechunguza kanisa,luteri na katoliki,
Viongozi nawaasa,roho hazimpi chuki,
Zile ibada za misa,watu wanajazwa chuki,
Padri hanalo jambo,ila kudai michango.
kupitia ubeti huo mwandishi wa shairi la CHANZO CHA HUO UOZO anaonesha namna maana ya dini inavyopotoshwa watu wanachukizwa na kuchoshwa na michango na kuona kanisa kama sehemu ya maudhi badala ya faraja.Mwandishi anawataka viongozi wa dini kuwasaidia waumini wao waende mbinguni na sio kudai michango pekee.
  1. SUALA  LA UONGOZI
Mwandishi amejadili suala la uongozi kwa kuonesha namna viongozi wetu wengi wasivyo wasikivu na kutotekeleza wajibu wao.Mwandishi ameonesha namna ambavyo viongozi wengi wanavyoweka ahadi ambazo hazitekelezwi,ahadi zao ni za kutaka madaraka wakati wa kampeni za uchaguzi.katika shairi la MTOTO ASO RIZIKI mwandishi ameonesha namna viongozi wanzvotusaliti.Msanii anasema;
Wasalitiwa mbali, wala si waamerika
Ni hawana wala mali, hatamu walioshika,
Weusi kwa kila hali, madaraka waloshika,
Si wote hilo ni wazi, lakini ni wamo wengi.
Katika shairi la MASHAIRI YA NGULU mwandishi ameonesha namna viongozi wanavyojipendelea na kufanya dhuluma kwa wananchi,wakulima na wafanyakazi hawatendewi haki wanadhulumiwa mazao na mishahara yao.Msanii anasema;
Diwani unasaili,falsafa za kukwama,
Uongozi usojali,taabu za wakulima,
Wale wasio na hali,wanarudishwa nyuma,
Waporwa mazao yao,kwa hoja za ulaghai.
                        
