MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MOFOLOJIA YA KISWAHILI: MUHADHARA WA TATU: DHANNA YA ALOMOFU

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
MOFOLOJIA YA KISWAHILI: MUHADHARA WA TATU: DHANNA YA ALOMOFU
#1
MUHADHARA WA TATU: DHANNA YA ALOMOFU
Alomofu  hufafanuliwa kama maumbo zaidi ya moja (mbalimbali) ya mofimu moja.
Neno alomofu linatokana na maneno mawili ambayo ni “alo” lenye maana ya zaidi ya moja au mbalimbali na “mofu” lenye maana ya umbo (ma)
Mfano
  • M(u)+tu : wa+tu
  • M(u)+ke : wa+ke
  • Mw+alimu : w+alimu
  • mw+anajeshi : w+anajeshi
Katika mifano hiyo //mu// ya umoja ina maumbo mawili ambayo ni //m// na  //mw// halikadhalika //wa// ya wingi nayo ina maumbo mawili ambayo ni  //wa// na  //w//  hivyo maumbo haya yanaweza kuelezwa kwa kanuni ifuatayo:
//mu//——->[m]/-k
——->[mw]/-I
//wa//——–>[wa]/-k
— ——->[w]/-I
MAZINGIRA YA UTOKEAJI wa ALOMOFU
Alomofu hutokea katika mazingira maalumu. Mazingira mengine yanatabirika na mengine hayatabiriki. Hata hivyo, alomofu huweza kutokea katika mazingira ya aina tatu ambayo ni:,
v    mazingira ya kifonolojia
v    mazingira ya kileksika (kikamusi)
v    mazingira ya kisarufi
  1.  Mazingira ya kifonolojia
    Mazingira ya kifonolojia ya utokeaji wa alomofu hujitokeza pale ambapo maumbo fulani hutokea kama alomofu kutokana na athari za kifonolojia.
      Mfano
[Image: SAM_1502.JPG]
Mifano hiyo inaonesha jinsi umbo moja linavyoweza kubadilika na kuwa katika muonekano tofauti huku maumbo yote hayo yakiendelea kubeba taarifa ileile. Mabadiliko haya huwa yamesababishwa na athari za kifonolojia za sauti fulani.
Umbo  “mu” linatokea kama //mu// au //m// linapofuatwa na konsonanti na linakuwa  umbo //mw// linapofuatwa  na irabu.
Vilevile umbo //wa// linalojitokeza kama //wa// linapofuatwa na konsonanti  na linakuwa //w// linapofuatwa na irabu.
Vilevile mazingira ya kifonolojia hujidhihirisha katika utendaji. Utokeaji wa alomofu za kauli huwa katika mazingira yanayotabirika na yasiyotabirika.
  • Mazingira yanayotabirika ya utendea
[Image: SAM_1503.JPG]
[Image: SAM_1504.JPG]
Mofimu ya utendea “le” inatokea iwapo mzizi una irabu e au o.
Mazingira ya utokeaji wa alomofu ya utendeshi.
  • Mazingira yasiyotabirika
Mfano
  1. a) lala-laza
  2. b) shuka-shusha
  3. c) lewa-levya
  4. d) ogopa-ogofya
  5. e) gawana-gawanya
Alomofu za utendeshi ni z, sh, vy, fy, ny.
2  Mazingira ya kileksika
Utokeaji wa alomofu katika mazingira ya kileksika huwa tunazingatia ngeli za nomino kupitia mofu za umoja na wingi za nomino husika.
Mfano
  1. a) kijana   vijana
  2. b)  mtume     mitume
  3. c)  θRaisi    maraisi
  4. d)  θMungu    θMungu
Katika mifano hiyo;
  • Alomofu za umoja ni ki,m,θ
  • Alomofu za wingi ni,vi,mi,ma,θ
//umoja//—-> ki /-konsonanti
//wingi//—-> vi/-k
//umoja//—–>m/-k
//wingi// —->mi/-k
//umoja//—->  /-raisi
//wingi//—–> ma/-raisi
//umoja//—–> θ/-Mungu
//wingi//——> θ/-Mungu
  1. Mazingira ya kisarufi
Mfano
  1. a) anapika – hapiki
  2. b) alipika – hakupika
  3. c) atapika – hakupika
  4. d) amepika – hajapika
(i) Alomofu za njeo ni:-na, li, ta, me, i, ku, ja
(ii) Alomofu za njeo uyakinishi ni; na, li, ni, ta, me
(iii) Alomofu za njeo ukanushi ni; i, ku, ta, ja
VIGHAIRI
Vighairi ni dhanna inayohusu alomofu ambazo utokeaji wake   haufungamani na kanuni wala masharti yoyote.
Mifano
(a) ki+tabu  –  vi+tabu
(b) ki+jiko  –  vi+jiko
© ki+nu    –  vi+nu
(d) ch+umba  –  vy+umba
(e) ch+eti   –  vy+eti
(f) ki+oo    –  vi+oo
(g) ch+oo    – vy+oo
(h) ch+umba  – vy+umba
Mifano hiyo //ki// ya ngeli ya KI-VI umoja ina alomufu //ki// na //ch// na mofu //vi// ya wingi ina alomofu //vi// na //vy//.
NB: Maneno choo,vyoo, chumba, vyumba, chetu, vyetu, ni vighairi kwa sababu yanashiriki ngeli ya KI-VI lakini hayakubali mofu //ki// na //vi// kukaa mwanzoni. Kimsingi //ch// na //vy// zipo kwenye ngeli ya  KI-VI  lakini mwanzoni zipo zilivyo yaani, ki-vi itatokea tu kwenye kitenzi cha upatanisho wa kisarufi.
Mfano;   choo kimejengwa
Vyoo vimejengwa
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)