                      Tazama mfanyakazi,mshahara wa mwezi,
                       Utani wa uchochezi,hautoshi hata nazi
                       Ni vipi asiwe mwizi,nani asiye mwizi?
                       Ujira wa moja juma, ati ndo wa wote mwezi.
Katika ubeti huo hapo juu mwandishi ametoa mfano wa dhuluma hizo wanazofanyiwa wakulima kwa kulaghaiwa bei wauzapo mazao yao (bei hailingani na thamani ya mazao). Pia wafanyakazi wanapata mishahara midogo ambayo haikidhi mahitaji yao na ndiyo maana wengi wanapokea rushwa katika utendaji wao.
 Vivyo hivyo katika shairi la MUWAPI NAWAULIZA msanii ameeleza namna viongozi wanavyolala na kuacha baadhi ya watu kufanya watakavyo. kwa mfano; Wafanyabiashara kupanga bei za mazao  ya wakulima watakavyo kwa madai kuwa biashara ngumu,Aidha wauzapo huuza kwa bei wazipendazo eti biashara huria.
Katika shairi la RAIA SI MALI KITU Mshairi ameonesha kuwa viongozi hawashirikishi wananchi katika kutoa maamuzi, mambo mengine huamuliwa na viongozi na wananchi wanaambiwa tu kutekeleza.
 Mwandishi anawataka viongozi kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi hasa ahadi wanazoahidi pindi wanapotaka uongozi.
      FANI
  1.  MUUNDO
Mwandishi amegawa mashairi katika makundi mawili, mashairi ya kawaida na tena ambapo aina zote kwa kuzingatia beti, vina, mizani na vituo.
Kwa upande wa beti yapo mashairi yenye beti nyingi na yenye beti beti chache. Mashairi yenye beti nyingi ni pamoja na LAZIMA WAUMINI  lenye beti 10, RAIA SI MALI KITU lenye beti 9 na yenye beti chache ni KIMOYO lenye beti 4.
Mizani,mwandishi ameunga mkono mashairi kwa idadi ya mizani ambapo mashairi ya kawaida yana mizani 16 kwa mgao wa 8¤8kwa kila shairi, mfano shairi la MWENYEWE UMEWASHAMOTO.
                   Hao wamekuzunguka,walaji hawako mbali,
                   Vipigo vimetukuka,ndilo jina la awali,
                   Hawa ndio wasifika,kwa hidhini na vibali,
                   Usoni tadhani watu,lo aheri mbwa mwitu,
Kwa upandewa ametumia mizani nane (8) kwa kila shairi, mfano shairi la SENG’ENGE
                    Nipishe wewe seng’enge,
                   Nipishe kando jitenge,
                   Nipishe usinifunge,
                   Usiwe haambiliki
Vina,kwenye mashairi ya kawaida kuna vina vya kati na mwisho.Mfano shairi la CHATU MMEZA MATONGE.
                   Sipendi yanatokea, shirika macho kufumba,
                   Kukataa kusikiya, ya wapangaji wa nyumba,
                   Watu walifikia, shirika la nyumba,
                   Ndilo kimbilio lao, hawa wavuja majasho
Katika ubeti huo kuna vina vya kati “a” na vina vya mwisho ni“mba” na upande wa tenzi huwa  na vina vya mwisho. Mfano utenzi wa INDIRA
                   Sifazo kwa jitihada,
                   Tuishi kwa kawaida,
                   Kwetu ukawa ushuhuda,
                   Takukumbuka daima.
Vituo,mwandishi ametunga mashairi yenye vituo vitoshelezi kwakuwa katika mashairi yake yote kila ubeti una kituo chake
2.  MTINDO
Mwandishi  katika mashairi yake yote yamezingatia urari wa vina na mizani, pia ametumia mtindo na maelezo yaani anaelezea ufahamu alionao juu ya jambo analozungumzia.Aidha ametumia mtindo wa nafsi ambapo nafsi karibu zote zimetumika. Mfano
-“Mwinyi amewasha moto” (U-nafsi ya pili umoja-wewe),
-“Tuambae ukasuku” (Tu-sisi nafsi ya kwanza wingi),
– “lazima mniamini (nyinyi- nafsi ya pili wingi) n.k.
3.  LUGHA
Mshairi ametumia vipengele mbalimbalivya lugha ili kuifanya kazi yake na mvuto wa kueleweka kwa hadhira, baadhi ya vipengele hivyo ni :-
4. TASWIRA/ PICHA
Mshairi ametumia taswira mbalimbali yani zahisi,au za kuonekana.Mfano;
 -Shairi la KUNA NINI HUKO NDANI inamaanisha matumizi mabaya ya madaraka ),
– CHATU MMEZA MATONGE linamaanisha matumizi mabaya ya mali za umma, GUNIA LA MIKUTANO (ufugaji wa fedha)
METHALI
Mshairi ametumia baadhi ya methali katika mashairi yake mfano
–Taratibu ndio mwendo, katika shairi la MOYO,
–Umoja ni nguvu, katika shairi la KAZI ZETU HARAKATI.
TAMATHALI ZA SEMI
Mwandishi ametumia tamathali za semi mbalimbali ili kuongeza mvuto kwenye kazi yake, mfano
  Ø Tashibisha
Ni tamathali inayolinganisha vitu viwili au zaidi kwa kutumia viunganishi.mfano katika shairi la LAZIMA MNIAMINI mandishi anasema;
                   Mlevi akakolea,kama tumbaku ya tozo
Miguu ikalegea, katika kuchezacheza,
                   Kaziongeza bia, watu wakatumbuiza,
                   Watoto wakirimu,mradi kiitikio,
vile vile katika shairi la MOYO mwandishi anasema;
                   Moyo nimeushauri, lakini umekaidi,
                   Moyo kiburi hatari, mfanowe kama radi,
                   Moyo mefumbata shairi, unayakwepa maradi,
                   Moyo mwilini mwangu,jiradi tuwe pamoja
  Ø Sitiari
Ni tamathali inayounganisha vitu pasipo kutumia viunganishi.Mfano katika shairi la INDIRA Mwandishi anasema;
                   Mwenzetu Gandi kwaheri,
                   Moyo hutuna shwari,
                   Machozi yetu bahari,
                   Gandhi ulitudhamini.
Aidha katika shairi la UTU UMEKUWA KIMA mwandishi anasema;
                   Dhuluma ndio hekima,
                   Utu umekuwa kima,
                   Hafai huyo mnyama,
                   Jumlaye ni uhuru.
  Ø Tashihisi
Ni tamathali ivipavyo uwezo vitu visivyo binadamu kutenda matendo ya binadamu. mfano, katika shairi la NJIWA KIUMBE MTINI mwandishi anasema;
                   Mmejaribu kujongea,ndege awe mkononi,
                   Yeye juu hurukia, na muomba samahani,
                   Nyimbo anaziimba, nyimbo zachoma moyoni,
                   Basi mie kaabani, njiwa akitabasamu.
Katika shairi ubeti huo njiwa amepewa uwezo wa kumwimbia mwanadamu nyimbo kuomba msamaha na kutabasamu.Matendo hayo kiuhalisia yanatakiwa yatendwe na watu sio ndege (njiwa).
Katika shairi la MOYO unaambiwa uache jeuri na ukaidi na ujifunze busara.
MKATO WA MANENO
Baadhi ya maneno yamekatwa katika diwani hii ili kupata urari wa mizani na vina.Mfano maneno asotaka badala ya asiyetakana walojonea baala ya waliojionea, katika shairi la LAZIMA MNIAMINI na katika shairi la MOYO mwandishi anasemamekuwa badala ya imekuwa.
 
Kwa ujumla Mwandishi amejitahidi sana kutumia utenzi na utumizi wa lugha na hivyo kufanya kazi yake iwe na mvuto.

Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)